unfoldingWord 36 - Kubadilika Sura
![unfoldingWord 36 - Kubadilika Sura](https://static.globalrecordings.net/300x200/z40_Mt_17_05.jpg)
План-конспект: Matthew 17:1-9; Mark 9:2-8; Luke 9:28-36
Номер текста: 1236
Язык: Swahili
Aудитория: General
Цель: Evangelism; Teaching
Features: Bible Stories; Paraphrase Scripture
статус: Approved
Сценарии - это основные инструкции по переводу и записи на другие языки. Их следует при необходимости адаптировать, чтобы сделать понятными и актуальными для каждой культуры и языка. Некоторые используемые термины и концепции могут нуждаться в дополнительном пояснении или даже полностью замещаться или опускаться.
Текст программы
![](https://static.globalrecordings.net/300x200/z40_Mt_17_01.jpg)
Siku moja, Yesu aliwachukua wanafunzi wake watatu Yakobo, Petro na Yohana. ( Mwanafunzi aitwae Yohana sio yule aliyembatiza Yesu.) Walipanda juu ya mlima mrefu kuomba pekeyao.
![](https://static.globalrecordings.net/300x200/z40_Mt_17_02.jpg)
Yesu akiwa anaomba uso wake ulibadilika na kung'aa kama jua na mavazi yake yakawa meupe kama mwanga, yalikua meupe sana zaidi awezavyo mtu duniani kuyafanya yang'ae.
![](https://static.globalrecordings.net/300x200/z40_Mt_17_03.jpg)
Ndipo Musa na nabii Eliya wakawatokea. Watu hawa waliishi duniani miaka mingi kabla. Waliongea na Yesu juu ya kifo chake ambacho kitatokea Yerusalemu siku chache baadae.
![](https://static.globalrecordings.net/300x200/z40_Mt_17_04.jpg)
Wakati Musa na Eliya wanaongea na Yesu, Petro akamwambia Yesu, "Ni vizuri sisi kuwa hapa, hivyo naomba tutengeneze nyumba tatu moja ya kwako, nyingine ya Eliya na nyingine ya Musa". Lakini Petro hakujua alinenalo.
![](https://static.globalrecordings.net/300x200/z40_Mt_17_05.jpg)
Wakati Petro anaongea wingu jeupe lilishuka na kuwazunguka na sauti ikatoka katika lile wingu ikisema " Huyu ni Mwanagu nimpendaye. Ninayependezwa naye msikilizeni yeye".Wale wanafunzi watatu waliogopa na kuanguka chini.
![](https://static.globalrecordings.net/300x200/z40_Mt_17_06.jpg)
Ndipo Yesu akawagusa na kuwaambia "Msiogope inukeni". walipotazama pembeni ni Yesu pekee ndiye aliyebaki pale.
![](https://static.globalrecordings.net/300x200/z40_Mt_17_07.jpg)
Yesu pamoja na wanafunzi wake watatu wakashuka kutoka mlimani. Yesu akawaambia "Msimwambie mtu yeyote yale yaliyotokea, siku chache baadae nitakufa kisha nitakua hai tena. Baada ya hapo mtawaambia watu."