unfoldingWord 07 - Mungu Anambariki Yakobo

unfoldingWord 07 - Mungu Anambariki Yakobo

Grandes lignes: Genesis 25:27-35:29

Numéro de texte: 1207

Lieu: Swahili

Audience: General

Objectif: Evangelism; Teaching

Features: Bible Stories; Paraphrase Scripture

Statut: Approved

Les scripts sont des directives de base pour la traduction et l'enregistrement dans d'autres langues. Ils doivent être adaptés si nécessaire afin de les rendre compréhensibles et pertinents pour chaque culture et langue différente. Certains termes et concepts utilisés peuvent nécessiter plus d'explications ou même être remplacés ou complètement omis.

Corps du texte

Wavulana walipokomaa, Yakobo alipenda kukaa nyumbani, ila Esau alipenda kuwinda. Rebeka alimpenda Yakobo, ila Isaka alimpenda Esau.

Siku moja Esau alipotoka kuwinda, alikuwa na njaa sana, Esau alisema kwa Yakobo, "tafadhali naomba chakula ulichopika." Yakobo akajibu akamwambia, "kwanza nipe mimi haki yako ya mtoto mkubwa". Ndipo Esau akampa haki yake ya mtoto mkubwa."Hivyo Esau alimpa Yakobo chakula.

Isaka alitaka kumpa Esau baraka zake. Kabla ya kufanya hivyo, Rebeka na Yakobo wamdanganya kwa Yakobo kujifanya kuwa Esau. Isaka alikuwa mzee na hakuweza kuona. Yakobo alivaa nguo za Esau na ngozi za mbuzi mikononi na shingoni.

Yakobo alikuja kwa Isaka akasema, "mimi ni Esau. Nimekuja ili kwamba unibariki." Isaka aliposikia harufu na kuhisi nywele za mbuzi na kunusa nguo, alidhani ni Esau na akambariki.

Esau alimchukia Yakobo kwa kuwa Yakobo alikuwa ameiba haki yake ya kuwa mkubwa na baraka zake. Hivyo alipanga moyoni mwake kumuua baada ya baba yao kufariki.

Rebeka alisikia mpango wa Esau. Yeye na Isaka walimtorosha Yakobo aende mbali akaishi na ndugu zake.

Yakobo akaishi na ndugu zake Rebeka kwa miaka mingi. Katika kipindi hicho alioa na akazaa watoto wa kiume kumi na wawili na wa kike mmoja. Mungu akamtajirisha sana.

Baada ya kuishi nje ya Kanaani kwa miaka ishirini, Yakobo alirudi nyumbani na familia yake, watumwa wake, na mifugo yake yote.

Yakobo aliogopa sana kwa sababu alidhani Esau bado alitaka kumuua. Akatuma makundi ya mifugo kwa Esau kama zawadi. Watumwa waliopeleka mifugo wakasema kwa Esau, "Mtumwa wako Yakobo anakupa wewe mifugo hii. Anakuja hivi karibuni."

Ila Esau alikuwa amemsamehe Yakobo, na walifurahi kuonana tena kila mmoja.Yakobo akaishi Kanaani kwa amani. Isaka akafa huko, Esau naYakobo wakamzika. Ahadi za agano, Mungu alizomhaidia Ibrahimu kumpata zikatoka kwa Isaka kwenda kwa Yakobo.

Informations reliées

Mots de Vie - GRN présente des messages sonores évangéliques dans des milliers de langues à propos du salut et de la vie chrétienne.

Téléchargements gratuits - Ici vous allez trouver le texte pour les principaux messages GRN en plusieurs langues, plus des images et autres documents prêts à télécharger

La collection d'Enregistrements de GRN - Matériel d'évangélisation et d'enseignement biblique de base adapté aux besoins et à la culture du peuple, dans une variété de styles et de formats.

Choosing the audio or video format to download - What audio and video file formats are available from GRN, and which one is best to use?

Copyright and Licensing - GRN shares its audio, video and written scripts under Creative Commons