unfoldingWord 11 - Pasaka

Тойм: Exodus 11:1-12:32
Скриптийн дугаар: 1211
Хэл: Swahili
Үзэгчид: General
Зорилго: Evangelism; Teaching
Features: Bible Stories; Paraphrase Scripture
Статус: Approved
Скрипт нь бусад хэл рүү орчуулах, бичих үндсэн заавар юм. Тэдгээрийг өөр өөр соёл, хэл бүрт ойлгомжтой, хамааралтай болгохын тулд шаардлагатай бол тохируулсан байх ёстой. Ашигласан зарим нэр томьёо, ухагдахууныг илүү тайлбарлах шаардлагатай эсвэл бүр орлуулах эсвэл бүрмөсөн орхиж болно.
Скрипт Текст

Mungu alimuonya Farao ikiwa hatawaruhusu Waisraeli kuondoka, ya kuwa atawaua wazaliwa wa kwanza wote wa kiume wa watu wa Misri na wa wanyama. Baada ya kusikia hayo Farao aliendelea kutomwamini wala kumtii Mungu.

Mungu alifanya njia ya kuwaokoa wazaliwa wa kwanza wa kiume kwa yeyote atakayemwamini Yeye. Kila nyumba ya Israeli ilipaswa kuchagua mwanakondoo aliye mkamilifu na kumchinja.

Mungu aliwaelekeza Waisraeli kupaka damu ya Mwanakondoo kwenye milango yao, kuichoma nyama ya Mwanakondoo na kuila kwa haraka pamoja na mikate isiyowekewa amira. Vile vile Mungu aliwaambia mara baada ya kula wawe tayari kuondoka Misri.

Waisraeli walitimiza yote waliyoagizwa na Mungu. Usiku wa manane Mungu alipita juu ya Wamisri wote na kuwaua wazaliwa wao wote wa kwanza wa kiume.

Nyumba zote za Waisraeli zilipakwa damu katika milango yake, hivyo Mungu alipita juu ya nyumba zao. Katika nyumba hizo wote waliokolewa. Walipona kwa sababu ya damu ya Mwanakondoo.

Wamisri hawakuamini wala kutii maelekezo ya Mungu. Hivyo basi Mungu hakupita juu ya nyumba zao. Akawauwa wazaliwa wao wa kwanza wa kiume.

Kila mzaliwa wa kwanza wa kiume wa Wamisri alikufa, tangu mzaliwa wa kwanza wa aliyekuwa gerezani mpaka mzaliwa wa kiume wa kwanza wa Farao. Wengi walilia na kuomboleza kwa ajili ya huzuni kubwa iliyowapata.

Usiku ule ule, Farao aliwaita Musa na Haruni na kuwaambia, "wachukueni Waisraeli muondoke haraka." Hata Wamisri pia waliwasihi Waisraeli watoke haraka.