unfoldingWord 46 - Paulo Anakuwa Mkristo

unfoldingWord 46 - Paulo Anakuwa Mkristo

概要: Acts 8:1-3; 9:1-31; 11:19-26; 13-14

文本編號: 1246

語言: Swahili

聽眾: General

類型/流派: Bible Stories & Teac

目的: Evangelism; Teaching

聖經摘錄: Paraphrase

狀態: Approved

腳本是翻譯和錄製成其他語言的基本指南,它們需要根據實際需要而進行調整以適合不同的文化和語言。某些使用術語和概念可能需要有更多的解釋,甚至要完全更換或省略。

文本文字

Kijana Sauli ndiye alitunza nguo za wanaume waliomuua Stefano. Yeye hakuwa mfuasi wa Yesu. Kazi yake ilikuwa kuwatesa wakristo. Alizungukia kila kaya mjini Yerusalemu akiwakamata watu wa jinsia zote waliomwamini Yesu na kuwaweka gerezani. Mkuu wa makuhani alimpa kibali kwenda Dameski kuwakamata wafuasi wa Yesu na kuwaleta Yerusalemu.

Sauli alipokuwa akienda Damesiki, nuru kuu kutoka mbinguni ilimwangaza pande zote na akaanguka chini. Sauli alisikia mtu akisema, "Sauli! Sauli! Kwa nini unaniudhi?" Sauli alimuuliza" Wewe ni nani Bwana?" Jibu la Yesu lilikuwa, "Mimi ni Yesu unayeniudhi."

Sauli alipoamuka, hakuweza kuona. Waliokuwa pamoja naye ilibidi wampeleke Dameski. Alikaa siku tatu bila kula wala kunywa.

Huko Dameski alikuwapo mwanafunzi wa Yesu aliyeitwa Anania. Mungu alimwagiza, "Nenda katika nyumba ambamo anaishi Sauli. Weka mikono juu yake ili apate kuona tena." Bali Anania akajibu, "Bwana nimesikia jinsi mtu huyu anavyowaudhi wafuasi wa wako. "Mungu akamwambia, Nenda! Nimemchagua alitangaze Jina langu kwa Wayahudi na kwa watu kutoka Mataifa mengine. Naye atateseka sana kwa ajili ya jina langu."

Ndipo Anania alikaenda kwa Sauli, akamwekea mikono, akasema, "Yesu uliyekutana naye njiani wakati unakuja hapa, amenituma kwako ili upate kuona tena na ujazwe na Roho Mtakatifu". Mara akaweza kuona tena. Kisha Anania akambatiza, akala chakula na nguvu zake zikamrudia.

Mara hiyo, Sauli alianza kuhubiri Wayahudi katika Dameski akisema, "Yesu ni Mwana wa Mungu". Wayahudi walishangaa kuona mtu aliyekuwa akijitahidi kuwaangamiza wakristo amegeuka kuwa mfuasi wa Yesu! Sauli alibainisha kuwa Yesu ndiye Masihi.

Siku nyingi baadaye, Wayahudi walipanga kumuua Sauli. Waliwatuma watu kumfuatilia katika malango ya miji kwa lengo la kumwangamiza. Lakini Sauli aligundua mpango huo, na rafiki zake walimsaidia kutoroka. Usiku mmoja aliteremshwa akiwa ndani ya kikapu ukutani, akishatoroka kutoka Dameski aliendelea tu kuhubiri habari za Yesu.

Sauli alitembelea Yerusalemu, lakini wanafunzi wa Yesu walimhofu. Kisha muumuni aliyeitwa Barinaba alimpeleka kwa mitume kuwaeleza jinsi alivyo hubiri kwa ujasiri habari njema huko Dameski. Taarifa hiyo ilisababisha mitume wamkubali Sauli.

Baadhi ya waumini waliokimbia mateso huko Yerusalemu na kwenda mbali huko Antiokia, walizidi kuhubiri kuhusu Yesu. Wenyeji wengi wa Antiokia hawakuwa Wayahudi, hicho ndicho kipindi ambacho watu wa mataifa kwa mara ya kwanza waliipokea imani. Barinaba na Sauli walikwenda huko kuwafundisha hao waumini wachanga zaidi kuhusu Yesu na kulikomaza kanisa. Kwa mara ya kwanza wafuasi wa Yesu waliitwa Wakristo hapo Antiokia.

Hapo Antiokia, siku moja wakristo walipo kuwa katika maombi ya kufunga, Roho Mtakatifu aliwaambia nitengeeni Sauli na Barinaba wafanye kazi niliyo waitia. Hivyo kanisa liliwaombea na kuwawekea mikono, kisha wakawatuma waende maeneo mengine mengi kuhubiri habari njema za Yesu. Barinaba na Sauli walifundisha makundi ya watu wa matifa mbalimbali, watu wengi wakamwamini Yesu.

相關信息

生命之道 - 環球錄音網擁有用數以千計的語言去錄製的福音信息,內容包括一些有關救恩和基督徒樣式的聖經信息。

免費下載 - 免費下載傳教及發展教會組織所用的錄音、圖片、文本和其他相關資料。內容包括聖經故事與傳教課程,并已被翻譯成上千種語言。

環球錄音網音頻圖書館 - 提供mp3,CD和磁帶形式的傳播福音和基本的宣教材料,適宜人們的需要和文化。錄音材料的形式多樣,包括簡單的聖經故事,福音信息,經文朗誦和歌曲。

Copyright and Licensing - GRN shares it's audio, video and written scripts under Creative Commons

Choosing the right audio or video format - What audio and video file formats are available from GRN, and which one is best to use?