unfoldingWord 40 - Yesu Anasulubiwa

unfoldingWord 40 - Yesu Anasulubiwa

إستعراض: Matthew 27:27-61; Mark 15:16-47; Luke 23:26-56; John 19:17-42

رقم النص: 1240

لغة: Swahili

الجماهير: General

فصيل: Bible Stories & Teac

الغرض: Evangelism; Teaching

نص من الإنجيل: Paraphrase

حالة: Approved

هذا النص هو دليل أساسى للترجمة والتسجيلات فى لغات مختلفة. و هو يجب ان يعدل ليتوائم مع اللغات و الثقافات المختلفة لكى ما تتناسب مع المنطقة التى يستعمل بها. قد تحتاج بعض المصطلحات والأفكار المستخدمة إلى شرح كامل أو قد يتم حذفها فى ثقافات مختلفة.

النص

Baada ya askari kumdhihaki Yesu, walimpeleka kumsulibisha. walimlazimisha aubebe msalaba ambao ungetumika kumuua.

Askari walimpeleka Yesu eneo liitwalo "fuvu la kichwa" wakaipigilia miguu na mikono yake msalabani. Lakini Yesu akasema, "Baba wasamehe, kwa sababu hawajui wanalotenda." Pilato akaagiza waandike kwamba, "Mfalme wa Wayahudi" ikiwa ni ishara; na waweke msalabani, juu ya kichwa cha Yesu.

Askari walipigia kura mavazi yake. Na kitendo hiki kinatimiza unabii usemao kwamba, " wakagawana nguo zangu na kucheza kamali."

Yesu alisulibiwa katikati ya wanyang'anyi wawili; mmojawapo alimdhihaki Yesu, lakini mwingine alisema, "Humwogopi Mungu!? Sisi tunahatia, lakini huyu hana hatia" Ndipo yeye akamwabia Yesu "Tafadhali unikumbuke katika ufalme wako" Yesu akamjibu, leo, utakuwa nami Paradiso."

Viongozi wa wayahudi na baadhi ya wengine katika umati walimdhihaki Yesu. Wakisema, "kama wewe ni Mwana wa Mungu, shuka msalabani, jiokoe mwenyewe, ndipo tutakuamini."

Ndipo katika eneo hilo kukawa giza nene, ingawa ilikuwa mchana. Mchana huo kukawa giza kwa saa tatu.

Yesu akalia, "Baba imekwisha naweka mikononi mwako roho yangu." Ndipo akainama akajitoa mwenyewe roho yake. Alipokufa lilitokea tetemeko la ardhi na pazia la hekaluni lililowatenga watu na Mungu lilipasuka vipande viwili, tokea juu hadi chini.

Kifo chake Yesu kinafungua njia ili watu waje kwa Mungu. Askari aliyemlinda Yesu alipoona mambo haya yote yanatokea alisema, "Hakika mtu huyu hakuwa na hatia, alikuwa Mwana wa Mungu."

Na ndipo Yusufu na Nikodemo viongozi wa Wayahudi walioamini Yesu kuwa ni Masihi wakauomba mwili wa Yesu na kuufunga kwenye sanda na kupeleka kwenye kaburi lililochongwa tayari mwambani na wakasogeza jiwe kubwa kulifunga kaburi.

معلومات ذات صلة

كلمات الحياة - GRN لديها رسائل صوتية تبشيرية فى الاف الغات تحتوى على رسائل الكتاب المقدس الرئيسية عن الفداء والحياة المسيحية.

تحميلات مجانية - هنا يمكنك أن تجد نصوص رسائل GRN الرئيسية فى عدة لغات، بالإضافة إلى صور ومواد أخرى مرتبطة، متوفرة للتحميل.

مكتبة GRN الصوتية - المواد التبشيرية و التعليمية للكتاب المقدس الملائمة لإحتياجات الناس و ثقافاتهم متاحة فى أشكال و أنماط عديدة.

Copyright and Licensing - GRN shares it's audio, video and written scripts under Creative Commons

Choosing the right audio or video format - What audio and video file formats are available from GRN, and which one is best to use?