unfoldingWord 18 - Ufalme Uliogawanyika

unfoldingWord 18 - Ufalme Uliogawanyika

Outline: 1 Kings 1-6; 11-12

Script Number: 1218

Language: Swahili

Audience: General

Genre: Bible Stories & Teac

Purpose: Evangelism; Teaching

Bible Quotation: Paraphrase

Status: Approved

Scripts are basic guidelines for translation and recording into other languages. They should be adapted as necessary to make them understandable and relevant for each different culture and language. Some terms and concepts used may need more explanation or even be replaced or omitted completely.

Script Text

Baada ya miaka mingi Daudi alifariki, na mwanae aitwaye Solomoni akatawala Israeli badala yake. Mungu alimuuliza Solomoni kitu muhumu amabcho angetaka apewe. Mungu alimpa Solomoni hekima nyingi kuliko watu wote kama alivyoomba. Naye alijifunza mambo mengi na kutawala kwa haki. Pia Mungu alimpa Solomoni utajiri mwingi.

Katika mji wa Jerusalemu, Solomoni alijenga Hekalu ambayo Baba yake Daudi alikusudia kuujenga na hivyo kuandaa vifaa vya ujenzi. Watu walianza kumuabudu na kumtolea Mungu sadaka ndani ya Hekalu badala ya kwenye hema ya kukutania. Mungu alishuka na kukaa ndani ya hekalu na kuishi pamoja na watu wake.

Lakini Solomoni aliwapenda wanawake wa mataifa mengine .Hakumtii Mungu kwa kuwaoa wanawake wengi. Aliwaoa karibu wake 1000. Hao wanawake waliolewa na Solomoni kutoka mataifa mengine walileta na kuaendelea kuabudu miungu yao . Hata Solomoni alipokuwa mzee, naye akaabudu hizo miungu.

Mungu alimkasirikia Solomoni, na kukusudia kumuadhibu kwasababu ya kukosa uaminifu. Hivyo Mungu akaahidi kugawa Taifa la Israeli kuwa falme mbili baada ya kifo chake.

Baada ya Solomoni kufa, Rehoboamu mwanaye , akawa Mfalme. Rehoboamu alikuwa mfalme mpumbavu , watu wote wa Israeli walimridhia yeye kuwa mfalme wao. Watu walimjia na kumlalamikia kuwa Baba yake Solomoni aliwatesa kwa kazi ngumu na kuwatoza gharama kubwa ya kodi.

Mfalme Rehoboamu aliwajibu kwa upumbavu kuwa , msidhani ya kuwa baba yangu aliwapa ninyi kazi nguu , kwani mimi nitawafanya ninyi mfanye kazi ngumu zaidi kuliko alizowapa Baba yangu na kuwapatia ninyi adhabu zaidi kuliko yale ya Baba yangu.

Makabila kumi ya Taifa la Israeli yalimuasi mfalme Rehoboamu , na makabila mawili yaliendelea kuwa waaminifu kwake. Hayo makabila mawili yaliunda ufalme wa Yuda.

Makabila yale kumi ya Israeli yaliyo muasi Rehoboamu, waliungana na kumchagua mtu aitwaye Jeroboamu kuwa mfalme wao. Wao walikaa kazikazini mwa nchi ya Israeli. Makabila hayo kumi yaliunda ufalme wa Israeli.

Jeroboamu alimuasi Mungu a kuwafanya watu kutenda dhambi. Alitengeneza sanamu mbili na kuwafanya watu kuiabudu badala ya kumuabudu Mungu wa kweli anayeabuduiwa katika Hekalu lililoko Yuda.

Ufalme wa Yuda na Israeli wakawa maadui, na mara nyingi hupigana wao kwa wao

Katika Ufalme mpya wa Israeli wafalme wote walikuwa waovu, na wafalme wengi waliuwawa na waisraeli waliotaka kuwa wafalme badala yao

Wafalme wote , na watu wengi waliopo katika ufalme wa Israeli waliabudu sanamu. Baadhi ya vitu walivyoabudu ni pamoja na uzinzi na kutoa kafara ya watoto wao.

Wafalme wa Yuda ni wazaliwa wa Daudi, baadhi ya wafalme hao waliongoza kwa haki na kumuabudu Mungu, hata hivyo wengi wa wafalme wa Yuda walikuwa waovu na walarushwa, baadhi yao hutoa watoto wao kama kafara kwa miungu. Pia watu wengi wa ufalme wa Yuda walimuasi Mungu na kuabudu miungu mingine.

Related information

Words of Life - Audio gospel messages in thousands of languages containing Bible based messages about salvation and Christian living.

Free downloads - Here you can find all the main GRN message scripts in several languages, plus pictures and other related materials, available for download.

The GRN Audio Library - Evangelistic and basic Bible teaching material appropriate to the people's need and culture in a variety of styles and formats.

Copyright and Licensing - GRN shares it's audio, video and written scripts under Creative Commons

Choosing the right audio or video format - What audio and video file formats are available from GRN, and which one is best to use?