unfoldingWord 26 - Yesu Anaanza Huduma yake

unfoldingWord 26 - Yesu Anaanza Huduma yake

إستعراض: Matthew 4:12-25; Mark 1-3; Luke 4

رقم النص: 1226

لغة: Swahili

الجماهير: General

فصيل: Bible Stories & Teac

الغرض: Evangelism; Teaching

نص من الإنجيل: Paraphrase

حالة: Approved

هذا النص هو دليل أساسى للترجمة والتسجيلات فى لغات مختلفة. و هو يجب ان يعدل ليتوائم مع اللغات و الثقافات المختلفة لكى ما تتناسب مع المنطقة التى يستعمل بها. قد تحتاج بعض المصطلحات والأفكار المستخدمة إلى شرح كامل أو قد يتم حذفها فى ثقافات مختلفة.

النص

Baada ya kushinda majaribu ya Ibilisi Yesu alirudi kwa nguvu za Roho mtakatifu katika mkoa wa Galilaya. Yesu alienda sehemu moja baada ya nyigine akifundisha. Kila mmoja alisema vyema juu yake.

Yesu akaenda mji wa Nazareti alikokuwa akiishi wakati wa utoto wake. Siku ya sabato, alienda sehemu ya kuabudia. wakamkabidhi chuo cha nabii isaya ili aweze kusoma. Yesu akakifungua chuo na kusoma sehemu yake mbele za watu.

Yesu kasema "Bwana amenipa Roho wake ili kwamba nitangaze habari njema kwa maskini, uhuru kwa wafungwa, vipofu kuona, kutolewa waliodhurumiwa. huu ni mwaka wa Bwana uliokubalika.

Tena Yesu akaa chini "Kila mmoja akamsogelea na kumtazama. walijua aya aliyoisoma inamhusu masia. Yesu akasema "Maneno niliyosoma mbele yenu yanatokea sasa. watu wote wakashangaa. huyu si mwana wa Yusufu"? Walisema.

Tena Yesu akasema "Ni kweli kwamba hakuna nabii anayekubalika katika mji wa kwao. Wakati wa nabii Eliya, kulikuwa na wajane katika Israeli. lakini mvua iliposimama bila kunyesha kwa miaka mitatu na nusu, Mungu hakumtuma Eliya kumsaidia mwanamke mjane kutoka Israel, badala yake alikuwa ni mjane kutoka taifa tofauti"

Yesu akaendelea kusema "Kipindi cha nabii Elisha kulikuwa na watu wengi katika Israeli wenye magonjwa ya Ngozi. lakini Elisha hakumponya hata mmoja wao. lakini aliponya ugonjwa wa ngozi wa Naamani pekee aliyekuwa kamanda wa maadui wa Israel. watu waliokuwa wanamsikiliza Yesu walikuwa ni wayahudi. Kwa hiyo walipomsikia anasema hayo wakawa na hasira juu yake.

Watu wa Nazareti wakamvuta Yesu mbali na mahali pa kuabudia na kumtupa nje ili wamwue. Lakini Yesu akaondoka Mbele yao na akauacha mji wa Nazaleti.

Tena Yesu alienda mpaka mkoa wa Galilaya na mkutano mkubwa wakaja kwake. wakawealeta watu wengi waliokuwa wagonjwa, au walemavu, kama wasioona, kutembea, kusikia au kuongea, na Yesu akawaponya.

Watu wengi waliokuwa na mapepo ndani yao waliletwa kwa Yesu. Kwa amri ya Yesu aliwaamuru wawatoke watu hao, na waliendelea kupiga kelele "Wewe ni mwana wa Mungu!" Umati wa watu walishangaa na walimwabudu Mungu.

Tena Yesu akachagua watu kumi na wawili ambao aliwaita mitume. Mitume walizunguka na Yesu tena walijifunza kutoka kwake.

معلومات ذات صلة

كلمات الحياة - GRN لديها رسائل صوتية تبشيرية فى الاف الغات تحتوى على رسائل الكتاب المقدس الرئيسية عن الفداء والحياة المسيحية.

تحميلات مجانية - هنا يمكنك أن تجد نصوص رسائل GRN الرئيسية فى عدة لغات، بالإضافة إلى صور ومواد أخرى مرتبطة، متوفرة للتحميل.

مكتبة GRN الصوتية - المواد التبشيرية و التعليمية للكتاب المقدس الملائمة لإحتياجات الناس و ثقافاتهم متاحة فى أشكال و أنماط عديدة.

Copyright and Licensing - GRN shares it's audio, video and written scripts under Creative Commons

Choosing the right audio or video format - What audio and video file formats are available from GRN, and which one is best to use?