unfoldingWord 39 - Yesu Anashitakiwa

unfoldingWord 39 - Yesu Anashitakiwa

เค้าโครง: Matthew 26:57-27:26; Mark 14:53-15:15; Luke 22:54-23:25; John 18:12-19:16

รหัสบทความ: 1239

ภาษา: Swahili

ผู้ฟัง: General

ประเภท: Bible Stories & Teac

เป้าหมายของสื่อบันทึกเสียง: Evangelism; Teaching

ข้ออ้างอิงจากพระคัมภีร์: Paraphrase

สถานะ: Approved

บทความเป็นแนวทางพื้นฐานสำหรับการแปลและบันทึกเสียงภาษาอื่นๆ ควรดัดแปลงตามความจำเป็นเพื่อให้เข้าใจและเหมาะสมกับวัฒนธรรมและภาษาแต่ละภาษา คำศัพท์และแนวคิดบางคำที่ใช้อาจต้องอธิบายเพิ่มเติม หรือแทนที่ หรือตัดออก

เนื้อหาบทความ

Ilikuwa usiku wa manane wakati huo. Askari wakampeleka kwenye nyumba ya kuhani mkuu ili kumhoji. Petro akawafuata kwa mbali nyuma yao. Wakati Yesu anachukuliwa kwenye nyumba, Petro alikuwa nje peke yake akiota moto.

Ndani ya Nyumba viongozi wa kiyahudi wakamshitaki Yesu. Wakaleta mashahidi wengi wa uongo walioshuhudia uongo dhidi ya Yake. vile vile hata maelezo yao yalitofautiana kila mmoja alisema tofauti. kwa hiyo viongozi wa kiyahudi hawakukubaliana kama alikuwa na hatia yeyote. Yesu hakusema chochote.

Hatimaye kuhani mkuu akamwangalia Yesu na kusema "Tuambie wewe ni Masihi mwana wa Mungu aliye hai?"

Yesu akamjibu, "Mimi ndiye, utaniona nimekaa na Mungu na pia nikishuka kutoka mbinguni" Kuhani mkuu akararua mavazi yake kwa hasira na akasema kwa sauti kuu kwa viongozi wa kidini wengine "Hatuhitaji mashahidi zaidi ya hawa! Mmesikia toka kwake mwenyewe, akisema yeye ni mwana wa Mungu. Hukumu yenu ni ipi?"

Viongozi wa kiyahudi wote wakamjibu kuhani mkuu kuwa "Anastahili kufa" baadaye wakamfunika macho Yesu, wakamtemea mate, wakampiga, na kumdhihaki.

Na Petro alikuwa inje ya nyumba akisubiri. Mtumishi mmoja msichana akamwona na akamwambia "Na wewe pia ulikuwa na Yesu!" Petro akakana. baadaye binti mwingine akasema kitu hichohicho. Na petro akakataa tena. hatimaye watu wakasema "Tunajua wewe ulikuwa pamoja naye maana ninyi nyote ni wenyeji wa Galilaya.

Tena Petro akaapa, akisema, "Mungu wangu na anilaani kama mimi namjua mtu huyu!" Mara ghafla Jogoo akawika na Yesu akageuka kumwangalia Petro.

Petro akaondoka na akilia kwa huzuni kubwa. Wakati huo huo, Yuda, mwenye kumsaliti Yesu, akaona kwamba viongozi wa kiyahudi wamemweka Yesu hatiani. Yuda akapatwa na huzuni kubwa sana na akaondoka mahali pale akaenda kujiua mwenyewe.

Asubuhi na mapema, viongozi wa kiyahudi wakamleta Yesu kwa Pilato liwali wa Kirumi. wakitumaini kuwa Pilato atamhukumu Yesu kama mtu mwenye hatia na wakamwambia auawe. Pilato akamuuliza Yesu "Wewe ni mfalme wa wayahudi?"

Yesu akamjibu "Wewe ndiye umesema hivyo, lakini ufalme wangu si ufalme wa dunia hii, kama ingekuwa hivyo watumishi wangu wangepigana kwa ajili yangu. Nimekuja ulimwenuni ili kuusema ukweli kuhusu Mungu. na kila mmoja anayependa huu ukweli hunisikiliza. Pilato akasema "Ukweli ni nini?"

Baada ya kuongea na Yesu Pilato alitoka nje katika umati wa Watu na kusema "Nimeona hakuna hatia juu ya mtu huyu" lakini viongozi wa kiyahudi na makutano wote wakapiga kelele "Msulubishe" pilato akajibu "Hana hatia" lakini waliendelea kupiga kelele tena kwa nguvu. na Pilato akasema kwa mara ya tatu "Hana hatia yeyote"

Pilato akaogopa kwamba makutano wataanza kuleta Ghasia, kwa hiyo aliwaruhusu askari wake kumsulubisha Yesu. Askari wa Kirumi wakampiga Yesu huku wakimpa vazi la kifalme na kofia iliyotengenezwa na miiba wakamvika. pia wakamdhihaki kwa kusema "Mtazame mfalme wa wayahudi"

ข้อมูลที่เกี่ยวข้อง

สื่อบันทึกเสียงรูปแบบmp3, ซีดี, เทปคาสเซ็ท - องค์กรจีอาร์เอ็น มีสื่อบันทึกเสียงต่างๆ หลายพันภาษา เนื้อหาสื่อบันทึกเสียงตรงกับความจริงในพระคัมภีร์ เป็นเรื่องราวเกี่ยวกับความรอดและชีวิตคริสเตียน

ดาวน์โหลดฟรี - ที่นี่ท่านสามารถค้นหาบทความต่างๆ ของจีอาร์เอ็นในภาษาต่างๆ พร้อมทั้งภาพประกอบ และสื่ออื่นๆ ที่สามารถดาวน์โหลดได้

ห้องสมุดสื่อบันทึกเสียงข่าวประเสริฐของจีอาร์เอ็น - เจ็ดสิบกว่าปีที่นักบันทึกเสียงขององค์กรจีอาร์เอ็นได้บันทึกเสียงภาษาของชนกลุ่มน้อยต่างๆ และได้ผลิตสื่อบันทึกเสียงข่าวประเสริฐมากมาย

Copyright and Licensing - GRN shares it's audio, video and written scripts under Creative Commons

Choosing the right audio or video format - What audio and video file formats are available from GRN, and which one is best to use?