unfoldingWord 50 - Yesu Anarudi

unfoldingWord 50 - Yesu Anarudi

概要: Matthew 13:24-42; 22:13; 24:14; 28:18; John 4:35; 15:20; 16:33; 1 Thessalonians 4:13-5:11; James 1:12; Revelation 2:10; 20:10; 21-22

文本编号: 1250

语言: Swahili

听众: General

类型/流派: Bible Stories & Teac

目的: Evangelism; Teaching

圣经摘录: Paraphrase

状态: Approved

脚本是翻译和录制成其他语言的基本指南,它们需要根据实际需要而进行调整以适合不同的文化和语言。某些使用术语和概念可能需要有更多的解释,甚至要完全更换或省略。

文本正文

Kwa zaidi ya miaka 2,000, zaidi na zaidi watu ulimwenguni kote wamekuwa wakisikia habari njema kuhusu Yesu Masihi. Kanisa limekuwa likikua. Yesu aliahidi angerudi mwisho wa dunia. Ingawa bado hajarudi, ataitimiza ahadi yake.

Wakati tunamsubiri Yesu kurudi, Mungu anataka tuishi maisha ya utakatifu na ya kumweshimu. Tena anatutaka tuwaambie wengine habari za ufalme wake. Wakati Yesu alipokuwa akiishi duniani alisema, "Wanafunzi wangu wataihubiri habari njema ya ufalme wa Mungu kwa watu wote ulimwenguni na ndipo mwisho utawadia."

Makundi ya watu wengi bado hawajasikia habari za Yesu. Kabla hajarudi mbinguni, Yesu aliwaambia wakristo kuitangaza habari njema kwa watu ambao kamwe hawajasikia. Alisema, "Enendeni na kufanya wanafunzi kwa watu wa makundi yote!" na "Mashamba yamekomaa kwa mavuno!"

Pia Yesu alisema, "Mtumwa si mkuu juu ya bwana wake. Kama ilivyo mamlaka ya dunia hii inavyonichukia mimi, watawatesa na kuwaua kwa sababu yangu. Ingawaje katika dunia hii mtateswa, iweni na ujasiri kwa sababu nimemshinda Shetani, ambaye anatawala dunia hii. Ikiwa mtabaki waaminifu kwangu hadi mwisho, kisha Mungu atawaokoa!"

Yesu aliwaambia wanafunzi wake simlizi juu ya namna itakavyotokea kwa watu wakati dunia itakapokwisha. Alisema, "Mtu alipanda mbegu njema katika shamba lake. Wakati alipokuwa amelala, adui yake alikuja na kupanda mbegu za magugu sambamba na ngano na kisha akaenda zake."

Wakati mimea ilipoota, watumishi wa bwana walisema, 'Bwana, ulipanda mbegu njema katika shamba lile, Je, kwanini kuna magugu ndani yake?' Bwana akajibu, 'Lazima adui ameyapanda.'

Watumishi wakamjibu bwana wao, 'Je, tunaweza kuyang'oa magugu?' Bwana akasema, 'Hapana. Mkifanya hivyo, mtang'oa na ngano pamoja. Subirini hadi mavuno kisha mkusanye magugu katika matita na kuyateketeza kwa moto, bali muilete ngano gharani mwangu.'

Wanafunzi hawakufahamu maana ya simulizi, hivyo walimwomba Yesu awafafanulie. Yesu alisema, "Mtu aliyepanda mbegu njema anawakilisha Masihi. Na shamba linawakilisha ulimwengu. Mbegu njema inawakilisha watu wa ufalme wa Mungu.'"

Magugu yanawakilisha watu wa milki ya mwovu. Adui aliyepanda magugu anamwakilisha Ibilisi. Mavuno yanawakilisha mwisho wa dunia, na wavunaji wanawakilisha Malaika wa Mungu.

Wakati wa mwisho wa dunia, malaika watawakusanya pamoja watu wote walio wa milki ya Ibilisi na kuwatupa katika moto, mahali watakapolia na kusaga meno katika mateso ya kutisha. Kisha wenye haki watang'aa kama jua katika ufalme wa Mungu Baba yao."

Pia Yesu aliwaambia kwamba angerudi duniani kabla ya mwisho wa dunia. Atarudi kwa namna ilie ile alivyoondoka, kwa hali hiyo, atakuwa na mwili na atakuja na mawingu katika anga. Wakati Yesu akirudi, kila mkristo aliye kufa atafufuka kutoka wafu na kukutana naye mawinguni.

Kisha wakristo watakaosalia hai watanyakuliwa juu katika mawingu na kuungana pamoja na wakristo waliofufuka kutoka wafu. Wote watakuwa pamoja na Yesu huko. Baada ya hapo, Yesu atakaa na watu wake katika amani timilifu na umoja wa milele.

Yesu aliahidi kuwapa taji kwa kila mtu amwaminiye yeye. Watakaa na kutawala pamoja na Mungu katika amani timilifu ya milele.

Lakini Mungu atamhukumu kila mmoja ambaye hakumwamini Yesu. Atawatupa wote jehanamu, mahali watakapolia na kusaga meno katika mateso ya milele. Moto usioweza kuzimika utaendelea kuwaunguza, na funza hawatakoma kuwatafuna.

Wakati Yesu akirudi, atamwangamiza kabisa Shetani na ufalme wake. Atamtupa Shetani Jehanamu ambapo atachomwa milele, pamoja na kila mmoja aliyechagua kumfuata yeye badala ya kumtii Mungu.

Kwa sababu Adamu na Eva walimwasi Mungu na kuleta dhambi humu ulimwenguni, Mungu aliilaani na kukusudia kuiangamiza. Lakini kuna siku Mungu ataumba mbingu mpya na nchi mpya itakayokuwa kamilifu.

Yesu na watu wake wataishi katika nchi mpya, na atatawala milele juu ya kila kitu kilichopo. Atafuta kila chozi na hapatakuwa tena na mateso, huzuni, kilio, uovu, maumivu, au kifo. Yesu atatawala katika ufalme wake kwa haki na amani, na atakuwa na watu wake milele.

相关信息

人生箴言 - GRN提供几千种语言的福音音频信息,包含圣经信息,救赎和基督徒生活。

免费下载 - 免费下载传福音及发展教会所用的录音、图片、文本和其他相关资料。内容包括福音与圣经故事,并已被翻译成上千种语言。

环球录音网音频图书馆 - Mp3,CD和磁带格式的福音材料和圣经教学材料,满足人们不同文化的需求。录音材料的形式多样,包括简单的圣经故事,福音信息,经文朗诵和歌曲。

Choosing the audio or video format to download - What audio and video file formats are available from GRN, and which one is best to use?

Copyright and Licensing - GRN shares it's audio, video and written scripts under Creative Commons