unfoldingWord 27 - Simulizi ya Msamaria Mwema

unfoldingWord 27 - Simulizi ya Msamaria Mwema

概要: Luke 10:25-37

文本编号: 1227

语言: Swahili

听众: General

类型/流派: Bible Stories & Teac

目的: Evangelism; Teaching

圣经摘录: Paraphrase

状态: Approved

脚本是翻译和录制成其他语言的基本指南,它们需要根据实际需要而进行调整以适合不同的文化和语言。某些使用术语和概念可能需要有更多的解释,甚至要完全更换或省略。

文本正文

Siku moja Mwalimu wa mambo ya sheria ya Kiyahudi alimwendea Yesu na kumuuliza kwa kumjaribu akisema,"Mwalimu nifanyeje ili ni urithi uzima wa milele?" Yesu akamjibu " sheria ya Mungu imeandikwaje?"

Mwalimu wa mambo ya sheria ya Kiyahudi alimjibu Yesu na kusema, sheria ya Mungu inasema "Mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, kwa nafsi yako yote, kwa nguvu zako zote na kwa akili zako zote. Na pia inasema "Mpende jirani yako kama unavyojipenda mwenyewe. Yesu akamwambia "uko sahihi. Fanya hivyo na utaurithi uzima wa milele."

Lakini huyu Mwalimu wa mambo ya sheria ya Kiyahudi akitaka kujionyesha kwamba yeye ni mwenye haki, alimuuliza Yesu; "Jirani yangu ni nani?"

Yesu alimjibu huyu Mwalimu wa mambo ya sheria ya Kiyahudi kwa kumpa simulizi. " Kulikuwa na Myahudi mmoja aliyekuwa anasafiri kwa barabara kutoka Yerusalemu kwenda Yeriko.

Wakati Myahudi huyu alipokuwa akisafiri kikundi cha wezi kilimvamia na kumwibia kila kitu na kumpiga sana karibu ya kufa. Walipokuwa wamempiga sana karibu ya kufa, walimwacha hapo barabarani na kuondoka zao.

Muda mfupi baada ya tukio hilo Kuhani wa Kiyahudi alikuwa akisafiri na kupitia katika barabara hii ambayo Myahudi yule alikuwa amepigwa na kuachwa pale. Alipomuona alipita upande mwingine wa barabara mbali na alipokuwepo mtu huyo na kuendelea na safari yake wala asimjali na kumsaidia mtu yule.

Baada ya muda mfupi Mlawi (Walawi walikuwa kabila la Wayahudi ambao lilikuwa linawasadia makuhani katika huduma hekaluni) naye alipita barabara hiyohiyo na alipomuona mtu yule aliyekuwa amepigwa na kuumizwa na wezi alipita upande mwingine wa barabara na kuendelea na safari yake bila kumjali.

Mtu mwingine aliyepita barabara hiyo alikuwa ni Msamaria (Wasamaria walikuwa wa uzao wa Wayahudi na ni watu waliooa na kuolewa na watu wa mataifa mengine. Wasamaria walikuwa wanachukiana sana na Wayahudi). Huyo Msamaria alipomuona Myahudi yule aliyekuwa amepigwa na kuumizwa sana na wezi, alimuonea sana huruma. Alimchukua na kuyahudumia majeraha yake na kumfunga pandeji.

Msamaria baada ya hapo alimchukua huyo Myahudi na kumpandisha kwenye Punda wake na kumpeleka kwenye nyumba ya wageni iliyokuwa karibu na barabara na kumuhudumia zaidi.

Siku iliyofuata Msamaria huyu alihitaji kuendelea na safari yake na hivyo alimkabidhi yule muangalizi wa nyumba ya wageni na kumwambia " Mhudumie Myahudi huyu aliyepigwa na wezi. Akampa fedha yule muangalizi na kumwambia, kama utatumia fedha zaidi katika kumhudumia Myahudi huyu basi nikirudi kutoka safari yangu nitakuja nilipe kiasi kilichoongezeka.

Baada ya hadithi hiyo, Yesu alimuuliza yule Mwalimu wa mambo ya sheria ya Kiyahudi, kwamba "Unafikiri katika watu hao watatu, ni nani aliyekuwa jirani yake yule Myahudi aliyepigwa na wezi?" Yule Mwalimu wa mambo ya sheria ya Kiyahudi alijibu na kumwambia Yesu "ni yule aliyemuonea huruma". Yesu akamwambia "Wewe nawe nenda kafanye vivyo hivyo."

相关信息

人生箴言 - GRN提供几千种语言的福音音频信息,包含圣经信息,救赎和基督徒生活。

免费下载 - 免费下载传福音及发展教会所用的录音、图片、文本和其他相关资料。内容包括福音与圣经故事,并已被翻译成上千种语言。

环球录音网音频图书馆 - Mp3,CD和磁带格式的福音材料和圣经教学材料,满足人们不同文化的需求。录音材料的形式多样,包括简单的圣经故事,福音信息,经文朗诵和歌曲。

Choosing the audio or video format to download - What audio and video file formats are available from GRN, and which one is best to use?

Copyright and Licensing - GRN shares it's audio, video and written scripts under Creative Commons