unfoldingWord 10 - Mapigo Kumi

unfoldingWord 10 - Mapigo Kumi

概要: Exodus 5-10

文本编号: 1210

语言: Swahili

听众: General

类型/流派: Bible Stories & Teac

目的: Evangelism; Teaching

圣经摘录: Paraphrase

状态: Approved

脚本是翻译和录制成其他语言的基本指南,它们需要根据实际需要而进行调整以适合不同的文化和语言。某些使用术语和概念可能需要有更多的解释,甚至要完全更换或省略。

文本正文

Watu wawili ambao ni Musa na Haruni walimwendea Farao na kumweleza kwamba, "Mungu wa Israeli anasema hivi, waruhusu watu wangu kuondoka katika nchi ya Misri." Farao hakukubali, alichofanya ni kuongeza uzito wa kazi kuliko hapo awali.

Farao aliendelea kuwakatalia Waisraeli wasiondoke, kwa sababu hiyo Mungu alileta mapigo kumi kwa Wamisri ya madhara makubwa sana. Kwa kufanya hivyo Mungu alionesha kuwa yeye anao uwezo mkubwa kuliko Farao na miungu yote ya Wamisri.

Mungu aliyabadilisha maji ya mto Naili kuwa damu. Pamoja na pigo kama hilo Farao hakutoa ruhusa kwa Waisraeli kuondoka katika nchi ya Misri.

Mungu alileta vyura kuwasumbua Wamisri wote. Farao alimwomba Musa aombe ili vyura wasiendelee kuwepo. Lakini baada ya Musa kuomba na vyura kutoweka moyo wa Farao uliendelea kuwa mgumu asiwaruhusu Waisraeli kuondoka katika nchi ya Misri.

Kwa sababu hiyo Mungu alileta pigo la chawa. Zaidi ya hapo Mungu alileta nzi, pigo ambalo lilimfanya Farao kuwaita Musa na Haruni kuwaambia kuwa kama janga hilo wataliondoa watapewa ruhusa ya kuondoka katika nchi ya Misri. Musa alimwomba Mungu kuondoa janga la nzi na Mungu akawaondoa nzi wote. Hata hivyo moyo wa Farao ulikuwa mgumu asiwaruhusu Waisraeli kuondoka.

Mungu alileta pigo la ugonjwa kwa mifugo wa Wamisri kwamba mifugo iliugua na kufa. Hata hivyo Farao alikuwa kaidi kuweza kuwaruhusu Waisreli kuondoka.

Ndipo Mungu akamwambia Musa kupeperusha majivu angani machoni pa Farao. Majivu hayo yalisababisha majipu yenye vidonda kwa Wamisri peke yake, Waisraeli hawakudhurika na majipu hayo. Mungu alimfanya Farao kuwa na moyo wa ukaidi na hivyo hakuweza kuwaruhusu Waisraeli kuondoka.

Baada ya janga la majipu, Mungu alileta mvua ya mawe iliyo haribu mazao na kuleta maafa kwa mtu yeyote aliyenyeshewa na mvua hiyo katika nchi ya Misri. Farao alionekana kujuta aliwaita Musa na Haruni na kusema, "nimefanya dhambi," sasa nitawaruhusu kuondoka. Musa alimwomba Mungu, mvua haikuendelea kunyesha.

Farao hata hivyo, hakuacha kutenda dhambi na moyo wake ukaendelea kuwa wenye ukaidi kwa kutowaachia uhuru Waisraeli kuondoka.

Kwa sababu hiyo Mungu alituma nzige wengi sana walioharibu mazao yote yaliyosalia na mvua ya mawe katika nchi ya Misri

Ndipo Mungu alileta giza totoro katika nchi ya Misri lillosababisha Wamisri wabakie majumbani mwao, wasitoke kwa muda wa siku tatu. Lakini mahali Waisraeli walipokuwa hapakuwa na giza.

Ingawa kulitokea mapigo tisa Farao hakukubali kuwaruhusu Waisraeli kuondoka. Kwa kuwa Farao hangeweza kusikiliza Mungu alikusudia kuleta pigo la mwisho. Pigo hili lingemfanya Farao kubadilisha mawazo yake.

相关信息

人生箴言 - GRN提供几千种语言的福音音频信息,包含圣经信息,救赎和基督徒生活。

免费下载 - 免费下载传福音及发展教会所用的录音、图片、文本和其他相关资料。内容包括福音与圣经故事,并已被翻译成上千种语言。

环球录音网音频图书馆 - Mp3,CD和磁带格式的福音材料和圣经教学材料,满足人们不同文化的需求。录音材料的形式多样,包括简单的圣经故事,福音信息,经文朗诵和歌曲。

Choosing the audio or video format to download - What audio and video file formats are available from GRN, and which one is best to use?

Copyright and Licensing - GRN shares it's audio, video and written scripts under Creative Commons