unfoldingWord 31 - Yesu Atembea Juu ya Maji

unfoldingWord 31 - Yesu Atembea Juu ya Maji

إستعراض: Matthew 14:22-33; Mark 6:45-52; John 6:16-21

رقم النص: 1231

لغة: Swahili

الجماهير: General

فصيل: Bible Stories & Teac

الغرض: Evangelism; Teaching

نص من الإنجيل: Paraphrase

حالة: Approved

هذا النص هو دليل أساسى للترجمة والتسجيلات فى لغات مختلفة. و هو يجب ان يعدل ليتوائم مع اللغات و الثقافات المختلفة لكى ما تتناسب مع المنطقة التى يستعمل بها. قد تحتاج بعض المصطلحات والأفكار المستخدمة إلى شرح كامل أو قد يتم حذفها فى ثقافات مختلفة.

النص

Kisha Yesu aliwaambia wanafunzi wapande kwenye mtumbwi na wasafiri hadi ng'ambo ya ziwa wakati alipokuwa akiyaaga makutano. Baada ya Yesu kuyaaga makutano kwenda zao, alipanda mlimani ili aombe huko. Yesu alibaki huko pekee yake, na aliomba mpaka usiku wa manane.

Wakati huo huo, wanafunzi walikuwa wakipiga kasia kwa mtumbi wao, lakini wakati wa usiku wa manane walikuwa pekee yao katikati ya ziwa. Walikuwa wakipiga kasia kwa shida kwa sababu upepo ulikuwa ukivuma kinyume chao.

Kisha Yesu alimaliza kuomba na akaenda kwa wanafunzi. Alitembea juu ya maji akivuka ziwa mbele ya mtumbwi wao!

Wanafunzi walijawa na hofu kuu walipomwona Yesu, sababu walidhani walikuwa wakiona roho. Yesu hali akijua kuwa wanafunzi wake wameogopa, alipaza sauti kwao kusema, "Msiogope. Ni mimi!

Kisha Petro akamwambia Yesu, "Bwana, kama ni wewe niruhusu nije kwako juu ya maji". Yesu akamwambia Petro "Njoo!"

Hivyo, Petro akatoka kwenye mtumbwi na kuanza kutembea kwenda kwa Yesu juu ya uso wa maji. Lakini baada ya kwenda mwendo mfupi, aliyaondoa macho yake kwa Yesu na kuanza kutazama mawimbi na kuhisi nguvu ya upepo.

Kisha Petro akashikwa na woga na kuanza kuzama ndami ya maji. Akapaza sauti kwake, "Bwana, niokoe!" Yesu alimwendea na kumnyakua. Kisha akamwambia Petro, "Wewe mwenye imani haba, kwa nini umeona shaka?"

Wakati Yesu na Petro walipopanda ndani ya mtumbwi, mara upepo ulikoma kuvuma na maji yakatulia. Wanafunzi wakashangaa. Wakamwabudu Yesu wakisema, "Hakika, wewe ni Mwana wa Mungu".

معلومات ذات صلة

كلمات الحياة - GRN لديها رسائل صوتية تبشيرية فى الاف الغات تحتوى على رسائل الكتاب المقدس الرئيسية عن الفداء والحياة المسيحية.

تحميلات مجانية - هنا يمكنك أن تجد نصوص رسائل GRN الرئيسية فى عدة لغات، بالإضافة إلى صور ومواد أخرى مرتبطة، متوفرة للتحميل.

مكتبة GRN الصوتية - المواد التبشيرية و التعليمية للكتاب المقدس الملائمة لإحتياجات الناس و ثقافاتهم متاحة فى أشكال و أنماط عديدة.

Copyright and Licensing - GRN shares it's audio, video and written scripts under Creative Commons

Choosing the right audio or video format - What audio and video file formats are available from GRN, and which one is best to use?