unfoldingWord 02 - Dhambi Inaingia Ulimwenguni

unfoldingWord 02 - Dhambi Inaingia Ulimwenguni

概要: Genesis 3

文本编号: 1202

语言: Swahili

主题: Sin and Satan (Sin, disobedience, Punishment for guilt)

听众: General

类型/流派: Bible Stories & Teac

目的: Evangelism; Teaching

圣经摘录: Paraphrase

状态: Approved

脚本是翻译和录制成其他语言的基本指南,它们需要根据实际需要而进行调整以适合不同的文化和语言。某些使用术语和概念可能需要有更多的解释,甚至要完全更换或省略。

文本正文

Adamu na mke wake waliishi kwa furaha katika bustani nzuri ambayo Mungu aliwaandalia. Hawa wawili hawakuvaa nguo, lakini hawakuona haya kwa sababu hakukuwa na dhambi duniani. Mara nyingi walitembea katika bustani na kuongea na Mungu.

Lakini kulikuwa na Nyoka mwerevu katika bustani. Alimuuliza mwanamke, "Je, ni kweli kwamba Mungu aliwaambia msile matunda ya mti wowote katika bustani?"

Mwanamke akajibu, "Mungu alisema twaweza kula matunda ya miti yote ya bustani isipokuwa matunda ya mti wa ujuzi wa mema na mabaya." Mungu alisema, "mukila au kugusa matunda ya mti huo, mtakufa."

Yule Nyoka akamjibu mwanamke, "Hiyo sio kweli! Hamwezi kufa. Mungu anajua kwamba pindi mtakapokula mtakuwa kama Mungu kwa kujua mema na mabaya kama ajuavyo."

Mwanamke aliona kuwa matunda yalikuwa mazuri na yalionekana kuwa matamu. Pia alitaka kuwa na hekima, hivyo alichuma tunda akala. Kisha akampa mume wake aliyekuwa pamoja naye, naye pia akala.

Mara macho yao yakafunguliwa, na wakagundua kwamba walikuwa uchi. Wakajaribu kuficha miili yao kwa kushona majani ili kujifanyia nguo.

Ndipo Adamu na mke wake wakasikia sauti ya Mungu akitembea katika bustani. Wote wakajificha. Mungu akamwita mwanaume, "Uko wapi?" Adamu akajibu, "Nimekusikia ukitembea katika bustani, nikaogopa kwa kuwa ni uchi, hivyo nikajificha."

Kisha Mungu akamuuliza, "Ni nani aliyekuambia kuwa u uchi? Je, umekula tunda nililokuambia usile?" Mwanaume akajibu, "wewe ulinipa huyu mwanamke, naye amenipa tunda." Ndipo Mungu akamuuliza mwanamke, "Umefanya nini?" Mwanamke akajibu, "Nyoka alinidanganya."

Mungu akamwambia Nyoka, "Umelaaniwa! kwa tumbo lako utaenda na utakula mavumbi. Wewe na mwanamke mtakuwa maadui, watoto wake na watoto wako watakuwa maadui pia. Uzao wa mwanamke utakuponda kichwa, nawe utamgonga kisigino chake."

Mungu akamwambia mwanamke, "Nitaongeza uchungu wakati wa kuzaa kwako. Hamu yako itakuwa juu ya mume wako, naye atakutawala."

Mungu akamwambia mwanaume, "Umemsikiliza mke wako na hukunitii mimi. Sasa ardhi imelaaniwa, na utafanya kazi kwa bidii ili upate chakula. Na kisha utakufa, na mwili wako utarudi katika uchafu." Mwanaume akamwita mke wake jina Eva, akimaanisha "Mtoa uhai," kwakuwa atafanyika mama wa watu wote. Na Mungu akawavalisha Adamu na Eva mavazi ya ngozi ya Wanyama.

Kisha Mungu akasema, "Kwakuwa sasa wanadamu wamekuwa kama sisi kwa kujua mema na mabaya, wasiruhusiwe kula tunda la mti wa uzima wakaishi milele." Hivyo Mungu aliwafukuza Adamu na Eva kutoka katika bustani nzuri ya Edeni. Mungu akaweka Malaika wenye nguvu kwenye malango ya bustani ili kuzuia mtu yeyote asile matunda ya mti wa uzima.

相关信息

人生箴言 - GRN提供几千种语言的福音音频信息,包含圣经信息,救赎和基督徒生活。

免费下载 - 免费下载传福音及发展教会所用的录音、图片、文本和其他相关资料。内容包括福音与圣经故事,并已被翻译成上千种语言。

环球录音网音频图书馆 - Mp3,CD和磁带格式的福音材料和圣经教学材料,满足人们不同文化的需求。录音材料的形式多样,包括简单的圣经故事,福音信息,经文朗诵和歌曲。

Choosing the audio or video format to download - What audio and video file formats are available from GRN, and which one is best to use?

Copyright and Licensing - GRN shares it's audio, video and written scripts under Creative Commons