unfoldingWord 42 - Yesu Anarudi Mbinguni

unfoldingWord 42 - Yesu Anarudi Mbinguni

Samenvatting: Matthew 28:16-20; Mark 16:12-20; Luke 24:13-53; John 20:19-23; Acts 1:1-11

Scriptnummer: 1242

Taal: Swahili

Gehoor: General

Genre: Bible Stories & Teac

Doel: Evangelism; Teaching

Bijbelse verwijzing: Paraphrase

Toestand: Approved

De scripts dienen als basis voor de vertaling en het maken van opnames in een andere taal. Ze moeten aangepast worden aan de verschillende talen en culturen, om ze zo begrijpelijk en relevant mogelijk te maken. Sommige termen en begrippen moeten verder uitgelegd worden of zelfs weggelaten worden binnen bepaalde culturen.

Tekst van het script

Siku ile Yesu alipofufuka, wanafunzi wake wawili walikuwa wanaenda mji jirani. Wakiendelea kutembea, walizungumza habari zilizotokea kumuhusu Yesu. Walitumaini kuwa alikuwa Masihi, lakini aliuawa. Wanawake waliwaambia yu hai anaishi tena. Nao hawakujua cha kuamini.

Yesu aliwakaribia na akaanza kutembea nao, lakini hawakumtambua. Aliwauliza juu ya mazungumzo yao, nao wakamueleza maajabu yote yaliyo tokea kumuhusu Yesu kwa siku chache zilizopita. Kwani walidhani wanaongea na mgeni asiyejua habari zilizotokea katika Yerusalemu.

Ndipo Yesu akawaelezea jinsi neno la Mungu linavyo sema kumuhusu Masihi. Aliwakumbusha manabii walivyosema, kwamba Masihi atateswa na kuuawa, na atafufuka tena siku ya tatu. Nao walipofika katika mji waliokuwa wamepanga kufikia hawa wanaume wawili, ilikuwa imekaribia jioni.

Hawa wanaume wawili walimkaribisha Yesu akae nao, naye akafanya hivyo. Walipokuwa tayari kula chakula cha jioni, Yesu alichukua kipande cha mkate, alimshukuru Mungu kwa mkate huo, akaumega. Ghafla, wakamtambua kuwa ni Yesu. Lakini wakati huo huo, Yesu akatoweka eneo hilo.

Hawa wanaume wawili waka ambiana, "Yule alikuwa ni Yesu! Ndiyo maana mioyo yetu ilikuwa inaungua wakati akielezea neno la Mungu kwetu." Punde, walirudi Yerusalemu. Nao walipofika, waliwaambia wanafunzi, "Yesu yu hai! tumemuona."

Wakati wanafunzi wanaendelea kuongea, Yesu alijitokeza katikati yao kwenye kile chumba na kusema, "Amani iwe kwenu!" Wanafunzi walidhani kuwa ni mzimu, lakini Yesu akawaambia, "Mbona mnaogopa na kuwa na mashaka? Angalieni mikono yangu na miguu. Mizimu haina mwili kama mimi." Kuwahakikishia kuwa Yeye si mzimu, aliwaomba chakula. Walimpa kipande cha samaki kilichopikwa, naye akala.

Yesu alisema, "Niliwaambia kila kitu kilicho andikwa katika neno la Mungu kunihusu mimi ni lazima kitimie." Ndipo alipofungua akili zao ili waweze kulielewa neno la Mungu. Akasema, "Iliandikwa muda mrefu uliopita yakuwa Masihi atateswa, atakufa na kufufuka kwa wafu siku ya tatu."

Iliandikwa pia katika maandiko kwamba wanafunzi, wangu watatangaza kwa kila mtu katika makundi, kwamba lazima watubu ili wapate msamaha wa dhambi zao. Nao watafanya hivyo kuanzia Yerusalem, nao wataenda kwa watu wote mahali pote. Ninyi ni mashahidi wa mambo haya.

Ndani ya siku arobaini zilizofuata, Yesu aliwatokea wanafunzi wake mara kwa mara. Wakati mwingine aliwatokea watu zaidi ya 500 kwa wakati mmoja! aliwadhibitishia wanafunzi wake kwa njia nyingi kuwa Yeye yu hai, na aliwafundisha kuhusu ufalme wa Mungu.

Yesu akawaambia wanafunzi wake, "Nimepewa mamlaka yote mbinguni na duniani. Kwa hiyo nendeni mkawafanye watu wote kuwa wanafunzi wangu, mkiwabatiza kwa jina la Mungu Baba, Mwana, na Roho Mtakatifu, mkiwafundisha kuyatii yote niliyowaamuru. Kumbukeni kuwa nitakuwa pamoja nanyi siku zote."

Siku arobaini baada ya Yesu kufufuka kwa wafu, aliwaambia wanafunzi wake, "Kaeni Yerusalemu mpaka hapo Baba yangu atakapo wapa nguvu, pale Roho Mtakatifu atakapowajilia ninyi. Kisha Yesu akaenda mbinguni, nayo mawingu yakamfunika akatoweka kwao. Yesu alikaa mkono wa kuume wa Mungu kutawala vitu vyote.

Verwante informatie

Woorden van Leven - GRN beschikt over audio opnamen in duizenden talen. Deze opnamen gaan over het verlossingsplan en het leven als christen.

Vrij te downloaden - Download Bijbelverhalen in audio formaat en Bijbellessen in duizenden talen, afbeeldingen, scripts en andere verwante materialen die geschikt zijn voor evangelisatie en gemeenteopbouw.

De GRN-audiobibliotheek - Evangelisatiemateriaal en basisbijbelonderricht, aangepast aan de behoeften en de cultuur van het volk, in verschillende stijlen en formaten.

Copyright and Licensing - GRN shares it's audio, video and written scripts under Creative Commons

Choosing the right audio or video format - What audio and video file formats are available from GRN, and which one is best to use?