Veldu tungumál

mic

unfoldingWord 33 - Simulizi ya Mkulima

unfoldingWord 33 - Simulizi ya Mkulima

Útlínur: Matthew 13:1-23; Mark 4:1-20; Luke 8:4-15  

Handritsnúmer: 1233

Tungumál: Swahili

Áhorfendur: General

Tilgangur: Evangelism; Teaching

Features: Bible Stories; Paraphrase Scripture

Staða: Approved

Forskriftir eru grunnleiðbeiningar fyrir þýðingar og upptökur á önnur tungumál. Þau ættu að vera aðlöguð eftir þörfum til að gera þau skiljanleg og viðeigandi fyrir hverja menningu og tungumál. Sum hugtök og hugtök sem notuð eru gætu þurft frekari skýringar eða jafnvel skipt út eða sleppt alveg.

Handritstexti

Siku moja, Yesu alikuwa akifundisha makutano wengi katika pwani ya ziwa. Na watu wengi walimfuata wapate kumsikiliza. Yesu aliingia ndani ya mashua mahali pa juu apate nafasi nzuri ya kuzungumza nao. Yesu alikaa kwenye mashua akawafundisha watu.

Yesu aliwasimulia hadithi," Mpanzi alikwenda kupanda mbegu shambani, alipokuwa akimwaga mbegu kwa kutumia mikono yake. Mbegu zingine ziliangukia kwenye njia, ndege wakazila zote."

Mbegu zingine zilianguka kwenye ardhi yenye mawe, nazo zikachipuka haraka. Lakini jua lilipowaka zote zika ungua, kwa sababu mizizi haikuweza kustawi vizuri katika ule udongo mchache, hivyo miche ile ikafa.

Mbegu zingine zilianguka kwenye miiba, nazo zikamea lakini zikasongwa na miiba. Kwa hiyo mbengu hizo hazikuweza kuzaa matunda.

Mbegu zingine ziliangukia penye udongo mzuri. Mbengu hizo ziliweza kustawi na kuzaa 30, 60 na 100 zaidi kadri ya wingi wake katika kupandwa. Aliye na masikio, na asikie.

Hadithi iliwachanganya watu. Naye Yesu akawafafanulia akasema, "mbegu ni neno la Mungu. Mbegu zilizoanguka kwenye njia, ni yule mtu anaye lisikia neno la Mungu, lakini halielewi. Shetani huja na kulichukua neno kwa mtu huyo."

“Ile ardhi ya udongo wa mawe, ni yule mtu anayelisikia neno na kulipokea kwa furaha. Lakini yajapotokea mateso na majaribu, hushindwa kustahimili na huanguka dhambini.”

“Ardhi yenye miiba, ni yule mtu anayelisikia neno la Mungu, lakini kwa kadri siku zinavyoendelea, utajiri, anasa za maisha humtenga na upendo wa Mungu. Matokeo yake, lile neno la Mungu alilolisikia halizai matunda.”

“Ule udongo mzuri ni yule mtu anaye lisikia neno la Mungu na kuliaminii hivyo huzaa matunda.”

Tengdar upplýsingar

Orð lífsins - Hljóðboðskapur í guðspjalli á þúsundum tungumála sem inniheldur biblíutengdan boðskap um hjálpræði og kristna lífsstíl.

Choosing the audio or video format to download - What audio and video file formats are available from GRN, and which one is best to use?

Copyright and Licensing - GRN shares its audio, video and written scripts under Creative Commons