unfoldingWord 45 - Stephano na Filipo

unfoldingWord 45 - Stephano na Filipo

개요: Acts 6-8

스크립트 번호: 1245

언어: Swahili

청중: General

장르: Bible Stories & Teac

목적: Evangelism; Teaching

성경 인용: Paraphrase

지위: Approved

이 스크립트는 다른 언어로 번역 및 녹음을위한 기본 지침입니다. 그것은 그것이 사용되는 각 영역에 맞게 다른 문화와 언어로 조정되어야 합니다. 사용되는 몇 가지 용어와 개념은 다른 문화에서는 다듬어지거나 생략해야 할 수도 있습니다.

스크립트 텍스트

Mmoja wa viongozi wa Kanisa la kwanza aliyeitwa Stephano. Alikuwa na tabia nzuri, mwenye kujawa na Roho Mtakatifu na hekima. Stephano alifanya miujiza mingi na kutumia ushawishi mkubwa illi watu wapate kumwamini Yesu.

Siku moja wakati Stephano anafundisha habari za Yesu, baadhi ya Wayahudi wasiomwamini Yesu walianza kubishana na Stephano. Walikasirika sana na kusema uongo kinyume cha Stephano kwa viongozi wa kidini. Wakasema, "Tumemsikia akisema vibaya juu ya Musa na Mungu!" Hivyo viongozi wa kidini walimkamata Stephano na kumpeleka kwa Kuhani Mkuu na viongozi wengine wa kiyahudi mahali ambapo mashahidi wengine zaidi walishuhudia uongo juu ya Stephano.

Kuhani Mkuu akamwuliza Stephano, "Maneno hayo ni ya kweli?" Stephano aliwajibu kwa kuwakumbusha mambo mengi makuu ambayo Mungu ameyafanya kutoka Ibrahimu hata wakati wa Yesu, jinsi ambavyo watu wa Mungu waliendelea kutomtii Mungu. Ndipo aliposema, "Enyi watu wagumu na waasi kila mara mnamkataa Roho Mtakatifu, kama wazazi wenu walivyomkataa Mungu na kuwaua manabii wake. Na nyinyi mmefanya jambo baya zaidi kuliko wao! Mmemwua Masihi."

Viongozi wa kidini ya kiyahudi waliposikia hayo, walikasirika, wakaziba masikio yao na kupaza sauti kubwa. Walimburuta Stephano kwa nguvu na kumpeleka nje ya mji na kumponda kwa mawe ili kumwua.

Stephano alipokaribia kufa, alilia kwa sauti, "Ee Yesu, pokea roho yangu." Ndipo alipopiga magoti na kusema tena, "Bwana, usiwahesabie dhambi hii." Baadaye akafa.

Kijana mmoja aitwaye Sauli alikubaliana na watu waliomwua Stephano na akalinda nguo zao walipokuwa wanamponda mawe. Tangu siku hiyo, watu wa Yerusalemu wakaanza kuwatesa wafuasi wa Yesu, hivyo waamini wakakimbia kwenda sehemu zingine. Licha ya hayo, walihubiri habari za Yesu popote walipoenda.

Mwanafunzi wa Yesu jina lake Filipo, alikuwa mmoja wa waumini waliokimbia kutoka Yerusalemu wakati wa mateso. Alienda Samaria alipohubiri habari za Yesu na watu wengi wakaokolewa. Ndipo siku moja malaika kutoka kwa Bwana akamwambia Filipo kwenda katika njia fulani jangwani. Alipokuwa akitembea barabarani, Filipo alimuona afisa mashuhuri kutoka nchi ya Ethiopia akiwa amepanda gari lake. Roho Mtakatifi alimwambia aende kukutana na kuzungumza na mtu huyo.

Filipo alipolikaribia gari, alimsikia mu-Ethiopia akisoma kile ambacho nabii Isaya aliandika. Huyo mtu alisoma, "Walimwongoza kama mwanakondoo na kumwua, kama mwanakondoo, alikaa kimya bila kusema neno. Walimtendea vibaya na hata hawakumheshimu. Walitoa uhai wake na kumwua."

Filipo alimwuliza huyo mtu wa Ethiopia, "Unaelewa kile unachokisoma?" Yule mtu akajibu, "Hapana. Siwezi kuelewa isipokuwa awepo mtu wa kunielezea. Tafadhali njoo ukae pamoja nami. Isaya aliandika kuhusu yeye au juu ya mtu mwingine?"

Filipo alimuelezea Muethiopia kuwa Isaya aliiandika juu ya Yesu. Vile vile Filipo alitumia maandiko mengine kumuelezea habari njema za Yesu.

Filipo na yule mtu wa Ethiopia walipokuwa wanasafiri, walifika kwenye maji. Muethiopia akasema, "Tazama! Kuna maji hapa! Je naweza kubatizwa?" Akamwambia dereva wake kusimamisha gari.

Kwa hiyo walienda kwenye maji, na Filipo akambatiza yule mtu wa Etheopia. Baada ya kutoka majini, ghafla Roho Mtakatifu alimwondoa Filipo na kumpeleka mahali pengine kuendelea kuwaambia watu habari za Yesu.

Yule mtu wa Ethiopia aliendelea na safari yake kwenda nyumbani akimfurahia za Mungu kuwa amemjua Kristo.

관련정보

생명의 말씀 - GRN 은 성경에 기반한 구원과 그리스도인의 삶에 대한 수천개의 오디오 복음 메시지를 가지고 있습니다.

무료 다운로드 - 여기에서 다운로드 가능한 여러 언어로 된 주요 GRN 메시지 스크립트, 그림 및 기타 관련 자료를 찾을 수 있습니다.

GRN 오디오 도서관 - 전도와 기본 성경 가르침을 위한 자료는 mp3, CD, 카세트 테이프 형태로 사람들의 필요와 문화에 맞추어졌습니다. 녹음은 성경이야기, 전도 메시지, 말씀 읽기, 노래를 포함하여 다양한 스타일로 구성되었습니다.

Copyright and Licensing - GRN shares it's audio, video and written scripts under Creative Commons

Choosing the right audio or video format - What audio and video file formats are available from GRN, and which one is best to use?