unfoldingWord 06 - Mungu anamjalia Isaka

Đề cương: Genesis 24:1-25:26
Số kịch bản: 1206
ngôn ngữ: Swahili
Khán giả: General
Mục đích: Evangelism; Teaching
Features: Bible Stories; Paraphrase Scripture
Trạng thái: Approved
Bản văn này là một hướng dẫn cơ bản cho dịch và thu âm trong các ngôn ngữ khác. Nó phải được thích nghi với nền văn hóa và ngôn ngữ để làm cho nó phù hợp với từng khu vực, nơi nó được sử dụng khác nhau. Một số thuật ngữ và khái niệm được sử dụng có thể cần một lời giải thích đầy đủ hơn hoặc thậm chí bị bỏ qua trong các nền văn hóa khác nhau.
Kịch bản

Wakati Ibrahimu alipokuwa mzee sana, mtoto wake wa kiume, Isaka alikuwa amekuwa mtu mzima. Ibrahimu alimtuma mmoja wa watumishi wake kwenda katika nchi walioishi ndugu zake na Ibrahimu ili kumtafutia mke kwa ajili ya mtoto wake, Isaka.

Baada ya safari ndefu ya kwenda walikoishi ndugu zake na Ibrahimu, Mungu alimwongoza mtumishi wa Ibrahimu kwa Rebeka. Rebeka alikuwa ni mjukuu wa kaka yake na Ibrahimu.

Rebeka alikubali kuiacha familia yake na kwenda pamoja na yule mtumishi wa Ibrahimu hadi nyumbani kwa Isaka. Na mara baada ya kufika huko, Isaka alimuoa Rebeka.

Baada ya muda mrefu, Ibrahimu alifariki na ahadi zote alizokuwa ameahidiwa na Mungu katika agano zilihamishwa kwa Isaka, mwanae. Mungu alikuwa ameahidi kuwa Ibrahimu atakuwa na uzao mwingi usiohesabika, lakini Rebeka, mkewe Isaka, hakujaliwa kuwa na watoto.

Isaka alimwombea Rebeka. Mungu alimjibu na Rebeka akabeba mimba ya mapacha. Wale watoto wawili walikuwa wakishindana tumboni mwa Rebeka. Rebeka akamwuliza Mungu juu ya hicho kilichokuwa kikitokea tumboni mwake.

Mungu akamwambia Rebeka, " Mataifa mawili yatatokea kutokana na watoto wawili wa kiume walio tumboni mwako. Na kutakuwa na ushindani kati yao, na mtoto mkubwa atamtumikia mdogo."

Na siku ile walipozaliwa watoto wa Rebeka, mtoto mkubwa alitoka akiwa mwekundu na mwenye nywele nyingi katika mwili wake; walimwita jina lake, Esau. Mtoto mdogo alizaliwa huku akiwa amekishikilia kisigino cha Esau, naye walimwita jina lake, Yakobo.