unfoldingWord 13 - Agano la Mungu na Israeli

unfoldingWord 13 - Agano la Mungu na Israeli

概要: Exodus 19-34

文本編號: 1213

語言: Swahili

聽眾: General

類型/流派: Bible Stories & Teac

目的: Evangelism; Teaching

聖經摘錄: Paraphrase

狀態: Approved

腳本是翻譯和錄製成其他語言的基本指南,它們需要根據實際需要而進行調整以適合不同的文化和語言。某些使用術語和概念可能需要有更多的解釋,甚至要完全更換或省略。

文本文字

Baada ya Mungu kuwaongoza wana wa Israeli kupita bahari nyekundu, aliwaongoza kupitia nyikani hadi mlima ulioitwa Sinai. Mlima huu ndio mlima Musa alikiona kichaka kilichokuwa kikiwaka moto. Watu waliweka mahema yao pembezoni mwa mlima.

Mungu akasema na Musa na wana wa Israeli, "kama mtanitii na kulishika agano langu mtakuwa miliki yangu ya thamani, Makuhani wa Kifalme na taifa takatifu."

Baada ya siku tatu, watu walipokuwa wamejiandaa kiroho, Mungu alishuka juu ya mlima Sinai kwa ngurumo na radi, moshi na sauti ya mvumo wa tarumbeta. Musa peke yake aliruhusiwa kupanda mlimani.

Kisha Mungu aliwapa Agano akisema, "Mimi ni Yawe, Mungu wako aliyekuokoa kutoka utumwani Misri. Msiabudu miungu mingine."

Usijifanyie sanamu ya kuchonga wala usiiabudu, kwa sababu mimi Yawe ni Mungu mwenye wivu. Msilitaje bure jina la Bwana Mungu. Ikumbukeni siku ya sabato na kuitakasa. Kwa maneno mengine, fanya kazi kwa siku sita na siku ya saba ni sabato ya kupumzika kunikumbuka mimi.

Waheshimu Baba yako na Mama yako, usiue, usizini, usiibe., usiseme uongo, usimtamani mke wa jirani yako, nyumba yake au chochote kilicho chini ya milki yake.

Ndipo Mungu akaandika amri kumi katika mbao mbili za mawe akampa Musa. Vilevile Mungu alitoa sheria na amri nyingi na miongozo ya kufuata. Ikiwa watu watazitii sheria hizo, Mungu aliwaahidi kuwalinda na kuwabariki. Kama hawatamtii, Mungu angewaadhibu.

Mungu aliwapa Waisraeli maelekezo ya kina ya namna hema alivyota liwe. liliitwa hema la kukutania, na lilikuwa na vyumba viwili vilivyogawanywa kwa pazia kubwa. Kuhani Mkuu peke yake aliruhusiwa kuingia kwenye chumba nyuma ya pazia. Kwa sababu Mungu aliishi humo.

Kila ambaye hakuzitii sheria za Mungu, alipaswa kuleta mnyama kwenye madhabahu mbele ya hema ya kukutania kama dhabihu kwa Mungu. Kuhani alimchinja huyo mnyama na kumteketeza juu ya madhabahu. Damu ya mnyama huyo ilikuwa dhabihu ya kufunika dhambi za mtu na kuwa safi machoni pa Mungu. Mungu alimchagua Haruni ndugu yake na Musa na uzao wa Haruni kuwa Makuhani.

Watu walikubali kutii sheria ambazo Mungu aliwapa, kumwabudu Mungu pekee na kuwa watu wake maalumu. Lakini muda mfupi baada ya kuahidi kumtii Mungu, walimwasi vibaya sana.

Kwa siku nyingi, Musa alikuwa juu ya mlima Sinai akizungumza na Mungu. Watu walichoka kumsubiri alipokawia kurudi. Kwa hiyo walimletea Haruni dhahabu na kumtaka awatengenezee sanamu kwa ajili yao!

Haruni alitengeneza sanamu ya dhahabu kwa sura ya ndama. Watu walianza kuiabudu sanamu ya dhahabu nyikani na kutoa dhabihu juu yake. Mungu aliwakasirikia Kwa sababu ya dhambi yao na kupanga kuwaangamiza. Bali Musa aliwaombea, na Mungu akasikiliza maombi yake na kutokuwaangamiza.

Musa aliposhuka mlimani na kuiona hiyo sanamu alikasirika sana akazivunja hizo mbao za mawe zilizoandikwa amri kumi za Mungu.

Musa aliisagasaga sanamu na kuwa unga na kuutupa huo unga katika maji na watu kunywa hayo maji . Mungu alituma pigo kwa watu na wengi wao walikufa.

Musa alitengeneza mbao mpya za mawe za amri kumi za Mungu sawa na zile za kwanza zilizovunjika. Kisha alipanda tena mlimani na kuomba kwamba awasamehe hao watu. Musa alishuka mlimani na hizo mbao mpya za mawe zilizoandikwa amri kumi za Mungu. Kisha Mungu aliwaongoza Waisraeli kutoka mlima Sinai kuelekea nchi ya ahadi.

相關信息

生命之道 - 環球錄音網擁有用數以千計的語言去錄製的福音信息,內容包括一些有關救恩和基督徒樣式的聖經信息。

免費下載 - 免費下載傳教及發展教會組織所用的錄音、圖片、文本和其他相關資料。內容包括聖經故事與傳教課程,并已被翻譯成上千種語言。

環球錄音網音頻圖書館 - 提供mp3,CD和磁帶形式的傳播福音和基本的宣教材料,適宜人們的需要和文化。錄音材料的形式多樣,包括簡單的聖經故事,福音信息,經文朗誦和歌曲。

Choosing the audio or video format to download - What audio and video file formats are available from GRN, and which one is best to use?

Copyright and Licensing - GRN shares it's audio, video and written scripts under Creative Commons