unfoldingWord 16 - Wakombozi

unfoldingWord 16 - Wakombozi

개요: Judges 1-3; 6-8; 1 Samuel 1-10

스크립트 번호: 1216

언어: Swahili

청중: General

장르: Bible Stories & Teac

목적: Evangelism; Teaching

성경 인용: Paraphrase

지위: Approved

이 스크립트는 다른 언어로 번역 및 녹음을위한 기본 지침입니다. 그것은 그것이 사용되는 각 영역에 맞게 다른 문화와 언어로 조정되어야 합니다. 사용되는 몇 가지 용어와 개념은 다른 문화에서는 다듬어지거나 생략해야 할 수도 있습니다.

스크립트 텍스트

Baada ya Yoshua kufa, Waisraeli hawakumutii Mungu na hawakuwaondoa Wakanaani wala kuzitii amri za Mungu. Waisraeli walianza kuhabudu miungu ya Wakanaani badala ya Yehova, Mungu wa kweli. Waisraeli hawakuwa na mfalme, kwa hiyo kila mmoja alifanya alichofikiri ni sahihi.

Kwa sababu Waisraeli waliendelea kutomtii Mungu, aliwaadhibu kwa kuruhusu maadaui zao kuwashinda. Hawa maadui walichukua vitu kutoka kwa Waisraeli, wakaharibu mali zao na kuwaua wengi wao. Baada ya miaka mingi ya kutomtii Mungu na kuteswa na maadui, Waisraeli walitubu na kumuuomba Mungu awaokoe.

Baadaye Mungu alituma mkombozi aliyewaokoa kutoka kwa maadui zao na kuleta amani katika nchi. Lakini baadaye watu walimsahau Mungu na kuunza kuhabudu miungu yao tena. Kwa hiyo Mungu akaruhusu Wamidiani, kundi la watu maadui wakaribu, kuwashinda.

Wamidiani walichukua mazao yote ya Waisrael kwa miaka saba. Waisraeli wakaogopa sana; wakajificha mapangoni ili Wamidiani wasiwapate. Hatimaye, wakamuomba Mungu awaokoe.

Siku moja, mtu wa Israeli jina lake Gidioni alikuwa akipura ngano katika sehemu ya siri ili Wamidiani wasije wakaiba. Malaika wa Yehova alimtokea Gidioni na kusema "Usiogope, Mungu yuko pamoja na wewe. Nenda ukawaokoe Waisraeli kutoka kwa Wamidiani."

Baba yake Gidioni alikuwa na madhabahu aliyoweka wakifu kwa mungu. Mungu akamwambia Gidioni kuvunja madhabahu hiyo. Lakini Gidioni aliogopa watu, hivyo akasubiri hadi ilipofika wakati wa usiku. Kisha akaivunjavunja madhabahu vipande vipande. Akamjengea Mungu madhabahu mpya karibu na ilipokuwa madhabahu ya mungu na kumtolea Mungu sadaka juu yake.

Asubuhi yake watu waliona mtu fulani amevunja na kuharibu madhabahu, na wakakasirika sana. Wakaenda nyumbani kwa Gidioni kumua, lakini baba yake Gidioni akasema, "Kwa nini mnajaribu kumsaidia mungu wenu? Kama ni mungu, muacheni ajilinde mwenyewe!" Kwa sababu alisema hayo, watu hawakumuua Gidioni.

Baadaye Wamidiani walikwenda tena kuiba kwa Waisraeli. Walikuwa wengi sana kiasi cha kutohesabika. Gidioni alikusanya Waisraeli pamoja ili kupigana nao. Gidioni akamuuliza Mungu ishara mbili zitakazompa uhakika kwamba Mungu atamtumia kuokoa Israeli.

Kwa ishara ya kwanza, Gidioni alitandika ngozi ya kondoo juu ya ardhi na akamwambia Mungu kuwa umande wote ufikie juu ya hiyo ngozi tu na sio juu ya ardhi. Mungu akafanya kama alivyoomba. Usiku uliofuata, akaomba ardhi ilowane maji lakini ngozi ibaki kuwa kavu. Na Mungu akafanya kama alivyoomba pia. Ishara hizi mbili zilimhamasisha Gidioni kuwa Mungu atamtumia kuwaokoa Waisraeli kutoka kwa Wamidiani.

