unfoldingWord 37 - Yesu Amfufua Lazaro kutoka Wafu

unfoldingWord 37 - Yesu Amfufua Lazaro kutoka Wafu

เค้าโครง: John 11:1-46

รหัสบทความ: 1237

ภาษา: Swahili

ผู้ฟัง: General

ประเภท: Bible Stories & Teac

เป้าหมายของสื่อบันทึกเสียง: Evangelism; Teaching

ข้ออ้างอิงจากพระคัมภีร์: Paraphrase

สถานะ: Approved

บทความเป็นแนวทางพื้นฐานสำหรับการแปลและบันทึกเสียงภาษาอื่นๆ ควรดัดแปลงตามความจำเป็นเพื่อให้เข้าใจและเหมาะสมกับวัฒนธรรมและภาษาแต่ละภาษา คำศัพท์และแนวคิดบางคำที่ใช้อาจต้องอธิบายเพิ่มเติม หรือแทนที่ หรือตัดออก

เนื้อหาบทความ

Siku moja, Yesu alipata habari kuwa Lazaro ni mgonjwa sana. Lazaro na dada zake wawili- Martha na Maria walikuwa marafiki wa karibu wa Yesu. Yesu alipopata habari hizi alisema, "Huu si ugonjwa wa kifo, bali ni ugonjwa wa kumtukuza Mungu." Yesu aliwapenda marafiki zake, lakini alisubiri hadi siku mbili.

Baada ya siku mbili, Yesu aliwaambia wanafunzi wake, ''Twendeni tena Uyahudi." "Lakini mwalimu. " Wanafunzi wake walisema, "Muda mfupi tu uliopita watu walitaka kukuua!" Yesu alisema "Rafiki yetu Lazaro amelala usingizi na ni lazima nimwamshe."

Wanafunzi wa Yesu walijibu, "Bwana, kama Lazaro amelala, basi atapata nafuu." Yesu aliwaambia wazi, "Lazaro amekufa, nafurahi kuwa sikuwepo ili mpate kuniamini."

Yesu alipofika katika mji wa Lazaro, Lazaro alikuwa tayari amekufa kwa siku nne. Martha alikwenda kumwona Yesu akasema, "Bwana, kama ungekuwa hapa, kaka yangu asingekufa . Lakini ninaamini kuwa Mungu atakupa chochote umwombacho."

Yesu akajibu akasema, "Mimi ni Ufufuo na Uzima, yeyote aniaminiye ataishi, hata kama akifa. Kila aniaminiye hatakufa. Unaamini hivyo?" Martha akajibu, "Ndiyo Bwana ninaamini kuwa wewe ni Masihi, Mwanawa Mungu."

Maria alipofika. Alianguka miguuni pa Yesu akasema, "Bwana, kama wewe tu ungekuwepo kaka yangu asingekufa." Yesu akawauliza, "Mmemuweka wapi Lazaro?" Walimjibu " Kaburini, njoo uone." Yesu alilia.

Kaburi lilikuwa pango limefunikwa na jiwe. Yesu alipofika kaburini aliwaambia, "Liondoeni jiwe." Lakini Martha alisema, "Amekuwa kaburini sasa siku nne, ananuka!"

Yesu alijibu, "Je, sikusema kuwa kama ukiniamini utaona utukufu wa Mungu?" Ndipo wakaliondoa jiwe.

Basi Yesu alitazama juu mbinguni akasema, "Baba, asante kwa kuwa unanisikia. Tena najua wewe hunisikia siku zote. Lakini nimesema haya kwa ajili ya watu hawa waliosimama hapa, kwa kuwa wataamini kuwa ulinituma." Kisha Yesu akapaza sauti, "Lazaro, njoo nje."

Ndipo Lazaro alitoka nje! Alikuwa bado amefungwa sanda, Yesu akawaambia, "Msaidieni kuondoa sanda na mwacheni huru!." Wayahudi wengi walimwamini Yesu kwa sababu ya muujiza huu.

Lakini viongozi wa dini ya kiyahudi waliona wivu, ndipo wakakusanyika pamoja kupanga watakavyoweza kumuua Yesu na Lazaro.

ข้อมูลที่เกี่ยวข้อง

สื่อบันทึกเสียงรูปแบบmp3, ซีดี, เทปคาสเซ็ท - องค์กรจีอาร์เอ็น มีสื่อบันทึกเสียงต่างๆ หลายพันภาษา เนื้อหาสื่อบันทึกเสียงตรงกับความจริงในพระคัมภีร์ เป็นเรื่องราวเกี่ยวกับความรอดและชีวิตคริสเตียน

ดาวน์โหลดฟรี - ที่นี่ท่านสามารถค้นหาบทความต่างๆ ของจีอาร์เอ็นในภาษาต่างๆ พร้อมทั้งภาพประกอบ และสื่ออื่นๆ ที่สามารถดาวน์โหลดได้

ห้องสมุดสื่อบันทึกเสียงข่าวประเสริฐของจีอาร์เอ็น - เจ็ดสิบกว่าปีที่นักบันทึกเสียงขององค์กรจีอาร์เอ็นได้บันทึกเสียงภาษาของชนกลุ่มน้อยต่างๆ และได้ผลิตสื่อบันทึกเสียงข่าวประเสริฐมากมาย

Copyright and Licensing - GRN shares it's audio, video and written scripts under Creative Commons

Choosing the right audio or video format - What audio and video file formats are available from GRN, and which one is best to use?