unfoldingWord 39 - Yesu Anashitakiwa

unfoldingWord 39 - Yesu Anashitakiwa

개요: Matthew 26:57-27:26; Mark 14:53-15:15; Luke 22:54-23:25; John 18:12-19:16

스크립트 번호: 1239

언어: Swahili

청중: General

장르: Bible Stories & Teac

목적: Evangelism; Teaching

성경 인용: Paraphrase

지위: Approved

이 스크립트는 다른 언어로 번역 및 녹음을위한 기본 지침입니다. 그것은 그것이 사용되는 각 영역에 맞게 다른 문화와 언어로 조정되어야 합니다. 사용되는 몇 가지 용어와 개념은 다른 문화에서는 다듬어지거나 생략해야 할 수도 있습니다.

스크립트 텍스트

Ilikuwa usiku wa manane wakati huo. Askari wakampeleka kwenye nyumba ya kuhani mkuu ili kumhoji. Petro akawafuata kwa mbali nyuma yao. Wakati Yesu anachukuliwa kwenye nyumba, Petro alikuwa nje peke yake akiota moto.

Ndani ya Nyumba viongozi wa kiyahudi wakamshitaki Yesu. Wakaleta mashahidi wengi wa uongo walioshuhudia uongo dhidi ya Yake. vile vile hata maelezo yao yalitofautiana kila mmoja alisema tofauti. kwa hiyo viongozi wa kiyahudi hawakukubaliana kama alikuwa na hatia yeyote. Yesu hakusema chochote.

Hatimaye kuhani mkuu akamwangalia Yesu na kusema "Tuambie wewe ni Masihi mwana wa Mungu aliye hai?"

Yesu akamjibu, "Mimi ndiye, utaniona nimekaa na Mungu na pia nikishuka kutoka mbinguni" Kuhani mkuu akararua mavazi yake kwa hasira na akasema kwa sauti kuu kwa viongozi wa kidini wengine "Hatuhitaji mashahidi zaidi ya hawa! Mmesikia toka kwake mwenyewe, akisema yeye ni mwana wa Mungu. Hukumu yenu ni ipi?"

Viongozi wa kiyahudi wote wakamjibu kuhani mkuu kuwa "Anastahili kufa" baadaye wakamfunika macho Yesu, wakamtemea mate, wakampiga, na kumdhihaki.

Na Petro alikuwa inje ya nyumba akisubiri. Mtumishi mmoja msichana akamwona na akamwambia "Na wewe pia ulikuwa na Yesu!" Petro akakana. baadaye binti mwingine akasema kitu hichohicho. Na petro akakataa tena. hatimaye watu wakasema "Tunajua wewe ulikuwa pamoja naye maana ninyi nyote ni wenyeji wa Galilaya.

Tena Petro akaapa, akisema, "Mungu wangu na anilaani kama mimi namjua mtu huyu!" Mara ghafla Jogoo akawika na Yesu akageuka kumwangalia Petro.

Petro akaondoka na akilia kwa huzuni kubwa. Wakati huo huo, Yuda, mwenye kumsaliti Yesu, akaona kwamba viongozi wa kiyahudi wamemweka Yesu hatiani. Yuda akapatwa na huzuni kubwa sana na akaondoka mahali pale akaenda kujiua mwenyewe.

Asubuhi na mapema, viongozi wa kiyahudi wakamleta Yesu kwa Pilato liwali wa Kirumi. wakitumaini kuwa Pilato atamhukumu Yesu kama mtu mwenye hatia na wakamwambia auawe. Pilato akamuuliza Yesu "Wewe ni mfalme wa wayahudi?"

Yesu akamjibu "Wewe ndiye umesema hivyo, lakini ufalme wangu si ufalme wa dunia hii, kama ingekuwa hivyo watumishi wangu wangepigana kwa ajili yangu. Nimekuja ulimwenuni ili kuusema ukweli kuhusu Mungu. na kila mmoja anayependa huu ukweli hunisikiliza. Pilato akasema "Ukweli ni nini?"

Baada ya kuongea na Yesu Pilato alitoka nje katika umati wa Watu na kusema "Nimeona hakuna hatia juu ya mtu huyu" lakini viongozi wa kiyahudi na makutano wote wakapiga kelele "Msulubishe" pilato akajibu "Hana hatia" lakini waliendelea kupiga kelele tena kwa nguvu. na Pilato akasema kwa mara ya tatu "Hana hatia yeyote"

Pilato akaogopa kwamba makutano wataanza kuleta Ghasia, kwa hiyo aliwaruhusu askari wake kumsulubisha Yesu. Askari wa Kirumi wakampiga Yesu huku wakimpa vazi la kifalme na kofia iliyotengenezwa na miiba wakamvika. pia wakamdhihaki kwa kusema "Mtazame mfalme wa wayahudi"

관련정보

생명의 말씀 - GRN 은 성경에 기반한 구원과 그리스도인의 삶에 대한 수천개의 오디오 복음 메시지를 가지고 있습니다.

무료 다운로드 - 여기에서 다운로드 가능한 여러 언어로 된 주요 GRN 메시지 스크립트, 그림 및 기타 관련 자료를 찾을 수 있습니다.

GRN 오디오 도서관 - 전도와 기본 성경 가르침을 위한 자료는 mp3, CD, 카세트 테이프 형태로 사람들의 필요와 문화에 맞추어졌습니다. 녹음은 성경이야기, 전도 메시지, 말씀 읽기, 노래를 포함하여 다양한 스타일로 구성되었습니다.

Copyright and Licensing - GRN shares it's audio, video and written scripts under Creative Commons

Choosing the right audio or video format - What audio and video file formats are available from GRN, and which one is best to use?