unfoldingWord 02 - Dhambi Inaingia Ulimwenguni

unfoldingWord 02 - Dhambi Inaingia Ulimwenguni

概要: Genesis 3

文本編號: 1202

語言: Swahili

主題: Sin and Satan (Sin, disobedience, Punishment for guilt)

聽眾: General

類型/流派: Bible Stories & Teac

目的: Evangelism; Teaching

聖經摘錄: Paraphrase

狀態: Approved

腳本是翻譯和錄製成其他語言的基本指南,它們需要根據實際需要而進行調整以適合不同的文化和語言。某些使用術語和概念可能需要有更多的解釋,甚至要完全更換或省略。

文本文字

Adamu na mke wake waliishi kwa furaha katika bustani nzuri ambayo Mungu aliwaandalia. Hawa wawili hawakuvaa nguo, lakini hawakuona haya kwa sababu hakukuwa na dhambi duniani. Mara nyingi walitembea katika bustani na kuongea na Mungu.

Lakini kulikuwa na Nyoka mwerevu katika bustani. Alimuuliza mwanamke, "Je, ni kweli kwamba Mungu aliwaambia msile matunda ya mti wowote katika bustani?"

Mwanamke akajibu, "Mungu alisema twaweza kula matunda ya miti yote ya bustani isipokuwa matunda ya mti wa ujuzi wa mema na mabaya." Mungu alisema, "mukila au kugusa matunda ya mti huo, mtakufa."

Yule Nyoka akamjibu mwanamke, "Hiyo sio kweli! Hamwezi kufa. Mungu anajua kwamba pindi mtakapokula mtakuwa kama Mungu kwa kujua mema na mabaya kama ajuavyo."

Mwanamke aliona kuwa matunda yalikuwa mazuri na yalionekana kuwa matamu. Pia alitaka kuwa na hekima, hivyo alichuma tunda akala. Kisha akampa mume wake aliyekuwa pamoja naye, naye pia akala.

Mara macho yao yakafunguliwa, na wakagundua kwamba walikuwa uchi. Wakajaribu kuficha miili yao kwa kushona majani ili kujifanyia nguo.

Ndipo Adamu na mke wake wakasikia sauti ya Mungu akitembea katika bustani. Wote wakajificha. Mungu akamwita mwanaume, "Uko wapi?" Adamu akajibu, "Nimekusikia ukitembea katika bustani, nikaogopa kwa kuwa ni uchi, hivyo nikajificha."

Kisha Mungu akamuuliza, "Ni nani aliyekuambia kuwa u uchi? Je, umekula tunda nililokuambia usile?" Mwanaume akajibu, "wewe ulinipa huyu mwanamke, naye amenipa tunda." Ndipo Mungu akamuuliza mwanamke, "Umefanya nini?" Mwanamke akajibu, "Nyoka alinidanganya."

Mungu akamwambia Nyoka, "Umelaaniwa! kwa tumbo lako utaenda na utakula mavumbi. Wewe na mwanamke mtakuwa maadui, watoto wake na watoto wako watakuwa maadui pia. Uzao wa mwanamke utakuponda kichwa, nawe utamgonga kisigino chake."

Mungu akamwambia mwanamke, "Nitaongeza uchungu wakati wa kuzaa kwako. Hamu yako itakuwa juu ya mume wako, naye atakutawala."

Mungu akamwambia mwanaume, "Umemsikiliza mke wako na hukunitii mimi. Sasa ardhi imelaaniwa, na utafanya kazi kwa bidii ili upate chakula. Na kisha utakufa, na mwili wako utarudi katika uchafu." Mwanaume akamwita mke wake jina Eva, akimaanisha "Mtoa uhai," kwakuwa atafanyika mama wa watu wote. Na Mungu akawavalisha Adamu na Eva mavazi ya ngozi ya Wanyama.

Kisha Mungu akasema, "Kwakuwa sasa wanadamu wamekuwa kama sisi kwa kujua mema na mabaya, wasiruhusiwe kula tunda la mti wa uzima wakaishi milele." Hivyo Mungu aliwafukuza Adamu na Eva kutoka katika bustani nzuri ya Edeni. Mungu akaweka Malaika wenye nguvu kwenye malango ya bustani ili kuzuia mtu yeyote asile matunda ya mti wa uzima.

相關信息

生命之道 - 環球錄音網擁有用數以千計的語言去錄製的福音信息,內容包括一些有關救恩和基督徒樣式的聖經信息。

免費下載 - 免費下載傳教及發展教會組織所用的錄音、圖片、文本和其他相關資料。內容包括聖經故事與傳教課程,并已被翻譯成上千種語言。

環球錄音網音頻圖書館 - 提供mp3,CD和磁帶形式的傳播福音和基本的宣教材料,適宜人們的需要和文化。錄音材料的形式多樣,包括簡單的聖經故事,福音信息,經文朗誦和歌曲。

Choosing the audio or video format to download - What audio and video file formats are available from GRN, and which one is best to use?

Copyright and Licensing - GRN shares it's audio, video and written scripts under Creative Commons