unfoldingWord 11 - Pasaka

Muhtasari: Exodus 11:1-12:32
Nambari ya Hati: 1211
Lugha: Swahili
Hadhira: General
Kusudi: Evangelism; Teaching
Features: Bible Stories; Paraphrase Scripture
Hali: Approved
Hati ni miongozo ya kimsingi ya kutafsiri na kurekodi katika lugha zingine. Yanafaa kurekebishwa inavyohitajika ili kuzifanya zieleweke na kufaa kwa kila utamaduni na lugha tofauti. Baadhi ya maneno na dhana zinazotumiwa zinaweza kuhitaji maelezo zaidi au hata kubadilishwa au kuachwa kabisa.
Maandishi ya Hati

Mungu alimuonya Farao ikiwa hatawaruhusu Waisraeli kuondoka, ya kuwa atawaua wazaliwa wa kwanza wote wa kiume wa watu wa Misri na wa wanyama. Baada ya kusikia hayo Farao aliendelea kutomwamini wala kumtii Mungu.

Mungu alifanya njia ya kuwaokoa wazaliwa wa kwanza wa kiume kwa yeyote atakayemwamini Yeye. Kila nyumba ya Israeli ilipaswa kuchagua mwanakondoo aliye mkamilifu na kumchinja.

Mungu aliwaelekeza Waisraeli kupaka damu ya Mwanakondoo kwenye milango yao, kuichoma nyama ya Mwanakondoo na kuila kwa haraka pamoja na mikate isiyowekewa amira. Vile vile Mungu aliwaambia mara baada ya kula wawe tayari kuondoka Misri.

Waisraeli walitimiza yote waliyoagizwa na Mungu. Usiku wa manane Mungu alipita juu ya Wamisri wote na kuwaua wazaliwa wao wote wa kwanza wa kiume.

Nyumba zote za Waisraeli zilipakwa damu katika milango yake, hivyo Mungu alipita juu ya nyumba zao. Katika nyumba hizo wote waliokolewa. Walipona kwa sababu ya damu ya Mwanakondoo.

Wamisri hawakuamini wala kutii maelekezo ya Mungu. Hivyo basi Mungu hakupita juu ya nyumba zao. Akawauwa wazaliwa wao wa kwanza wa kiume.

Kila mzaliwa wa kwanza wa kiume wa Wamisri alikufa, tangu mzaliwa wa kwanza wa aliyekuwa gerezani mpaka mzaliwa wa kiume wa kwanza wa Farao. Wengi walilia na kuomboleza kwa ajili ya huzuni kubwa iliyowapata.

Usiku ule ule, Farao aliwaita Musa na Haruni na kuwaambia, "wachukueni Waisraeli muondoke haraka." Hata Wamisri pia waliwasihi Waisraeli watoke haraka.