unfoldingWord 40 - Yesu Anasulubiwa

unfoldingWord 40 - Yesu Anasulubiwa

Esboço: Matthew 27:27-61; Mark 15:16-47; Luke 23:26-56; John 19:17-42

Número do roteiro: 1240

Idioma: Swahili

Público alvo: General

Tipo: Bible Stories & Teac

Propósito: Evangelism; Teaching

Passagem bíblica: Paraphrase

Estado: Approved

Os roteiros são guias básicos para a tradução e gravação em outros idiomas. Devem ser adaptados de acordo com a cultura e a língua de cada região, para fazê-lo relevante. Certos termos e conceitos podem precisar de uma explicação adicional ou mesmo serem omitidos no contexto de certos grupos culturais.

Texto do roteiro

Baada ya askari kumdhihaki Yesu, walimpeleka kumsulibisha. walimlazimisha aubebe msalaba ambao ungetumika kumuua.

Askari walimpeleka Yesu eneo liitwalo "fuvu la kichwa" wakaipigilia miguu na mikono yake msalabani. Lakini Yesu akasema, "Baba wasamehe, kwa sababu hawajui wanalotenda." Pilato akaagiza waandike kwamba, "Mfalme wa Wayahudi" ikiwa ni ishara; na waweke msalabani, juu ya kichwa cha Yesu.

Askari walipigia kura mavazi yake. Na kitendo hiki kinatimiza unabii usemao kwamba, " wakagawana nguo zangu na kucheza kamali."

Yesu alisulibiwa katikati ya wanyang'anyi wawili; mmojawapo alimdhihaki Yesu, lakini mwingine alisema, "Humwogopi Mungu!? Sisi tunahatia, lakini huyu hana hatia" Ndipo yeye akamwabia Yesu "Tafadhali unikumbuke katika ufalme wako" Yesu akamjibu, leo, utakuwa nami Paradiso."

Viongozi wa wayahudi na baadhi ya wengine katika umati walimdhihaki Yesu. Wakisema, "kama wewe ni Mwana wa Mungu, shuka msalabani, jiokoe mwenyewe, ndipo tutakuamini."

Ndipo katika eneo hilo kukawa giza nene, ingawa ilikuwa mchana. Mchana huo kukawa giza kwa saa tatu.

Yesu akalia, "Baba imekwisha naweka mikononi mwako roho yangu." Ndipo akainama akajitoa mwenyewe roho yake. Alipokufa lilitokea tetemeko la ardhi na pazia la hekaluni lililowatenga watu na Mungu lilipasuka vipande viwili, tokea juu hadi chini.

Kifo chake Yesu kinafungua njia ili watu waje kwa Mungu. Askari aliyemlinda Yesu alipoona mambo haya yote yanatokea alisema, "Hakika mtu huyu hakuwa na hatia, alikuwa Mwana wa Mungu."

Na ndipo Yusufu na Nikodemo viongozi wa Wayahudi walioamini Yesu kuwa ni Masihi wakauomba mwili wa Yesu na kuufunga kwenye sanda na kupeleka kwenye kaburi lililochongwa tayari mwambani na wakasogeza jiwe kubwa kulifunga kaburi.

Informações pertinentes

Palavras de Vida - A GRN tem mensagens evangelísticas em áudio em milhares de idiomas contendo a mensagem bíblica sobre a salvação e a vida cristã.

Downloads gratuitos - Baixe gratuitamente áudios de histórias bíblicas e estudos em milhares de idiomas, além de ilustrações, roteiros e vários outros tipos de material para evangelismo e crescimento da igreja.

Coleção de áudio da GRN - Material evangelístico e de ensino bíblico, adaptado às necessidades e cultura de cada povo em vários estilos e formatos.

Copyright and Licensing - GRN shares it's audio, video and written scripts under Creative Commons

Choosing the right audio or video format - What audio and video file formats are available from GRN, and which one is best to use?