unfoldingWord 11 - Pasaka
![unfoldingWord 11 - Pasaka](https://static.globalrecordings.net/300x200/z02_Ex_12_02.jpg)
Kontuur: Exodus 11:1-12:32
Skripti number: 1211
Keel: Swahili
Publik: General
Žanr: Bible Stories & Teac
Eesmärk: Evangelism; Teaching
Piibli tsitaat: Paraphrase
Olek: Approved
Skriptid on põhijuhised teistesse keeltesse tõlkimisel ja salvestamisel. Neid tuleks vastavalt vajadusele kohandada, et need oleksid arusaadavad ja asjakohased iga erineva kultuuri ja keele jaoks. Mõned kasutatud terminid ja mõisted võivad vajada rohkem selgitusi või isegi asendada või täielikult välja jätta.
Skripti tekst
![](https://static.globalrecordings.net/300x200/z02_Ex_10_12.jpg)
Mungu alimuonya Farao ikiwa hatawaruhusu Waisraeli kuondoka, ya kuwa atawaua wazaliwa wa kwanza wote wa kiume wa watu wa Misri na wa wanyama. Baada ya kusikia hayo Farao aliendelea kutomwamini wala kumtii Mungu.
![](https://static.globalrecordings.net/300x200/z02_Ex_12_01.jpg)
Mungu alifanya njia ya kuwaokoa wazaliwa wa kwanza wa kiume kwa yeyote atakayemwamini Yeye. Kila nyumba ya Israeli ilipaswa kuchagua mwanakondoo aliye mkamilifu na kumchinja.
![](https://static.globalrecordings.net/300x200/z02_Ex_12_02.jpg)
Mungu aliwaelekeza Waisraeli kupaka damu ya Mwanakondoo kwenye milango yao, kuichoma nyama ya Mwanakondoo na kuila kwa haraka pamoja na mikate isiyowekewa amira. Vile vile Mungu aliwaambia mara baada ya kula wawe tayari kuondoka Misri.
![](https://static.globalrecordings.net/300x200/z02_Ex_12_03.jpg)
Waisraeli walitimiza yote waliyoagizwa na Mungu. Usiku wa manane Mungu alipita juu ya Wamisri wote na kuwaua wazaliwa wao wote wa kwanza wa kiume.
![](https://static.globalrecordings.net/300x200/z02_Ex_12_04.jpg)
Nyumba zote za Waisraeli zilipakwa damu katika milango yake, hivyo Mungu alipita juu ya nyumba zao. Katika nyumba hizo wote waliokolewa. Walipona kwa sababu ya damu ya Mwanakondoo.
![](https://static.globalrecordings.net/300x200/z02_Ex_12_05.jpg)
Wamisri hawakuamini wala kutii maelekezo ya Mungu. Hivyo basi Mungu hakupita juu ya nyumba zao. Akawauwa wazaliwa wao wa kwanza wa kiume.
![](https://static.globalrecordings.net/300x200/z02_Ex_12_06.jpg)
Kila mzaliwa wa kwanza wa kiume wa Wamisri alikufa, tangu mzaliwa wa kwanza wa aliyekuwa gerezani mpaka mzaliwa wa kiume wa kwanza wa Farao. Wengi walilia na kuomboleza kwa ajili ya huzuni kubwa iliyowapata.
![](https://static.globalrecordings.net/300x200/z02_Ex_12_07.jpg)
Usiku ule ule, Farao aliwaita Musa na Haruni na kuwaambia, "wachukueni Waisraeli muondoke haraka." Hata Wamisri pia waliwasihi Waisraeli watoke haraka.