unfoldingWord 33 - Simulizi ya Mkulima

unfoldingWord 33 - Simulizi ya Mkulima

Zusammenfassung: Matthew 13:1-23; Mark 4:1-20; Luke 8:4-15  

Skript Nummer: 1233

Sprache: Swahili

Zuschauer: General

Genre: Bible Stories & Teac

Zweck: Evangelism; Teaching

Bibelzitat: Paraphrase

Status: Approved

Skripte dienen als grundlegende Richtlinie für die Übersetzung und Aufnahme in anderen Sprachen. Sie sollten, soweit erforderlich, angepasst werden, um sie für die jeweilige Kultur und Sprache verständlich und relevant zu machen. Einige der verwendeten Begriffe und Konzepte müssen unter Umständen ausführlicher erklärt oder sogar ersetzt oder ganz entfernt werden.

Skript Text

Siku moja, Yesu alikuwa akifundisha makutano wengi katika pwani ya ziwa. Na watu wengi walimfuata wapate kumsikiliza. Yesu aliingia ndani ya mashua mahali pa juu apate nafasi nzuri ya kuzungumza nao. Yesu alikaa kwenye mashua akawafundisha watu.

Yesu aliwasimulia hadithi," Mpanzi alikwenda kupanda mbegu shambani, alipokuwa akimwaga mbegu kwa kutumia mikono yake. Mbegu zingine ziliangukia kwenye njia, ndege wakazila zote."

Mbegu zingine zilianguka kwenye ardhi yenye mawe, nazo zikachipuka haraka. Lakini jua lilipowaka zote zika ungua, kwa sababu mizizi haikuweza kustawi vizuri katika ule udongo mchache, hivyo miche ile ikafa.

Mbegu zingine zilianguka kwenye miiba, nazo zikamea lakini zikasongwa na miiba. Kwa hiyo mbengu hizo hazikuweza kuzaa matunda.

Mbegu zingine ziliangukia penye udongo mzuri. Mbengu hizo ziliweza kustawi na kuzaa 30, 60 na 100 zaidi kadri ya wingi wake katika kupandwa. Aliye na masikio, na asikie.

Hadithi iliwachanganya watu. Naye Yesu akawafafanulia akasema, "mbegu ni neno la Mungu. Mbegu zilizoanguka kwenye njia, ni yule mtu anaye lisikia neno la Mungu, lakini halielewi. Shetani huja na kulichukua neno kwa mtu huyo."

“Ile ardhi ya udongo wa mawe, ni yule mtu anayelisikia neno na kulipokea kwa furaha. Lakini yajapotokea mateso na majaribu, hushindwa kustahimili na huanguka dhambini.”

“Ardhi yenye miiba, ni yule mtu anayelisikia neno la Mungu, lakini kwa kadri siku zinavyoendelea, utajiri, anasa za maisha humtenga na upendo wa Mungu. Matokeo yake, lile neno la Mungu alilolisikia halizai matunda.”

“Ule udongo mzuri ni yule mtu anaye lisikia neno la Mungu na kuliaminii hivyo huzaa matunda.”

Verwandte Informationen

Worte des Lebens - GRN hat Audio-Gospel-Botschaften in tausenden von Sprachen, beinhaltet bibelbasierte Botschaften über die Erettung und das christliche Leben.

Freie Downloads - Hier findet man alle GRN Botschaften, Schriften in vielen Sprachen, plus Bilder und andere verwandte Materialien, verfügbar zum Download.

The GRN Audio Library - Evangelistic and basic Bible teaching material appropriate to the people's need and culture in a variety of styles and formats.

Copyright and Licensing - GRN shares it's audio, video and written scripts under Creative Commons

Choosing the right audio or video format - What audio and video file formats are available from GRN, and which one is best to use?