unfoldingWord 46 - Paulo Anakuwa Mkristo

unfoldingWord 46 - Paulo Anakuwa Mkristo

개요: Acts 8:1-3; 9:1-31; 11:19-26; 13-14

스크립트 번호: 1246

언어: Swahili

청중: General

장르: Bible Stories & Teac

목적: Evangelism; Teaching

성경 인용: Paraphrase

지위: Approved

이 스크립트는 다른 언어로 번역 및 녹음을위한 기본 지침입니다. 그것은 그것이 사용되는 각 영역에 맞게 다른 문화와 언어로 조정되어야 합니다. 사용되는 몇 가지 용어와 개념은 다른 문화에서는 다듬어지거나 생략해야 할 수도 있습니다.

스크립트 텍스트

Kijana Sauli ndiye alitunza nguo za wanaume waliomuua Stefano. Yeye hakuwa mfuasi wa Yesu. Kazi yake ilikuwa kuwatesa wakristo. Alizungukia kila kaya mjini Yerusalemu akiwakamata watu wa jinsia zote waliomwamini Yesu na kuwaweka gerezani. Mkuu wa makuhani alimpa kibali kwenda Dameski kuwakamata wafuasi wa Yesu na kuwaleta Yerusalemu.

Sauli alipokuwa akienda Damesiki, nuru kuu kutoka mbinguni ilimwangaza pande zote na akaanguka chini. Sauli alisikia mtu akisema, "Sauli! Sauli! Kwa nini unaniudhi?" Sauli alimuuliza" Wewe ni nani Bwana?" Jibu la Yesu lilikuwa, "Mimi ni Yesu unayeniudhi."

Sauli alipoamuka, hakuweza kuona. Waliokuwa pamoja naye ilibidi wampeleke Dameski. Alikaa siku tatu bila kula wala kunywa.

Huko Dameski alikuwapo mwanafunzi wa Yesu aliyeitwa Anania. Mungu alimwagiza, "Nenda katika nyumba ambamo anaishi Sauli. Weka mikono juu yake ili apate kuona tena." Bali Anania akajibu, "Bwana nimesikia jinsi mtu huyu anavyowaudhi wafuasi wa wako. "Mungu akamwambia, Nenda! Nimemchagua alitangaze Jina langu kwa Wayahudi na kwa watu kutoka Mataifa mengine. Naye atateseka sana kwa ajili ya jina langu."

Ndipo Anania alikaenda kwa Sauli, akamwekea mikono, akasema, "Yesu uliyekutana naye njiani wakati unakuja hapa, amenituma kwako ili upate kuona tena na ujazwe na Roho Mtakatifu". Mara akaweza kuona tena. Kisha Anania akambatiza, akala chakula na nguvu zake zikamrudia.

Mara hiyo, Sauli alianza kuhubiri Wayahudi katika Dameski akisema, "Yesu ni Mwana wa Mungu". Wayahudi walishangaa kuona mtu aliyekuwa akijitahidi kuwaangamiza wakristo amegeuka kuwa mfuasi wa Yesu! Sauli alibainisha kuwa Yesu ndiye Masihi.

Siku nyingi baadaye, Wayahudi walipanga kumuua Sauli. Waliwatuma watu kumfuatilia katika malango ya miji kwa lengo la kumwangamiza. Lakini Sauli aligundua mpango huo, na rafiki zake walimsaidia kutoroka. Usiku mmoja aliteremshwa akiwa ndani ya kikapu ukutani, akishatoroka kutoka Dameski aliendelea tu kuhubiri habari za Yesu.

Sauli alitembelea Yerusalemu, lakini wanafunzi wa Yesu walimhofu. Kisha muumuni aliyeitwa Barinaba alimpeleka kwa mitume kuwaeleza jinsi alivyo hubiri kwa ujasiri habari njema huko Dameski. Taarifa hiyo ilisababisha mitume wamkubali Sauli.

Baadhi ya waumini waliokimbia mateso huko Yerusalemu na kwenda mbali huko Antiokia, walizidi kuhubiri kuhusu Yesu. Wenyeji wengi wa Antiokia hawakuwa Wayahudi, hicho ndicho kipindi ambacho watu wa mataifa kwa mara ya kwanza waliipokea imani. Barinaba na Sauli walikwenda huko kuwafundisha hao waumini wachanga zaidi kuhusu Yesu na kulikomaza kanisa. Kwa mara ya kwanza wafuasi wa Yesu waliitwa Wakristo hapo Antiokia.

Hapo Antiokia, siku moja wakristo walipo kuwa katika maombi ya kufunga, Roho Mtakatifu aliwaambia nitengeeni Sauli na Barinaba wafanye kazi niliyo waitia. Hivyo kanisa liliwaombea na kuwawekea mikono, kisha wakawatuma waende maeneo mengine mengi kuhubiri habari njema za Yesu. Barinaba na Sauli walifundisha makundi ya watu wa matifa mbalimbali, watu wengi wakamwamini Yesu.

관련정보

생명의 말씀 - GRN 은 성경에 기반한 구원과 그리스도인의 삶에 대한 수천개의 오디오 복음 메시지를 가지고 있습니다.

무료 다운로드 - 여기에서 다운로드 가능한 여러 언어로 된 주요 GRN 메시지 스크립트, 그림 및 기타 관련 자료를 찾을 수 있습니다.

GRN 오디오 도서관 - 전도와 기본 성경 가르침을 위한 자료는 mp3, CD, 카세트 테이프 형태로 사람들의 필요와 문화에 맞추어졌습니다. 녹음은 성경이야기, 전도 메시지, 말씀 읽기, 노래를 포함하여 다양한 스타일로 구성되었습니다.

Copyright and Licensing - GRN shares it's audio, video and written scripts under Creative Commons

Choosing the right audio or video format - What audio and video file formats are available from GRN, and which one is best to use?