unfoldingWord 41 - Mungu Anamfufua Yesu kutoka katika Wafu

unfoldingWord 41 - Mungu Anamfufua Yesu kutoka katika Wafu

Balangkas: Matthew 27:62-28:15; Mark 16:1-11; Luke 24:1-12; John 20:1-18

Bilang ng Talata: 1241

Wika: Swahili

Tagapakinig: General

Klase: Bible Stories & Teac

Layunin: Evangelism; Teaching

Kawikaan mula sa Bibliya: Paraphrase

Katayuan: Approved

Ang mga script ay panimulang gabay para sa pagsasalin at pagre-record sa ibat-ibang wika.Ang mga ito ay ay dapat na angkupin kung kinakailangan para maunawaan at makabuluhan sa bawat kultura at wika. Ilang termino at konsepto na ginamit ay maaaring gamitin para maipaliwanag o maaari di na palitan o tanggalin ng ganap.

Salita ng Talata

Baada ya askari kuwa wamemsulubisha Yesu, viongozi wa Kiyahudi wasioamini walimwambia Pilato, "Yule Muongo, Yesu, alisema angefufuka baada ya siku tatu. Mtu mmoja lazima alilinde kaburi ili kujihakikishia kwamba wanafunzi wake hawatauiba mwili wake na kusema amefufuka kutoka katika wafu."

Pilato alisema, "Chukueni baadhi ya askari na muhakikishe kaburi limelindwa ipasavyo." Hivyo wakaweka muhuri kwenye jiwe katika mlango wa kuingilia kaburini na kuweka maaskari ili kuhakikisha kwamba hakuna mtu yeyote ambaye angeuiba mwili.

Siku iliyofuata baada ya Yesu kuzikwa ilikuwa ni Sabato, na wayahudi hawakuruhusiwa kwenda kaburini siku hiyo. Hivyo asubuhi na mapema baada ya Sabato, wanawake wengi walijiandaa kwenda kwenye kaburi la Yesu kuupaka mwili wa Yesu marashi ya maziko.

Ghafla, kulikuwa na tetemeko kubwa. Malaika ambaye mng'ao wake ulikuwa kama mng'ao wa mwanga wa radi alitokea kutoka mbinguni. Aliliviringisha mbali lile jiwe lilokuwa limeufunika mlango wa kaburi na kulikalia. Askari waliokuwa wanalilinda kaburi waliogopa sana na kuanguka chini na kuwa kama watu waliokufa.

Wale wanawake walipofika kaburini, malaika aliwaambia. "Msiogope. Yesu hayupo hapa. Amefufuka kutoka katika wafu, kama alivyosema kwamba atafufuka! Angalieni kaburini na muone." Wale wanawake wakaangalia mle kaburini na kupaona mahali mwili wa Yesu ulipokuwa umelazwa. Mwili wake haukuwepo pale!

Malaika akawaambia wale wanawake, "Nendeni na mkawaambie wanafunzi, 'Kwamba Yesu amefufuka kutoka katika wafu na atawatangulia kwenda Galilaya."

Wanawake walijawa na hofu na furaha kuu. Wakakimbia kwenda kuwaambia wanafunzi habari njema.

Wale wanawake walipokuwa wanaenda kuwaambia wanafunzi wake habari njema, Yesu aliwatokea wale wanawake, nao wakamuabudu. Yesu akasema, "Msiogope. Nendeni mkawaambie wanafunzi wangu waende Galilaya.Wataniona huko."

Katulad na kaalaman

Salita ng Buhay - Ang GRN ay mayroong mensahe sa audio sa libo-libong wika na naglalaman ng mensahe base sa Bibliya tungkul sa kaligtasan at Kristyanong pamumuhay.

Libreng mga download - Dito ay matatagpuan ang lahat ng pangunahing scripts mensahe ng GRN sa ibat-ibang wika, at mga larawan at iba pang katulad na materyales, ay maaari ng i-download.

Ang GRN Aklatang Audio - Pag-eebanghelyo at panimulang kagamitan ng katuruang Bibliya na angkop sa mga pangangailangan at kultura ng mga tao sa isang iba't ibang estilo at mga format.

Choosing the audio or video format to download - What audio and video file formats are available from GRN, and which one is best to use?

Copyright and Licensing - GRN shares it's audio, video and written scripts under Creative Commons