unfoldingWord 06 - Mungu anamjalia Isaka
Kontur: Genesis 24:1-25:26
Skript nömrəsi: 1206
Dil: Swahili
Tamaşaçılar: General
Janr: Bible Stories & Teac
Məqsəd: Evangelism; Teaching
Müqəddəs Kitabdan Sitat: Paraphrase
Vəziyyət: Approved
Skriptlər digər dillərə tərcümə və qeyd üçün əsas təlimatlardır. Onlar hər bir fərqli mədəniyyət və dil üçün başa düşülən və uyğun olması üçün lazım olduqda uyğunlaşdırılmalıdır. İstifadə olunan bəzi terminlər və anlayışlar daha çox izahat tələb edə bilər və ya hətta dəyişdirilə və ya tamamilə buraxıla bilər.
Skript Mətni
Wakati Ibrahimu alipokuwa mzee sana, mtoto wake wa kiume, Isaka alikuwa amekuwa mtu mzima. Ibrahimu alimtuma mmoja wa watumishi wake kwenda katika nchi walioishi ndugu zake na Ibrahimu ili kumtafutia mke kwa ajili ya mtoto wake, Isaka.
Baada ya safari ndefu ya kwenda walikoishi ndugu zake na Ibrahimu, Mungu alimwongoza mtumishi wa Ibrahimu kwa Rebeka. Rebeka alikuwa ni mjukuu wa kaka yake na Ibrahimu.
Rebeka alikubali kuiacha familia yake na kwenda pamoja na yule mtumishi wa Ibrahimu hadi nyumbani kwa Isaka. Na mara baada ya kufika huko, Isaka alimuoa Rebeka.
Baada ya muda mrefu, Ibrahimu alifariki na ahadi zote alizokuwa ameahidiwa na Mungu katika agano zilihamishwa kwa Isaka, mwanae. Mungu alikuwa ameahidi kuwa Ibrahimu atakuwa na uzao mwingi usiohesabika, lakini Rebeka, mkewe Isaka, hakujaliwa kuwa na watoto.
Isaka alimwombea Rebeka. Mungu alimjibu na Rebeka akabeba mimba ya mapacha. Wale watoto wawili walikuwa wakishindana tumboni mwa Rebeka. Rebeka akamwuliza Mungu juu ya hicho kilichokuwa kikitokea tumboni mwake.
Mungu akamwambia Rebeka, " Mataifa mawili yatatokea kutokana na watoto wawili wa kiume walio tumboni mwako. Na kutakuwa na ushindani kati yao, na mtoto mkubwa atamtumikia mdogo."
Na siku ile walipozaliwa watoto wa Rebeka, mtoto mkubwa alitoka akiwa mwekundu na mwenye nywele nyingi katika mwili wake; walimwita jina lake, Esau. Mtoto mdogo alizaliwa huku akiwa amekishikilia kisigino cha Esau, naye walimwita jina lake, Yakobo.