unfoldingWord 18 - Ufalme Uliogawanyika

unfoldingWord 18 - Ufalme Uliogawanyika

概要: 1 Kings 1-6; 11-12

文本編號: 1218

語言: Swahili

聽眾: General

類型/流派: Bible Stories & Teac

目的: Evangelism; Teaching

聖經摘錄: Paraphrase

狀態: Approved

腳本是翻譯和錄製成其他語言的基本指南,它們需要根據實際需要而進行調整以適合不同的文化和語言。某些使用術語和概念可能需要有更多的解釋,甚至要完全更換或省略。

文本文字

Baada ya miaka mingi Daudi alifariki, na mwanae aitwaye Solomoni akatawala Israeli badala yake. Mungu alimuuliza Solomoni kitu muhumu amabcho angetaka apewe. Mungu alimpa Solomoni hekima nyingi kuliko watu wote kama alivyoomba. Naye alijifunza mambo mengi na kutawala kwa haki. Pia Mungu alimpa Solomoni utajiri mwingi.

Katika mji wa Jerusalemu, Solomoni alijenga Hekalu ambayo Baba yake Daudi alikusudia kuujenga na hivyo kuandaa vifaa vya ujenzi. Watu walianza kumuabudu na kumtolea Mungu sadaka ndani ya Hekalu badala ya kwenye hema ya kukutania. Mungu alishuka na kukaa ndani ya hekalu na kuishi pamoja na watu wake.

Lakini Solomoni aliwapenda wanawake wa mataifa mengine .Hakumtii Mungu kwa kuwaoa wanawake wengi. Aliwaoa karibu wake 1000. Hao wanawake waliolewa na Solomoni kutoka mataifa mengine walileta na kuaendelea kuabudu miungu yao . Hata Solomoni alipokuwa mzee, naye akaabudu hizo miungu.

Mungu alimkasirikia Solomoni, na kukusudia kumuadhibu kwasababu ya kukosa uaminifu. Hivyo Mungu akaahidi kugawa Taifa la Israeli kuwa falme mbili baada ya kifo chake.

Baada ya Solomoni kufa, Rehoboamu mwanaye , akawa Mfalme. Rehoboamu alikuwa mfalme mpumbavu , watu wote wa Israeli walimridhia yeye kuwa mfalme wao. Watu walimjia na kumlalamikia kuwa Baba yake Solomoni aliwatesa kwa kazi ngumu na kuwatoza gharama kubwa ya kodi.

Mfalme Rehoboamu aliwajibu kwa upumbavu kuwa , msidhani ya kuwa baba yangu aliwapa ninyi kazi nguu , kwani mimi nitawafanya ninyi mfanye kazi ngumu zaidi kuliko alizowapa Baba yangu na kuwapatia ninyi adhabu zaidi kuliko yale ya Baba yangu.

Makabila kumi ya Taifa la Israeli yalimuasi mfalme Rehoboamu , na makabila mawili yaliendelea kuwa waaminifu kwake. Hayo makabila mawili yaliunda ufalme wa Yuda.

Makabila yale kumi ya Israeli yaliyo muasi Rehoboamu, waliungana na kumchagua mtu aitwaye Jeroboamu kuwa mfalme wao. Wao walikaa kazikazini mwa nchi ya Israeli. Makabila hayo kumi yaliunda ufalme wa Israeli.

Jeroboamu alimuasi Mungu a kuwafanya watu kutenda dhambi. Alitengeneza sanamu mbili na kuwafanya watu kuiabudu badala ya kumuabudu Mungu wa kweli anayeabuduiwa katika Hekalu lililoko Yuda.

Ufalme wa Yuda na Israeli wakawa maadui, na mara nyingi hupigana wao kwa wao

Katika Ufalme mpya wa Israeli wafalme wote walikuwa waovu, na wafalme wengi waliuwawa na waisraeli waliotaka kuwa wafalme badala yao

Wafalme wote , na watu wengi waliopo katika ufalme wa Israeli waliabudu sanamu. Baadhi ya vitu walivyoabudu ni pamoja na uzinzi na kutoa kafara ya watoto wao.

Wafalme wa Yuda ni wazaliwa wa Daudi, baadhi ya wafalme hao waliongoza kwa haki na kumuabudu Mungu, hata hivyo wengi wa wafalme wa Yuda walikuwa waovu na walarushwa, baadhi yao hutoa watoto wao kama kafara kwa miungu. Pia watu wengi wa ufalme wa Yuda walimuasi Mungu na kuabudu miungu mingine.

相關信息

生命之道 - 環球錄音網擁有用數以千計的語言去錄製的福音信息,內容包括一些有關救恩和基督徒樣式的聖經信息。

免費下載 - 免費下載傳教及發展教會組織所用的錄音、圖片、文本和其他相關資料。內容包括聖經故事與傳教課程,并已被翻譯成上千種語言。

環球錄音網音頻圖書館 - 提供mp3,CD和磁帶形式的傳播福音和基本的宣教材料,適宜人們的需要和文化。錄音材料的形式多樣,包括簡單的聖經故事,福音信息,經文朗誦和歌曲。

Copyright and Licensing - GRN shares it's audio, video and written scripts under Creative Commons

Choosing the right audio or video format - What audio and video file formats are available from GRN, and which one is best to use?