unfoldingWord 09 - Mungu Anamwita Musa

unfoldingWord 09 - Mungu Anamwita Musa

概要: Exodus 1-4

スクリプト番号: 1209

言語: Swahili

観客: General

ジャンル: Bible Stories & Teac

目的: Evangelism; Teaching

聖書の引用: Paraphrase

状態: Approved

スクリプトは、他の言語への翻訳および録音の基本的なガイドラインです。スクリプトは、それぞれの異なる文化や言語で理解しやすく、関連性のあるものにするために、必要に応じて適応させる必要があります。使用される用語や概念の中には、さらに説明が必要な場合や、完全に置き換えたり省略したりする必要がある場合もあります。

スクリプトテキスト

Yusufu alipofariki, ndugu zake walidumu kuishi huko Misri. Wao pamoja na wazazi wao, kwa miaka mingi waliongezeka na walikuwa na watoto wengi. Kabila hilo waliitwa Waisraeli

Mamia ya miaka mingi ilipita, wakazidi kuongezeka. Wamisri walimsahau Yusufu na kazi nzuri alizozifanya kwa Wamisri. Wamisri waliwaogopa Waisraeli kwa kuwa walikuwa wengi na Farao wa kipindi hicho aliwafanya kuwa watumwa kwa Wamisri.

Waisraeli walitumikishwa na Wamisri kwa kazi ngumu kwa kujenga majumba na miji mikubwa. Ugumu wa kazi ulisababisha huzuni kimaisha. Bali baraka za Mungu ziliwazidishia watoto kwa wingi.

Farao aliona kuwa Waisraeli walikuwa wanazaa watoto wengi, aliamuru watoto wa kiume wauawe kwa kutupwa katika mto Naili.

Mtoto wa kiume alizaliwa na mama mmoja wa Kiisraeli. Wazazi wa mtoto huyo walimficha kwa muda walioweza.

Mtoto huyo alipokuwa hawezi kufichika tena, ili kumuokoa wazazi walimweka katika kikapu kieleacho na kukiweka katika majani kando ya mto Naili. Ili kujua kuwa ni jambo gani lingempata mtoto huko mtoni dada yake alikuwa akifanya uchunguzi.

Mtoto wa kike wa Farao aliona kikapu na alichungulia ndani yake. Alipoona mtoto, alimchukua awe wake na kumwajiri mwanamke wa Kiyahudi amtunze. Bila kutambua, mama huyo mlezi ndiye alikuwa mzazi wa mtoto huyo. Mtoto alipoacha kunyonya alikabidhiwa kwa binti Farao naye akamwita jina lake Musa.

Akiwa mtu mzima, siku moja Musa alimkuta Mmisri akimpiga mtumwa wa Kiisraeli. Na alijitahidi kumuokoa Mwisraeli mwenzake.

Musa alimuua Mmisri na kuuzika mwili wake akidhani kwamba hakuna mtu ambaye angemwona. Kumbe mtu mmoja alimwona akifanya kitendo hicho.

Habari za mauaji zilipomfikia Farao, aliazimia kumuua Musa. Musa alitoroka kutoka Misri na kukimbilia nyikani ili kujiokoa na walinzi wa Farao.

Musa alikuwa mchungaji wa kondoo huko nyikani mbali na nchi ya Misri. Alioa huko na kuzaa watoto wawili wa kiume.

Siku moja Musa alikuwa akichunga kondoo wake, aliona kichaka kilichowaka moto bila kuteketea. Musa alisogea kuona vizuri, alipokaribia, Mungu alisikika akisema, "Musa vua viatu vyako. Ardhi uliyosimama juu yake ni takatifu".

Mungu alimwambia Musa," Nimeyaona mateso ya watu wangu. Ili kuwakomboa kutoka utumwani huko Misri, nitakutuma wewe kwa Farao ukawaondoe Waisraeli kutoka utumwani Misri. Nami nitawapa nchi ya Kanaani, niliyowaahidia Ibrahimu, Isaka na Yakobo."

Musa akauliza, watakapotaka kujua Ni nani aliyenituma kwao nisemeje? Mungu akasema, "MIMI NIKO AMBAYE NIKO. Waambie AMBAE NIKO amenituma. Mimi ni YEHOVA Mungu wa baba zenu Ibrahimu, Isaka na Yakobo. Jina langu ndilo hilo milele."

Musa hakutaka kwenda kwa Farao kwani aliogopa, kwa sababu alihofia kutoweza kuongea vizuri. Mungu alimruhusu Haruni nduguye amsaidie. Aliwaonya kuwa Farao atakuwa na moyo mgumu.

関連情報

Free downloads - Here you can find all the main GRN message scripts in several languages, plus pictures and other related materials, available for download.

The GRN Audio Library - Evangelistic and basic Bible teaching material appropriate to the people's need and culture in a variety of styles and formats.

Choosing the audio or video format to download - What audio and video file formats are available from GRN, and which one is best to use?

Copyright and Licensing - GRN shares it's audio, video and written scripts under Creative Commons