Maaskari 32,000 wa Kiisraeli walikwenda kwa Gidioni, lakini Mungu akamwambia kuwa hao ni wengi mno. Ndipo Gidioni akawarudisha 22,000 waliokuwa na hofu ya kupigana. Mungu akamwambia Gidioni kuwa bado ana wanaume wengi sana. Hivyo Gidioni kuwarudisha wote nyumbani isipokuwa maaskari 300.

Usiku huo ndipo Mungu akamwambia Gidioni, " Shuka chini kwenye kambi ya Wamidiani na utakaposikia wanachoongea, usiogope." Kwa hiyo usiku huo, Gidioni akashuka chini kambini kwa Wamidiani na akasikia askari midiani akimwambia rafiki yake kuhusu ndoto aliyoota. Rafiki yake akamwambia, "Ndoto hii inamaanisha kwamba jeshi la Gidioni litashinda jeshi la Wamidiani!" Gidioni aliposikia hivyo akamwabudu Mungu.

Baadaye Gidioni akarudi kwa wanajeshi wake na kuwapa pembe, vyungu na kurunzi. Wakazunguka kambi ambayo Wamidiani walikuwa wamelala. Maaskari 300 wa Gidioni walikuwa na kurunzi zilizokuwa zimefichwa ndani ya vyungu ili kwamba Wamidiani wasije wakaona mwanga wa hizo kurunzi.

Ndipo, wanajeshi wote wa Gidioni walipovunja vile vyungu kwa pamoja, ghafla pakatokea mwanga wa kurunzi. Wakatoa pembe zao na kupaza sauti, "Upanga kwa Yehova na kwa Gidioni!"

Mungu aliwachanaganya Wamidiani, kiasi kwamba walianza kupigana na kuuwana wao kwa wao. Mara ghafla, Waisraeli wengine waliitwa kutoka kwenye miji yao ili kuja kusaidia kufukuza Wamidiani. Wakawaua wengi wao na kuwafukuza waliobaki kutoka katika nchi ya Waisraeli. Wamidiani 120,000 waliuwawa siku hiyo. Mungu akaiokoa Israeli.

Watu walitaka kumuweka Gidioni kuwa mfalme wao. Lakini Gidioni hakuwaruhusu kufanya hivyo, lakini akawaomba baadhi ya pete za dhahabu walizochukua kutoka kwa Wamidiani. Watu wakampatia Gidioni kiasi kikubwa cha dhahabu.

Baadaye Gidioni akatumia hizo dhahabu kutengeneza vazi maalumu kama lililokuwa likivaliwa na kuhani mkuu. Lakini watu wakaanza kulihabudi kana kwamba lilikuwa mungu. Kwa hiyo Mungu akaiadhibu Israeli tena kwa sababubu ya kuhabudu miungu. Mungu akaruhusu maadui wawashinde. Hatimaye walimuomba Mungu awasaidie tena, na Mungu aliwatumia mkombozi mwingine.

Tukio hili lilijirudia mara kwa mara: Waisraeli walipotenda dhambi, Mungu aliwaadhibu, walipotubu, na Mungu alituma mkombozi kwao. Yapata miaka mingi, Mungu alikuwa akituma wakombozi wa kuwaokoa Waisraeli kutoka kwa maadui zao.

Mwishowe, watu walimuomba Mungu awape mfalme kama mataifa mengine. Walitaka mfalme aliyekuwa mrefu na mwenye nguvu, na atakayeweza kuwaongoza vitani. Mungu hakupendezwa na ombi hilo, lakini akawapatia mfalme sawa na ombi lao.

관련정보

생명의 말씀 - GRN 은 성경에 기반한 구원과 그리스도인의 삶에 대한 수천개의 오디오 복음 메시지를 가지고 있습니다.

무료 다운로드 - 여기에서 다운로드 가능한 여러 언어로 된 주요 GRN 메시지 스크립트, 그림 및 기타 관련 자료를 찾을 수 있습니다.

GRN 오디오 도서관 - 전도와 기본 성경 가르침을 위한 자료는 mp3, CD, 카세트 테이프 형태로 사람들의 필요와 문화에 맞추어졌습니다. 녹음은 성경이야기, 전도 메시지, 말씀 읽기, 노래를 포함하여 다양한 스타일로 구성되었습니다.

Copyright and Licensing - GRN shares it's audio, video and written scripts under Creative Commons

Choosing the right audio or video format - What audio and video file formats are available from GRN, and which one is best to use?