unfoldingWord 28 - Kijana Tajiri Kiongozi

unfoldingWord 28 - Kijana Tajiri Kiongozi

Garis besar: Matthew 19:16-30; Mark 10:17-31; Luke 18:18-30

Nomor naskah: 1228

Bahasa: Swahili

Pengunjung: General

Jenis: Bible Stories & Teac

Tujuan: Evangelism; Teaching

Kutipan Alkitab: Paraphrase

Status: Approved

Naskah ini adalah petunjuk dasar untuk menerjemahkan dan merekam ke dalam bahasa-bahasa lain. Naskah ini harus disesuaikan seperlunya agar dapat dimengerti dan sesuai bagi setiap budaya dan bahasa yang berbeda. Beberapa istilah dan konsep yang digunakan mungkin butuh penjelasan lebih jauh, atau diganti atau bahkan dihilangkan.

Isi Naskah

Siku moja, kiongozi kijana tajiri alimwendea Yesu na kumuuliza, "mwalimu mwema nifanye kitu gani cha lazima ili niwe na uzima wa milele?" Yesu akamwambia, "kwanini unaniita mwema?" Kuna mmoja tu aliye mwema naye ni Mungu. Lakini ukitaka kuwa na uzima wa milele, tii sheria za Mungu.

"Ni mambo gani nahitaji kutii?" Aliuliza. Yesu akajibu, "usiuwe. Usizini. Usiibe. Usidanganye. Mheshimu baba yako na mama yako, na umpende jirani yako kama unavyojipenda mwenyewe.

Lakini kijana akasema, "Nimezitii sheria hizo zote tangu nikiwa kijana. Je, nahitaji kufanya nini bado ili niishi milele? Yesu alimwangalia na akampenda.

Yesu akajibu, kama unataka kuwa mkamilifu, nenda ukauze kila kitu ulichonacho na utoe pesa kwa maskini, na utakuwa na hazina mbinguni, kisha njoo unifuate.

Yule kijana aliposikia alichokisema Yesu, alihuzunika sana, kwa sababu alikuwa tajiri sana na hakutaka kutoa vitu vyote alivyomiliki. Akageuka na akaenda mbali na Yesu.

Kisha Yesu akawaambia wanafunzi wake, "Ni vigumu sana kwa watu matajiri kuingia katika ufalme wa Mungu! Ndiyo, ni rahisi zaidi kwa ngamia kupita katika tundu la sindano kuliko mtu tajiri kuingia katika ufalme wa Mungu

Wanafunzi waliposikia alichosema Yesu, walishikwa na mshangao na kusema, "Ni nani basi anaweza kuokolewa?"

Yesu akawatazama wanafunzi na kusema, "Kwa watu mambo haya hayawezekani, lakini kwa Mungu mambo yote yanawezekana".

Petro akamwambia Yesu, "Tumeacha kila kitu na kukufuata wewe. Je, tutapata thawabu gani?"

Yesu akajibu, "Kila mmoja aliyeacha nyumba, kaka, dada yake, baba, mama, watoto, au mali kwa ajili yangu atapokea mara 100 zaidi na pia atapokea uzima wa milele. Lakini wengi walio wa kwanza watakuwa wa mwisho, na wengi walio wa mwisho watakuwa wa kwanza."

Keterangan terkait

Firman Kehidupan - GRN mempunyai rekaman pesan Injil dalam ribuan bahasa berisikan pesan berdasarkan Alkitab tentang keselamatan dan kehidupan Kristiani.

Unduhan-Unduhan Gratis - Disini anda dapat menemukan semua pesan naskah GRN yang utama dalam beberapa bahasa, ditambah gambar dan materi terkait lainnya yang dapat diunduh.

Perpustakaan Audio GRN - Bahan pengabaran Injil dan pengajaran dasar Alkitab yang sesuai dengan kebutuhan masyarakat dan budaya dalam berbagai macam bentuk dan format.

Choosing the audio or video format to download - What audio and video file formats are available from GRN, and which one is best to use?

Copyright and Licensing - GRN shares it's audio, video and written scripts under Creative Commons