unfoldingWord 06 - Mungu anamjalia Isaka

Garis besar: Genesis 24:1-25:26
Nomor naskah: 1206
Bahasa: Swahili
Pengunjung: General
Tujuan: Evangelism; Teaching
Features: Bible Stories; Paraphrase Scripture
Status: Approved
Naskah ini adalah petunjuk dasar untuk menerjemahkan dan merekam ke dalam bahasa-bahasa lain. Naskah ini harus disesuaikan seperlunya agar dapat dimengerti dan sesuai bagi setiap budaya dan bahasa yang berbeda. Beberapa istilah dan konsep yang digunakan mungkin butuh penjelasan lebih jauh, atau diganti atau bahkan dihilangkan.
Isi Naskah

Wakati Ibrahimu alipokuwa mzee sana, mtoto wake wa kiume, Isaka alikuwa amekuwa mtu mzima. Ibrahimu alimtuma mmoja wa watumishi wake kwenda katika nchi walioishi ndugu zake na Ibrahimu ili kumtafutia mke kwa ajili ya mtoto wake, Isaka.

Baada ya safari ndefu ya kwenda walikoishi ndugu zake na Ibrahimu, Mungu alimwongoza mtumishi wa Ibrahimu kwa Rebeka. Rebeka alikuwa ni mjukuu wa kaka yake na Ibrahimu.

Rebeka alikubali kuiacha familia yake na kwenda pamoja na yule mtumishi wa Ibrahimu hadi nyumbani kwa Isaka. Na mara baada ya kufika huko, Isaka alimuoa Rebeka.

Baada ya muda mrefu, Ibrahimu alifariki na ahadi zote alizokuwa ameahidiwa na Mungu katika agano zilihamishwa kwa Isaka, mwanae. Mungu alikuwa ameahidi kuwa Ibrahimu atakuwa na uzao mwingi usiohesabika, lakini Rebeka, mkewe Isaka, hakujaliwa kuwa na watoto.

Isaka alimwombea Rebeka. Mungu alimjibu na Rebeka akabeba mimba ya mapacha. Wale watoto wawili walikuwa wakishindana tumboni mwa Rebeka. Rebeka akamwuliza Mungu juu ya hicho kilichokuwa kikitokea tumboni mwake.

Mungu akamwambia Rebeka, " Mataifa mawili yatatokea kutokana na watoto wawili wa kiume walio tumboni mwako. Na kutakuwa na ushindani kati yao, na mtoto mkubwa atamtumikia mdogo."

Na siku ile walipozaliwa watoto wa Rebeka, mtoto mkubwa alitoka akiwa mwekundu na mwenye nywele nyingi katika mwili wake; walimwita jina lake, Esau. Mtoto mdogo alizaliwa huku akiwa amekishikilia kisigino cha Esau, naye walimwita jina lake, Yakobo.