unfoldingWord 20 - Kuchukuliwa Mateka na Kurudi

unfoldingWord 20 - Kuchukuliwa Mateka na Kurudi

Grandes lignes: 2 Kings 17; 24-25; 2 Chronicles 36; Ezra 1-10; Nehemiah 1-13

Numéro de texte: 1220

Langue: Swahili

Audience: General

Genre: Bible Stories & Teac

Objectif: Evangelism; Teaching

Citation biblique: Paraphrase

Statut: Approved

Les scripts sont des directives de base pour la traduction et l'enregistrement dans d'autres langues. Ils doivent être adaptés si nécessaire afin de les rendre compréhensibles et pertinents pour chaque culture et langue différente. Certains termes et concepts utilisés peuvent nécessiter plus d'explications ou même être remplacés ou complètement omis.

Corps du texte

Ufalme wa Israel na ufalme wa Yuda walitenda dhambi mbele za Mungu. walivunja agano waliloweka na Mungu Sinai. Mungu aliwatuma Manabii wake kuwaonya ili watubu na kumuabudu yeye lakini walikataa.

Ndipo Mungu aliadhibu falme zote kwa kuruhusu maadui zao kuwapiga. Ufame wa Ashuru ulikua ni ufalme wenye nguvu, taifa korofi likaharibu ufalme wa Israel. katika ufalme wa Israel Waashuru waliwaua watu wengi sana na kuwanyang'anya kila kitu cha thamani kisha kuchoma moto sehemu kubwa ya ardhi yao.

Waashuru waliwakusanya viongozi wote, matajiri na watu wenye ujuzi kisha kuwapeleka Ashuru. Masikini ambao hawakuuawa ndio waliobaki Israeli.

Waashuru waliwaleta wageni ili waishi katika nchi ya Israel. Wageni hao walijenga miji iliyoharibiwa na kuoa waisrael waliobaki. Kizazi cha wana wa Israel waliooana wa wageni kiliitwa Wasamaria.

Watu wa ufame wa Yuda waliona jinsi ambavyo Mungu alivyowaadhibu watu wa Israel kwa kutokumtii na kumwamini Mungu. lakini waliendelea kuiabudu miungu na akiwemo Mungu wa wakaanani. Mungu alituma manabii kuwaonya lakini hawakusikia.

Takribani miaka 100 baada ya Waashuru kuharibu ufalme wa Israeli Mungu alimtuma Nebukadneza mfalme wa Babiloni kuvamia taifa la Yuda. Babiloni lilikua taifa ;enye nguvu. Mfalme wa Yuda akakubali kuwa mtumishi wa Nebukadneza na kulipwa pesa nyingi kila mwaka.

Miaka michace baadae Mfalme wa Yuda akasi juu ya Babiloni. Ndipo wababiloni wakarudi na kuuteka ufalme wa Yuda. Waliuvamia mji wa Yerusalem wakaharibu hekalu na kuchukua vitu vyote vya thamani vilivyokuwemo katika mji.

Kwa sababu ya uasi Askari wa Mfalme Nebukadneza waliwaua watoto wote wa mfalme wa Yuda mbele ya macho yake kisha wakamharibu macho yake. Baada ya hayo wakamchukua mfalme na kumpeleka gerezani Babiloni ili afie huko.

Mfalme Nebukadneza pamoja na jeshi lake waliwapeleka watu wengi wa Yuda Babiloni, wakawaacha masikini ili wafanye kazi katika mashamba. Kipindi ambacho watu wa Mungu walilazimishwa kuondoka nchi ya ahadi kiliitwa kipindi cha Mateka.

Japokua Mungu aliwaadhibu watu wake kwa dhambi zao kwa kuwafanya mateka lakini hakuwasahau watu wake na ahadi aliyowaahidi. Mungu aliendelea kuwaangalia na kuzungumza nao kupitia manabii. Aliwaahidi kua baada ya miaka sabini atawarudisha kwenye nchi ya ahadi.

Miaka sabini baadae mfalme wa Uajemi alimshinda Babiloni hivyo ufalme wa Uajemi ukachukua nafasi ya ufalme wa Babiloni. Waisrael wakaanza kuitwa wayahudi na wengi wao waliishi Babiloni. Wachache waliokua wazee waliikumbuka nchi ya Yuda.

Ufalme wa Uajemi ulikua na nguvu lakini ulikua na huruma kwa watu waliowateka. Baada ya Koreshi kua Mfalme wa Uajemi alitoa amri kuwa Myahudi yeyote anaetaka kurudi Yuda anaweza kuondoka uajemi na kurudi Yuda. Aliwapa pesa kwa ajili ya kujenga upya hekalu. Baada ya miaka sabini ya kuwa mateka wayahudi wachache walirudi Yuda katika mji wa Yerusalemu.

Waliporudi Yerusalemu walijenga upya hekalu pamoja na ukuta wa mji. Japokua walikua wakitawaliwa na watu wengine lakini walipata nafasi ya kuishi kwenye nchi ya ahadi na kumwabudu Mungu hekaluni.

Informations reliées

Mots de Vie - GRN présente des messages sonores évangéliques dans des milliers de langues à propos du salut et de la vie chrétienne.

Téléchargements gratuits - Ici vous allez trouver le texte pour les principaux messages GRN en plusieurs langues, plus des images et autres documents prêts à télécharger

La collection d'Enregistrements de GRN - Matériel d'évangélisation et d'enseignement biblique de base adapté aux besoins et à la culture du peuple, dans une variété de styles et de formats.

Choosing the audio or video format to download - What audio and video file formats are available from GRN, and which one is best to use?

Copyright and Licensing - GRN shares it's audio, video and written scripts under Creative Commons