unfoldingWord 22 - Kuzaliwa kwa Yohana

unfoldingWord 22 - Kuzaliwa kwa Yohana

概要: Luke 1

文本编号: 1222

语言: Swahili

听众: General

类型/流派: Bible Stories & Teac

目的: Evangelism; Teaching

圣经摘录: Paraphrase

状态: Approved

脚本是翻译和录制成其他语言的基本指南,它们需要根据实际需要而进行调整以适合不同的文化和语言。某些使用术语和概念可能需要有更多的解释,甚至要完全更换或省略。

文本正文

Hapo zamani Mungu alikua akiongea na watu wake kwa kupitia Malaika na Manabii. Ilipita miaka 400 Mungu alikua hajazungumza na watu wake. Ghafla Malaika alikuja na ujumbe kutoka kwa Mungu kwenda kwa kuhani mzee aitwae Zakaria. Zakaria na mke wake Elizabeti walikua ni watu wa Mungu lakini Elizabeti alikuwa hajapata mtoto yeyote.

Malaika akamwambia Zakaria "tazama mke wako atapata mtoto wa kiume, nawe utamuita jina lake Yohana. Nae atajazwa Roho Mtakatifu na atawaandaa watu kwaajili ya Kristo!". Zakaria akamjibu "Mimi na mke wangu tu wazee sana kuweza kupata watoto. Nitajuaje kama haya yatatokea?"

Malaika akamjibu Zakaria akasema " tazama nilitumwa na Mungu kukuletea habari hizi njema. Kwakua umeshindwa kuniamini hutaweza kuongea mpaka pale mtoto atakapozaliwa" Hapohapo Zakaria hakuweza kuongea. Ndipo malaika alimuacha Zakaria. Baada ya hapo Zakaria alirudi nyumbani na mke wake akapata mimba.

Elizabeti alipokuwa na mimba ya miezi sita, malaika yule yule alimtokea ndugu yake Elizabeti aliyeitwa Maria.Alikuwa ni bikira na alikuwa amechumbiwa aolewe na kijana aitwae Yusufu. Malaika akamwambia "Tazama utachukua mimba na kuzaa mtoto mwanamume. Utamuita jina lake Yesu. Atakuwa ni mtoto wa Mungu aliye juu na atatawala milele."

Maria akajibu "Inawezekanaje jambo hili kutokea ingali mimi ni bikira?" Malaika akamwambia "Roho wa Bwana atakuja kwako na nguvu za Mungu zitakuwa juu yako na kukufunika kama kivuli. Kwa sababu hiyo mtoto atakuwa mtakatifu, mwana wa Mungu". Maria akaamini na kukubali alichoambiwa na malaika.

Baada ya malaika kuongea na Maria, Maria akaenda kumtembelea Elizabeti. Baada ya Elizabeti kusikia salaamu ya Maria mtoto aliekuwepo tumboni kwake aliruka. Na wote wawili walishangilia kwa furaha mambo mazuri waliotendewa. Baada ya Maria kumtembelea Elizabeti kwa miezi mitatu. Maria alirudi nyumbani kwake.

Baada ya Elizabeti kujifungua mtoto wake wa kiume, Zakaria na Elizabeti walimuita huyo mtoto Yohana, kama malaika alivyoamuru. Kisha Mungu alifungua kinywa cha Zakaria na akaweza kusema tena. Zakaria alisema "Asifiwe Mungu kwa kuwa amewakumbuka watu wake! Nawe mwanangu utaitwa nabii wa Mungu aliye juu utakae waambia watu jinsi ya kupokea msamaha wa dhambi zao.

相关信息

人生箴言 - GRN提供几千种语言的福音音频信息,包含圣经信息,救赎和基督徒生活。

免费下载 - 免费下载传福音及发展教会所用的录音、图片、文本和其他相关资料。内容包括福音与圣经故事,并已被翻译成上千种语言。

环球录音网音频图书馆 - Mp3,CD和磁带格式的福音材料和圣经教学材料,满足人们不同文化的需求。录音材料的形式多样,包括简单的圣经故事,福音信息,经文朗诵和歌曲。

Choosing the audio or video format to download - What audio and video file formats are available from GRN, and which one is best to use?

Copyright and Licensing - GRN shares it's audio, video and written scripts under Creative Commons