ቋንቋ ይምረጡ

mic

unfoldingWord 23 - Kuzaliwa kwa Yesu

unfoldingWord 23 - Kuzaliwa kwa Yesu

ዝርዝር: Matthew 1-2; Luke 2

የስክሪፕት ቁጥር: 1223

ቋንቋ: Swahili

ታዳሚዎች: General

ዓላማ: Evangelism; Teaching

Features: Bible Stories; Paraphrase Scripture

ሁኔታ: Approved

ስክሪፕቶች ወደ ሌሎች ቋንቋዎች ለመተርጎም እና ለመቅዳት መሰረታዊ መመሪያዎች ናቸው። ለእያንዳንዱ የተለየ ባህል እና ቋንቋ እንዲረዱ እና እንዲስማሙ ለማድረግ እንደ አስፈላጊነቱ ማስተካከል አለባቸው። አንዳንድ ጥቅም ላይ የዋሉ ቃላቶች እና ጽንሰ-ሐሳቦች የበለጠ ማብራሪያ ሊፈልጉ ወይም ሊተኩ ወይም ሙሉ ለሙሉ ሊተዉ ይችላሉ.

የስክሪፕት ጽሑፍ

Mariamu alikuwa amechumbiwa na mtu mwadilifu aitwaye Yusufu. Yusufu kwasababu ya uhaki hakutaka Mariamu apate aibu kwaajili ya ujauzito ambao haukumhusu hivyo akaanza kutafuta njia akwepe kwa siri. Malaika akamtokea Yusufu katika ndoto.

Ndipo Malaika akamtahadharisha Yusufu kwamba asimwache Mariamu kwasababu mimba hiyo ni kwa uweza wa Roho Mtakatifu hivyo asiwe na wasiwasi. Mtoto atakayezaliwa ni wa kiume ataitwa jina lake Yesu (yaani Yehova huokoa), kwa kuwa atawaokoa watu waondoke dhambini.

Yusufu aliamua kumchukua Mariamu kuwa mkewe; lakini, hawakukaribiana mpaka pale Mariamu atakapomzaa mwana.

Wakati Mariamu alipokaribia kuzaa, ni kipindi kile utawala wa Rumi ulielekeza kila mtu ahesabiwe katika jamii anayotokea. Hapa inabidi sasa Yusufu na Mariamu wasafiri safari ndefu waelekee Bethlehemu tokea Nazareti kwa sababu ndiyo mji wao kwa asali yaani mji wa Daudi.

Baada ya kufika Bethlehemu hapakuwa na mahali ya kujihifadhi. Nafasi waliyopata ni pale mifugo ilihifadhiwa, ndipo mtoto alipozaliwa na mama yake alimlaza kwenye lishio la ng'ombe kwa kuwa hakuna kitanda; jina lake aliitwa Yesu.

Usiku ule ule walikuwepo wachungaji wa maeneo jirani wakilinda mifugo yao. Ghafla waliona malaika akin'gaa mbele yao wakatekewa; Malaika akasema, "msiwe na wasiwasi ninazo habari nzuri. Kristo Bwana amezaliwa Bethlehem!"

Akaongeza; "nendeni kwa mtoto, mtamuona amefungwa nguo akiwa amelazwa kwenye lishio la mifugo." Mawinguni walionekana Malaika, wakitukuza na kuimba Utukufu uko mbinguni kwa Mungu na amani duniani kwa wapendwa."

Wachungaji walifika mahali pale alipokuwa Yesu kama maelekezo ya malaika yalivyokuwa wakiwa wamejawa furaha. Baada ya hapo wakarudi ilipokuwa mifugo yao; wakimtukuza Mungu kwa yale waliyosikia na kuyaona.

Badaye wenye ujuzi tokea mashariki ya mbali wakiongozwa na nyota walifika Bethlehemu na hapo wakatambua ile nyota ilimaanisha Mfalme wa Wayahudi. Hivyo wakasafiri safari ndefu na wakaipata nyumba alimokuwa Yesu akiwa pamoja na wazazi wake.

Na wataalamu hawa walipomuona Yesu na mama yake, wakainama na kumwabudu. Ndipo walimpa Yesu zawadi za gharama kubwa. Wakarudi kwao mashariki.

ተዛማጅ መረጃ

የሕይወት ቃላት - ስለ ድነት እና ስለ ክርስቲያናዊ ኑሮ መጽሐፍ ቅዱሳዊ መልእክት የያዙ በሺዎች በሚቆጠሩ ቋንቋዎች የኦዲዮ የወንጌል መልእክቶች።

Choosing the audio or video format to download - What audio and video file formats are available from GRN, and which one is best to use?

Copyright and Licensing - GRN shares its audio, video and written scripts under Creative Commons