unfoldingWord 26 - Yesu Anaanza Huduma yake
![unfoldingWord 26 - Yesu Anaanza Huduma yake](https://static.globalrecordings.net/300x200/z42_Lk_04_13.jpg)
Контур: Matthew 4:12-25; Mark 1-3; Luke 4
Сценарий нөмірі: 1226
Тіл: Swahili
Аудитория: General
Жанр: Bible Stories & Teac
Мақсат: Evangelism; Teaching
Киелі кітап үзіндісі: Paraphrase
Күй: Approved
Сценарийлер басқа тілдерге аудару және жазу үшін негізгі нұсқаулар болып табылады. Оларды әр түрлі мәдениет пен тілге түсінікті және сәйкес ету үшін қажетінше бейімдеу керек. Пайдаланылған кейбір терминдер мен ұғымдар көбірек түсіндіруді қажет етуі немесе тіпті ауыстырылуы немесе толығымен алынып тасталуы мүмкін.
Сценарий мәтіні
![](https://static.globalrecordings.net/300x200/z42_Lk_04_09.jpg)
Baada ya kushinda majaribu ya Ibilisi Yesu alirudi kwa nguvu za Roho mtakatifu katika mkoa wa Galilaya. Yesu alienda sehemu moja baada ya nyigine akifundisha. Kila mmoja alisema vyema juu yake.
![](https://static.globalrecordings.net/300x200/z42_Lk_04_10.jpg)
Yesu akaenda mji wa Nazareti alikokuwa akiishi wakati wa utoto wake. Siku ya sabato, alienda sehemu ya kuabudia. wakamkabidhi chuo cha nabii isaya ili aweze kusoma. Yesu akakifungua chuo na kusoma sehemu yake mbele za watu.
![](https://static.globalrecordings.net/300x200/z42_Lk_04_11.jpg)
Yesu kasema "Bwana amenipa Roho wake ili kwamba nitangaze habari njema kwa maskini, uhuru kwa wafungwa, vipofu kuona, kutolewa waliodhurumiwa. huu ni mwaka wa Bwana uliokubalika.
![](https://static.globalrecordings.net/300x200/z42_Lk_04_13.jpg)
Tena Yesu akaa chini "Kila mmoja akamsogelea na kumtazama. walijua aya aliyoisoma inamhusu masia. Yesu akasema "Maneno niliyosoma mbele yenu yanatokea sasa. watu wote wakashangaa. huyu si mwana wa Yusufu"? Walisema.
![](https://static.globalrecordings.net/300x200/z42_Lk_04_15.jpg)
Tena Yesu akasema "Ni kweli kwamba hakuna nabii anayekubalika katika mji wa kwao. Wakati wa nabii Eliya, kulikuwa na wajane katika Israeli. lakini mvua iliposimama bila kunyesha kwa miaka mitatu na nusu, Mungu hakumtuma Eliya kumsaidia mwanamke mjane kutoka Israel, badala yake alikuwa ni mjane kutoka taifa tofauti"
![](https://static.globalrecordings.net/300x200/z42_Lk_04_17.jpg)
Yesu akaendelea kusema "Kipindi cha nabii Elisha kulikuwa na watu wengi katika Israeli wenye magonjwa ya Ngozi. lakini Elisha hakumponya hata mmoja wao. lakini aliponya ugonjwa wa ngozi wa Naamani pekee aliyekuwa kamanda wa maadui wa Israel. watu waliokuwa wanamsikiliza Yesu walikuwa ni wayahudi. Kwa hiyo walipomsikia anasema hayo wakawa na hasira juu yake.
![](https://static.globalrecordings.net/300x200/z42_Lk_04_18.jpg)
Watu wa Nazareti wakamvuta Yesu mbali na mahali pa kuabudia na kumtupa nje ili wamwue. Lakini Yesu akaondoka Mbele yao na akauacha mji wa Nazaleti.
![](https://static.globalrecordings.net/300x200/z42_LK_04_22.jpg)
Tena Yesu alienda mpaka mkoa wa Galilaya na mkutano mkubwa wakaja kwake. wakawealeta watu wengi waliokuwa wagonjwa, au walemavu, kama wasioona, kutembea, kusikia au kuongea, na Yesu akawaponya.
![](https://static.globalrecordings.net/300x200/z41_Mk_09_22.jpg)
Watu wengi waliokuwa na mapepo ndani yao waliletwa kwa Yesu. Kwa amri ya Yesu aliwaamuru wawatoke watu hao, na waliendelea kupiga kelele "Wewe ni mwana wa Mungu!" Umati wa watu walishangaa na walimwabudu Mungu.
![](https://static.globalrecordings.net/300x200/z40_Mt_10_01.jpg)
Tena Yesu akachagua watu kumi na wawili ambao aliwaita mitume. Mitume walizunguka na Yesu tena walijifunza kutoka kwake.