unfoldingWord 21 - Mungu Anaahidi Ujio wa Masihi

unfoldingWord 21 - Mungu Anaahidi Ujio wa Masihi

文本編號: 1221

語言: Swahili

聽眾: General

類型/流派: Bible Stories & Teac

目的: Evangelism; Teaching

聖經摘錄: Paraphrase

狀態: Approved

腳本是翻譯和錄製成其他語言的基本指南,它們需要根據實際需要而進行調整以適合不同的文化和語言。某些使用術語和概念可能需要有更多的解釋,甚至要完全更換或省略。

文本文字

Tangu mwanzo Mungu alipanga kumtuma masihi na ahadi ya kwanza ilikuwa kwa Adamu na Eva, Mungu akaahidi uzao kutoka kwa Eva kuwa atamponda Nyoka kichwa, Kwa maana aliyemdanganya Eva alikuwa Nyoka nae ni Shetani, ahadi hii inamaanisha mwokozi atakuja kumshinda Shetani.

Mungu alimuahidi Ibrahim kuwa kupitia yeye watu wote Duniani watabarikiwa, ahadi hii itatimia pale mwokozi atakapokuja, na watu katika makundi wa ulimwengu wataokoka kupitia ujio wa masihi.

Mungu alimuahidi Musa yakwamba baada ya yeye kumaliza atamuinua Nabii mwingine kama yeye, na hii ni ahadi nyingine juu ya ujio wa Masihi kwa siku zijazo.

Mungu alimuahidi Mfalme Daudi yakwamba mmoja kati ya mzaliwa wa vizazi vyake atainuliwa nakuwa Mfalme wa watu wa Mungu milele, hii inamaanisha kwamba masihi atakuwa miongoni kizazi kutoka kwa Daudi.

Kupitia Nabii Nehemia Mungu aliahidi kuweka maagano mapya, lakini hayatafanana na maagano aliyoweka kwa Wayahudi kwa iziraeli, kwenye maagano mapya Mungu ataandika sheria zake ndani ya miyoyo ya watu ili waweze kumjua kumjua Mungu nao watakuwa watu wake, na Mungu kuwasamehe dhambi zao, masihi kuanza maagano mapya.

Manabii wa Mungu wanasema masihi nae atakuwa nabii, Kuhani na Mfalme. Maana nabii ni mtu anaesikia neno la Mungu na kulitangaza kwa watu nae aliyeahidiwa kutumwa na Mungu atakuwa ni nabii wa kweli.

Makuhani wa iziraeli walimtolea Mungu dhabihu kwa niaba ya watu kwa hukumu ya dhambi zao pia humuomba Mungu kwaajili ya watu, Mwokozi ni kuhani aliyejitoa kuwa dhabihu kamilifu kwa Mungu.

Mfalme ni mtu anaetawala falme na kutoa hukumu kwa watu, mwokozi atakuwa Mfalme mkamilifu na kuweza kumiliki nafasi ya Daudi ili atawale na kutoa hukumu ya haki.

Manabii wa Mungu walitabili mengi kuhusu masihi, nabii Malaki alitabili ujio wa nabii mkubwa kabla wa Masihi kuja, nae nabii Isaya alitabili mwokozi kuzaliwa na bikila, nabii Maiko alisema masihi atazaliwa katika mji wa Betelehemu.

Nabii Isaya alisemamasihi ataishi Galilaya, atawafariji waliopondeka moyo na kutangaza uhuru kwa waliofungwa, pia walitabili masihi ataponya wagonjwa, viziwi, vipofu na mabubu.

Nabii Isaya alitabili juu ya kujchukiwa masihi atachukiwa bila sababu na kukataliwa, manabii wengine walinena yakwamba watakao kumuua masihi watagawa nguo zake na msaliti atakuwa mtu wa kalibu yake, nae nabii Zakaria akanena yakwamba sarafu therasini za fedha zitatumika kumlipa awezekumsaliti masihi.

Manabii walisema ni jinsi gani mwokozi atakufa, Isaya alitabili yakwamba watu wata mtemea mate, kumdhihaki na kumpiga masihi, kumsulubisha watamchoma mkuki nae atakufa na maumivu makali ijapokuwa hakutenda lolote baya.

Manabii walisema yakwamba masihi alikuwa mkamilifu na hakuwa na dhambi, alikufa ili azichukue dhambi za watu, mateso yake yataleta amani kati ya Mungu na wanadamu kwa maana hiyo ndipo Mungu akamsuribisha masihi.

Manabii walinena yakwamba masihi atakufa na Mungu atamuinua kutoka kwa wafu, kutokana na kifo na kufufuka kwa masihi, Mungu amekamilisha mpango wake wa kuokoa na dhambi na kuanza agano jipya.

Mungu aliwaonyesha mambo mengi kwa manabii kuhusu mwokozi, bali masihi hakuja kwa wakati wa manabii wengine na ni zaidi ya miaka, 400 baada ya nabii wa mwisho kupitta na wakati timilifu Mungu alimtuma masihi Duniani.

相關信息

生命之道 - 環球錄音網擁有用數以千計的語言去錄製的福音信息,內容包括一些有關救恩和基督徒樣式的聖經信息。

免費下載 - 免費下載傳教及發展教會組織所用的錄音、圖片、文本和其他相關資料。內容包括聖經故事與傳教課程,并已被翻譯成上千種語言。

環球錄音網音頻圖書館 - 提供mp3,CD和磁帶形式的傳播福音和基本的宣教材料,適宜人們的需要和文化。錄音材料的形式多樣,包括簡單的聖經故事,福音信息,經文朗誦和歌曲。

Choosing the audio or video format to download - What audio and video file formats are available from GRN, and which one is best to use?

Copyright and Licensing - GRN shares it's audio, video and written scripts under Creative Commons