選擇語言

mic

分享

分享鏈接

QR code for https://globalrecordings.net/script/sw/1224

unfoldingWord 24 - Yohana Anambatiza Yesu

unfoldingWord 24 - Yohana Anambatiza Yesu

概要: Matthew 3; Mark 1; Luke 3; John 1:15-37

文本編號: 1224

語言: Swahili

聽眾: General

目的: Evangelism; Teaching

Features: Bible Stories; Paraphrase Scripture

狀態: Approved

腳本是翻譯和錄製成其他語言的基本指南,它們需要根據實際需要而進行調整以適合不同的文化和語言。某些使用術語和概念可能需要有更多的解釋,甚至要完全更換或省略。

文本文字

Yohana mwana wa Zakaria na Elizabeth alikuwa na akawa nabii .Aliishi nyikani akila asali ya porini, nzige ,na kuvaa nguo zilizotengenezwa na manyoya ya ngamia.

Watu wengi walimfuata Yohana nyikani kumsikiliza.Aliwahubiri akisema,"tubuni kwa maana ufalme wa Mungu umekaribia"

Wakati watu waliposikia ujumbe wa Yohana wengi walitubu dhambi zao na kubatizwa .Viongozi wengi wa dini walikuja kubatizwa na Yohana lakini hawakutubu wala kuungama dhambi zao .

Yohana akawaambia viongozi wa dini" enyi nyoka wenye sumu! tubuni na kubadilisha tabia zenu.Kila mti usiozaa matunda mema hukatwa na kutupwa motoni. Yohana alitimiza kile kilichosemwa na manabii "angalia namtuma mjumbe wangu mbele yenu ambaye atawandalia njia zenu."

Baadhi ya Wayahudi wakamwuuliza Yohana kama yeye ni Kristo ,Yohana akajibu mimi siyo Kristo lakini kuna mmoja ajaye baada yangu ambaye ni mkuu sanakwani sistahili kufungua kamba ya viatu vyake .

Siku iliyofuata Yesu alikuja ili abatizwe na Yohana .Wakati alipomwona Yohana alisema,'angalia huyu ni mwanakondoo wa Mungu atakayechukua dhambi ya ulimwengu.

Yohana akamwambia Yesu mimi sistahili kukubatiza wewe ila wewe unastahili kunibatiza mimi.Lakini Yesu akasema "ni lazima kunibatiza mimi kwa sababu ni kitu sahihi kwa hiyo Yohana akambatizaYesu pamoja na kwamba Yesu hakuwahi kutenda dhambi.

Wakati Yesu alipotoka majini baada ya kubatizwa Roho wa Mungu alitokea katika umbo la njiwa alishuka akatulia juu yake.Wakati huo sauti ya Mungu ikaongea kutoka mbinguni na kusema "Wewe ni mwanangu ambaye ninakupenda na ninayependezwa naye ".

Mungu akamwambia Yohana," Roho wa Mungu atakuja juu ya mtu ambaye umembatiza .Na mtu huyo ni mwana wa Mungu ,"Kuna Mungu mmoja tu.Lakini wakati Yohana alipokuwa akimbatiza Yesu alisikia Baba Mungu akisema na akamuona Mungu mwana ,ambaye ni Yesu ,na akamwona Roho Mtakatifu.

相關信息

生命之道 - 環球錄音網擁有用數以千計的語言去錄製的福音信息,內容包括一些有關救恩和基督徒樣式的聖經信息。

Copyright and Licensing - GRN shares its audio, video and written scripts under Creative Commons

Choosing the audio or video format to download - What audio and video file formats are available from GRN, and which one is best to use?