unfoldingWord 32 - Yesu Amponya Mwanamume Aliyepagawa - pepo na Mwanamke Mgojwa

unfoldingWord 32 - Yesu Amponya Mwanamume Aliyepagawa - pepo na Mwanamke Mgojwa

개요: Matthew 8:28-34; 9:20-22; Mark 5; Luke 8:26-48

스크립트 번호: 1232

언어: Swahili

청중: General

장르: Bible Stories & Teac

목적: Evangelism; Teaching

성경 인용: Paraphrase

지위: Approved

이 스크립트는 다른 언어로 번역 및 녹음을위한 기본 지침입니다. 그것은 그것이 사용되는 각 영역에 맞게 다른 문화와 언어로 조정되어야 합니다. 사용되는 몇 가지 용어와 개념은 다른 문화에서는 다듬어지거나 생략해야 할 수도 있습니다.

스크립트 텍스트

Siku moja Yesu na wanafunzi wake walipanda mashua kuelekea mjini, ambako waliishi watu wa Gerasini.

Na walipofika upande wa pili wa ziwa, na alikuwako mtu mwenye mapepo alimkimbilia Yesu.

Mtu huyu alikuwa mwenye nguvu na hapukuwa na mtu yeyote wa kumdhibiti. watu walimfunga kamba mikonom na miguuni mwake lakini bado aliweza kuzikata.

Mtu huyo aliishi maeneo ya makaburi na mtu huyu alitetemeka mchana na usiku kwa sababu hakuvaa nguo zozote na mwili wake alijikata kwa mawe.

Mtu huyo alipokuja kwa Yesu, alianguka mbele ya magoti yake. Na Yesu akaliaamuru lile pepo "limtoke mtu huyo".

Mtu huyo mwenye pepo akalia kwa sauti " unataka nini kwangu Yesu, mwana wa Mungu aliyetukuzwa juu? tafadhali usinitese" ndipo Yesu akaliuliza lile pepo " je unaitwa nani"? akajibu " jina langu ni legioni" na kwa sababu tupo wengi ( " legioni" kikundi cha wanajeshi maelfu katika vikosi vya rumi).

Yale mapepo yakamwomba Yesu " tafadhali usituondoe katika mji huu", na hapo palikuwa na kundi la nguruwe karibu na kilima, yale mapepo yakamwomba Yesu " tuamuru twende kwenye nguruwe hao" na Yesu akajibu "nendeni".

Yale mapepo yakamtoka yule mtu na kuwaingia wale nguruwe, Na wale nguruwe wakakimbilia huko chini bondeni kwenye ziwa........ na palikuwako na nguruwe 2000 kundini.

Na watu wale waliokuwa wakiwaangalia wale nguruwe walipoona hayo yakitokea, walikimbia na kuelekea mjini na huko wakamwambia kila mmoja yakuwa wamemkuta Yesu na aliyokuwa akitenda. Na watu wa mjini wakaenda na kumwona yule mtu aliekuwa na mapepo. Alikuwa amekaa kwa utulivu,amevaa nguo na alikuwa anaonekana kama mtu wa kawaida.

Watu waliogopa na wakamuomba Yesu aondoke, ndipo Yesu akapanda ndani ya mashua na akijiandaa kwa ajili ya kuondoka. na mtu yule aliekuwa na mapepo akamusihi Yesu aondoke pamoja naye.

Yesu akajibu " hapana, ondoka uende nyumbani na uwaeleze marafiki na familia yako kuhusu yote alivyokutendea Mungu na alivyokufanyia huruma yake kwako.

Ndipo mtu yule akaondoka na kumweleza kila mtu yale yote Yesu aliyomtendea. Na kila mtu aliye sikia simulizi hizi alishangaa na kusitaajabishwa.

Ndipo Yesu akarudi upande mwingine wa ziwa, na lipofika lilikuwako kundi kubwa la watu waliokusanyika wakimzunguka. na hapo alikuwapo mwanamke aliegua na kutokwa damu miaka kumi na miwili. Alilipa pesa yake yote kwa waganga ili wamponye lakini hali ilizidi kuwa ngumu.

Alisikia ya kuwa Yesu aliponya watu wengi na akafikiri" hakika kama nitagusa vazi la Yesu na mimi nitapona pia". hivyo akaja karibu na Yesu akamgusa vazi lake. na baada ya kumgusa tu, alipona na hakutokwa damu kwake kukaisha.

Na ndipo Yesu akagundua yakuwa nguvu zimemuishia, hivyo akageuka nyuma na kuuliza " je ni nani aliye nigusa", wanafunzi wakamjibu " kuna kundi kubwa la watu limekuzunguka na wakikugusa je ni kwa nini umeuliza "ni nani aliyenigusa"

Kisha yule mwanamke akaanguka magotini pa Yesu akitetemeka na kuogopa, akamwambia yale yote aliyo yatenda na alivyopokea uponyaji. Yesu akamwambia " enenda kwa amani, imani yako imekuponya.

관련정보

생명의 말씀 - GRN 은 성경에 기반한 구원과 그리스도인의 삶에 대한 수천개의 오디오 복음 메시지를 가지고 있습니다.

무료 다운로드 - 여기에서 다운로드 가능한 여러 언어로 된 주요 GRN 메시지 스크립트, 그림 및 기타 관련 자료를 찾을 수 있습니다.

GRN 오디오 도서관 - 전도와 기본 성경 가르침을 위한 자료는 mp3, CD, 카세트 테이프 형태로 사람들의 필요와 문화에 맞추어졌습니다. 녹음은 성경이야기, 전도 메시지, 말씀 읽기, 노래를 포함하여 다양한 스타일로 구성되었습니다.

Copyright and Licensing - GRN shares it's audio, video and written scripts under Creative Commons

Choosing the right audio or video format - What audio and video file formats are available from GRN, and which one is best to use?