unfoldingWord 01 - Uumbaji

unfoldingWord 01 - Uumbaji

เค้าโครง: Genesis 1-2

รหัสบทความ: 1201

ภาษา: Swahili

หัวข้อ: Bible timeline (Creation)

ผู้ฟัง: General

ประเภท: Bible Stories & Teac

เป้าหมายของสื่อบันทึกเสียง: Evangelism; Teaching

ข้ออ้างอิงจากพระคัมภีร์: Paraphrase

สถานะ: Approved

บทความเป็นแนวทางพื้นฐานสำหรับการแปลและบันทึกเสียงภาษาอื่นๆ ควรดัดแปลงตามความจำเป็นเพื่อให้เข้าใจและเหมาะสมกับวัฒนธรรมและภาษาแต่ละภาษา คำศัพท์และแนวคิดบางคำที่ใช้อาจต้องอธิบายเพิ่มเติม หรือแทนที่ หรือตัดออก

เนื้อหาบทความ

Hivi ndivyo mwanzo wa kila kitu ulivyotokea. Mungu aliumba ulimwengu na vitu vyote katika siku sita. Maana nchi ilikuwa giza na tupu, na hakuna kilichokuwa kimeumbwa. Lakini Roho ya Mungu ilikuwa juu ya maji.

Ndipo Mungu akasema, "Na iwe mwanga." Na ikawa hivyo, Mungu aliona kuwa mwanga ni mzuri na akauita mchana, na akatenganisha kutoka giza, akauita usiku. Mungu aliumba mwanga siku ya kwanza ya uumbaji.

Siku ya pili ya uumbaji, Mungu alisema na kuumba anga juu ya dunia. Aliumba anga kwa kutenganisha na maji ya juu kutoka maji ya chini.

Siku ya tatu, Mungu alisema na kutenganisha maji na nchi kavu. Nchi kavu akaiita "dunia," na maji akayaita "bahari." Mungu aliona kila kitu alichokiumba ya kuwa ni chema.

Ndipo Mungu akasema, "Nchi izae aina zote za miti na mimea." Na ndivyo ilivyotokea. Mungu aliona kila kitu alichokiumba ni chema.

Katika siku ya nne ya uumbaji, Mungu alisema na kuumba jua, mwezi na nyota. Mungu aliviumba ili kuleta mwanga duniani na kuonesha mchana na usiku, nyakati na miaka. Mungu aliona alichokiumba ni chema.

Siku ya tano, Mungu alisema na kuumba vitu vyote viishivyo majini na ndege wote. Mungu aliona kuwa ni vyema, na akavibariki.

Siku ya sita ya uumbaji, Mungu alisema, "Na iwe wanyama wa aina zote katika nchi." Na ilitokea kama Mungu alivyosema. Wengine walikuwa wa shambani, wengine wa kutambaa na wa porini. Na ilitokea kama yeye alivyotamka. Na Mungu aliona kwamba ilikuwa ni vyema.

Ndipo Mungu akasema, "Na tumfanye mtu kwa mfano wetu kuwa kama sisi. Watakuwa na mamlaka juu ya dunia na wanyama wote."

Mungu alichukua vumbi, akamfanya mtu, na akapulizia uhai ndani yake. Akamwita Adamu kwa jina lake. Akatengeneza bustani ya Edeni akamweka aishi humo, na aitunze.

Katikati ya bustani, Mungu alipanda miti miwili muhimu- mti wa uzima na wa ujuzi wa mema na mabaya. Mungu alimwambia Adamu anaweza kula aina zote za miti isipokuwa mti wa ujuzi wa mema na mabaya. Kama akila tunda la mti huu, atakufa.

Mungu alisema, "Si vyema mtu kuwa peke yake." Lakini hakuna hata mnyama mmoja aliyeweza kuwa msaidizi wa Adamu.

Ndipo Mungu alimletea Adamu usingizi mzito. Akatoa ubavu mmoja kwa Adamu na kutengeneza mwanamke na akamleta kwake.

Adamu alipomwona, alisema, "Angalau! Huyu ni kama mimi! Ataitwa 'mwanamke' maana ametoka kwa mwanaume." Kwa maana mwanaume atamwacha baba na mama yake watakuwa pamoja na mkewe.

Mungu aliumba mwanamke na mwanaume kwa mfano wake. Akawabariki akasema, "zaeni watoto na wajukuu mkaijaze dunia." Mungu aliona kila kitu alichokifanya ni chema sana, na alifurahishwa sana na kila kitu. Hii ilitokea katika siku ya sita ya uumbaji wake.

Siku ya saba ilipofika, Mungu alikuwa amemaliza kazi yake.Hivyo Mungu alipumzika katika kila alichokifanya. Aliibariki siku ya saba akaifanya takatifu kwa sababu katika siku hii alipumzika. Hivyo ndivyo Mungu alivyoumba ulimwengu na kila kitu ndani yake.

ข้อมูลที่เกี่ยวข้อง

สื่อบันทึกเสียงรูปแบบmp3, ซีดี, เทปคาสเซ็ท - องค์กรจีอาร์เอ็น มีสื่อบันทึกเสียงต่างๆ หลายพันภาษา เนื้อหาสื่อบันทึกเสียงตรงกับความจริงในพระคัมภีร์ เป็นเรื่องราวเกี่ยวกับความรอดและชีวิตคริสเตียน

ดาวน์โหลดฟรี - ที่นี่ท่านสามารถค้นหาบทความต่างๆ ของจีอาร์เอ็นในภาษาต่างๆ พร้อมทั้งภาพประกอบ และสื่ออื่นๆ ที่สามารถดาวน์โหลดได้

ห้องสมุดสื่อบันทึกเสียงข่าวประเสริฐของจีอาร์เอ็น - เจ็ดสิบกว่าปีที่นักบันทึกเสียงขององค์กรจีอาร์เอ็นได้บันทึกเสียงภาษาของชนกลุ่มน้อยต่างๆ และได้ผลิตสื่อบันทึกเสียงข่าวประเสริฐมากมาย

Copyright and Licensing - GRN shares it's audio, video and written scripts under Creative Commons

Choosing the right audio or video format - What audio and video file formats are available from GRN, and which one is best to use?