unfoldingWord 33 - Simulizi ya Mkulima

unfoldingWord 33 - Simulizi ya Mkulima

طرح کلی: Matthew 13:1-23; Mark 4:1-20; Luke 8:4-15  

شماره کتاب: 1233

زبان: Swahili

مخاطبان: General

هدف: Evangelism; Teaching

Features: Bible Stories; Paraphrase Scripture

وضعیت: Approved

اسکریپت ها( سندها)، دستورالعمل های اساسی برای ترجمه و ضبط به زبان های دیگر هستند. آنها باید در صورت لزوم تطبیق داده شوند تا برای هر فرهنگ و زبان مختلف قابل درک و مرتبط باشند. برخی از اصطلاحات و مفاهیم مورد استفاده ممکن است نیاز به توضیح بیشتری داشته باشند، یا جایگزین، یا به طور کامل حذف شوند.

متن کتاب

Siku moja, Yesu alikuwa akifundisha makutano wengi katika pwani ya ziwa. Na watu wengi walimfuata wapate kumsikiliza. Yesu aliingia ndani ya mashua mahali pa juu apate nafasi nzuri ya kuzungumza nao. Yesu alikaa kwenye mashua akawafundisha watu.

Yesu aliwasimulia hadithi," Mpanzi alikwenda kupanda mbegu shambani, alipokuwa akimwaga mbegu kwa kutumia mikono yake. Mbegu zingine ziliangukia kwenye njia, ndege wakazila zote."

Mbegu zingine zilianguka kwenye ardhi yenye mawe, nazo zikachipuka haraka. Lakini jua lilipowaka zote zika ungua, kwa sababu mizizi haikuweza kustawi vizuri katika ule udongo mchache, hivyo miche ile ikafa.

Mbegu zingine zilianguka kwenye miiba, nazo zikamea lakini zikasongwa na miiba. Kwa hiyo mbengu hizo hazikuweza kuzaa matunda.

Mbegu zingine ziliangukia penye udongo mzuri. Mbengu hizo ziliweza kustawi na kuzaa 30, 60 na 100 zaidi kadri ya wingi wake katika kupandwa. Aliye na masikio, na asikie.

Hadithi iliwachanganya watu. Naye Yesu akawafafanulia akasema, "mbegu ni neno la Mungu. Mbegu zilizoanguka kwenye njia, ni yule mtu anaye lisikia neno la Mungu, lakini halielewi. Shetani huja na kulichukua neno kwa mtu huyo."

“Ile ardhi ya udongo wa mawe, ni yule mtu anayelisikia neno na kulipokea kwa furaha. Lakini yajapotokea mateso na majaribu, hushindwa kustahimili na huanguka dhambini.”

“Ardhi yenye miiba, ni yule mtu anayelisikia neno la Mungu, lakini kwa kadri siku zinavyoendelea, utajiri, anasa za maisha humtenga na upendo wa Mungu. Matokeo yake, lile neno la Mungu alilolisikia halizai matunda.”

“Ule udongo mzuri ni yule mtu anaye lisikia neno la Mungu na kuliaminii hivyo huzaa matunda.”

اطلاعات مربوطه

کلام زندگی - جی آر اِن پیام‌های صوتی انجیل شامل پیام‌هایی بر طبق کتاب مقدس درباره رستگاری و زندگی بصورت یک مسیحی را به هزارن زبان ارائه می‌دهد.

دریافت رایگان - در این قسمت شما می‌توانید تمام پیام‌های اصلی جی آر اِن به چندین زبان، به علاوه تصاویر و دیگر مطالب مرتبط که برای دریافت موجود است را مشاهده کنید.

The GRN Audio Library - Evangelistic and basic Bible teaching material appropriate to the people's need and culture in a variety of styles and formats.

Choosing the audio or video format to download - What audio and video file formats are available from GRN, and which one is best to use?

Copyright and Licensing - GRN shares its audio, video and written scripts under Creative Commons