unfoldingWord 09 - Mungu Anamwita Musa

unfoldingWord 09 - Mungu Anamwita Musa

개요: Exodus 1-4

스크립트 번호: 1209

언어: Swahili

청중: General

장르: Bible Stories & Teac

목적: Evangelism; Teaching

성경 인용: Paraphrase

지위: Approved

이 스크립트는 다른 언어로 번역 및 녹음을위한 기본 지침입니다. 그것은 그것이 사용되는 각 영역에 맞게 다른 문화와 언어로 조정되어야 합니다. 사용되는 몇 가지 용어와 개념은 다른 문화에서는 다듬어지거나 생략해야 할 수도 있습니다.

스크립트 텍스트

Yusufu alipofariki, ndugu zake walidumu kuishi huko Misri. Wao pamoja na wazazi wao, kwa miaka mingi waliongezeka na walikuwa na watoto wengi. Kabila hilo waliitwa Waisraeli

Mamia ya miaka mingi ilipita, wakazidi kuongezeka. Wamisri walimsahau Yusufu na kazi nzuri alizozifanya kwa Wamisri. Wamisri waliwaogopa Waisraeli kwa kuwa walikuwa wengi na Farao wa kipindi hicho aliwafanya kuwa watumwa kwa Wamisri.

Waisraeli walitumikishwa na Wamisri kwa kazi ngumu kwa kujenga majumba na miji mikubwa. Ugumu wa kazi ulisababisha huzuni kimaisha. Bali baraka za Mungu ziliwazidishia watoto kwa wingi.

Farao aliona kuwa Waisraeli walikuwa wanazaa watoto wengi, aliamuru watoto wa kiume wauawe kwa kutupwa katika mto Naili.

Mtoto wa kiume alizaliwa na mama mmoja wa Kiisraeli. Wazazi wa mtoto huyo walimficha kwa muda walioweza.

Mtoto huyo alipokuwa hawezi kufichika tena, ili kumuokoa wazazi walimweka katika kikapu kieleacho na kukiweka katika majani kando ya mto Naili. Ili kujua kuwa ni jambo gani lingempata mtoto huko mtoni dada yake alikuwa akifanya uchunguzi.

Mtoto wa kike wa Farao aliona kikapu na alichungulia ndani yake. Alipoona mtoto, alimchukua awe wake na kumwajiri mwanamke wa Kiyahudi amtunze. Bila kutambua, mama huyo mlezi ndiye alikuwa mzazi wa mtoto huyo. Mtoto alipoacha kunyonya alikabidhiwa kwa binti Farao naye akamwita jina lake Musa.

Akiwa mtu mzima, siku moja Musa alimkuta Mmisri akimpiga mtumwa wa Kiisraeli. Na alijitahidi kumuokoa Mwisraeli mwenzake.

Musa alimuua Mmisri na kuuzika mwili wake akidhani kwamba hakuna mtu ambaye angemwona. Kumbe mtu mmoja alimwona akifanya kitendo hicho.

Habari za mauaji zilipomfikia Farao, aliazimia kumuua Musa. Musa alitoroka kutoka Misri na kukimbilia nyikani ili kujiokoa na walinzi wa Farao.

Musa alikuwa mchungaji wa kondoo huko nyikani mbali na nchi ya Misri. Alioa huko na kuzaa watoto wawili wa kiume.

Siku moja Musa alikuwa akichunga kondoo wake, aliona kichaka kilichowaka moto bila kuteketea. Musa alisogea kuona vizuri, alipokaribia, Mungu alisikika akisema, "Musa vua viatu vyako. Ardhi uliyosimama juu yake ni takatifu".

Mungu alimwambia Musa," Nimeyaona mateso ya watu wangu. Ili kuwakomboa kutoka utumwani huko Misri, nitakutuma wewe kwa Farao ukawaondoe Waisraeli kutoka utumwani Misri. Nami nitawapa nchi ya Kanaani, niliyowaahidia Ibrahimu, Isaka na Yakobo."

Musa akauliza, watakapotaka kujua Ni nani aliyenituma kwao nisemeje? Mungu akasema, "MIMI NIKO AMBAYE NIKO. Waambie AMBAE NIKO amenituma. Mimi ni YEHOVA Mungu wa baba zenu Ibrahimu, Isaka na Yakobo. Jina langu ndilo hilo milele."

Musa hakutaka kwenda kwa Farao kwani aliogopa, kwa sababu alihofia kutoweza kuongea vizuri. Mungu alimruhusu Haruni nduguye amsaidie. Aliwaonya kuwa Farao atakuwa na moyo mgumu.

관련정보

생명의 말씀 - GRN 은 성경에 기반한 구원과 그리스도인의 삶에 대한 수천개의 오디오 복음 메시지를 가지고 있습니다.

무료 다운로드 - 여기에서 다운로드 가능한 여러 언어로 된 주요 GRN 메시지 스크립트, 그림 및 기타 관련 자료를 찾을 수 있습니다.

GRN 오디오 도서관 - 전도와 기본 성경 가르침을 위한 자료는 mp3, CD, 카세트 테이프 형태로 사람들의 필요와 문화에 맞추어졌습니다. 녹음은 성경이야기, 전도 메시지, 말씀 읽기, 노래를 포함하여 다양한 스타일로 구성되었습니다.

Copyright and Licensing - GRN shares it's audio, video and written scripts under Creative Commons

Choosing the right audio or video format - What audio and video file formats are available from GRN, and which one is best to use?