unfoldingWord 36 - Kubadilika Sura
Omrids: Matthew 17:1-9; Mark 9:2-8; Luke 9:28-36
Script nummer: 1236
Sprog: Swahili
Publikum: General
Genre: Bible Stories & Teac
Formål: Evangelism; Teaching
Bibel citat: Paraphrase
Status: Approved
Scripts er grundlæggende retningslinjer for oversættelse og optagelse til andre sprog. De bør tilpasses efter behov for at gøre dem forståelige og relevante for hver kultur og sprog. Nogle anvendte termer og begreber kan have behov for mere forklaring eller endda blive erstattet eller helt udeladt.
Script tekst
Siku moja, Yesu aliwachukua wanafunzi wake watatu Yakobo, Petro na Yohana. ( Mwanafunzi aitwae Yohana sio yule aliyembatiza Yesu.) Walipanda juu ya mlima mrefu kuomba pekeyao.
Yesu akiwa anaomba uso wake ulibadilika na kung'aa kama jua na mavazi yake yakawa meupe kama mwanga, yalikua meupe sana zaidi awezavyo mtu duniani kuyafanya yang'ae.
Ndipo Musa na nabii Eliya wakawatokea. Watu hawa waliishi duniani miaka mingi kabla. Waliongea na Yesu juu ya kifo chake ambacho kitatokea Yerusalemu siku chache baadae.
Wakati Musa na Eliya wanaongea na Yesu, Petro akamwambia Yesu, "Ni vizuri sisi kuwa hapa, hivyo naomba tutengeneze nyumba tatu moja ya kwako, nyingine ya Eliya na nyingine ya Musa". Lakini Petro hakujua alinenalo.
Wakati Petro anaongea wingu jeupe lilishuka na kuwazunguka na sauti ikatoka katika lile wingu ikisema " Huyu ni Mwanagu nimpendaye. Ninayependezwa naye msikilizeni yeye".Wale wanafunzi watatu waliogopa na kuanguka chini.
Ndipo Yesu akawagusa na kuwaambia "Msiogope inukeni". walipotazama pembeni ni Yesu pekee ndiye aliyebaki pale.
Yesu pamoja na wanafunzi wake watatu wakashuka kutoka mlimani. Yesu akawaambia "Msimwambie mtu yeyote yale yaliyotokea, siku chache baadae nitakufa kisha nitakua hai tena. Baada ya hapo mtawaambia watu."