unfoldingWord 08 - Mungu anamuokoa Yusufu na Familia yake

unfoldingWord 08 - Mungu anamuokoa Yusufu na Familia yake

概要: Genesis 37-50

文本編號: 1208

語言: Swahili

聽眾: General

類型/流派: Bible Stories & Teac

目的: Evangelism; Teaching

聖經摘錄: Paraphrase

狀態: Approved

腳本是翻譯和錄製成其他語言的基本指南,它們需要根據實際需要而進行調整以適合不同的文化和語言。某些使用術語和概念可能需要有更多的解釋,甚至要完全更換或省略。

文本文字

Baada ya miaka mingi kupita, Yakobo alipokuwa mzee sana, alimuagiza kijana wake aitwaye Yusufu, kuwatembelea kaka zake waliokuwa wakichunga mifugo ya baba yao.

Kwakuwa Yusufu alikuwa anapendwa sana na baba yake, na kwamba siku moja aliwahi kuota ndoto na akawasimulia kaka zake kwamba yeye atakuwa mtawala wao hapo baadae, kaka zake walimchukia. Hivyo, Yusufu alipofika kwa kaka zake, walimteka na wakamuuza kwa watu wenye kufanya biashara ya watumwa.

Basi kaka zake na Yusufu walipotaka kurudi nyumbani, walikubaliana kwa hila kuzichanachana nguo za mdogo wao, Yusufu, kisha wakaziloweka kwenye damu ya mbuzi. Walipofika wakamuonyesha baba yao nguo hizo zenye damu, ili kumuaminisha kuwa kuna mnyama mkali wa porini amemrarua na kumuua Yusufu. Basi Yakobo aliposikia habari hiyo alimhuzunikia sana Yusufu.

Na ndipo wale wafanyabiashara ya watumwa, wakamsafirisha Yusufu hadi nchi ya mbali sana iitwayo Misri. Nchi ya Misri ilikuwa maarufu na hodari kwa mambo mengi katika nchi za mwambao wa mto Naili.Yusufu akauzwa kama mtumwa katika nyumba ya afisa mmoja wa serikali ya misri aliyekuwa tajiri sana. Naye Yusufu akatumika kwa uaminifu sana katika nyumba ya bwana wake, na Mungu akambariki sana Yusufu.

Mke wa tajiri yake alimtaka Yusufu ili azini naye, lakini Yusufu alikataa ili asimkosee Mungu. Kisha baada ya hayo, yule mwanamke, mke wa tajiri, alikasirika sana, hata akamtuhumu Yusufu kwa kumsingizia ili Yusufu akamatwe na kufungwa gerezani. Hata hivyo, Yusufu aliendelea kuwa mwaminifu mbele za Mungu hata alipokuwa amefungwa gerezani, na Mwenyezi Mungu akambariki. Hata ilipotimia miaka miwili baadae, Yusufu alikuwa bado yumo gerezani, japo hakuwa na kosa lolote.

Yusufu alikuwa bado yumo gerezani hadi miaka miwili baadae, japo hakuwa na kosa lolote. Siku moja nyakati za usiku, Farao, mfalme wa Wamisri, aliota ndoto mbili zikamsumbua sana mawazoni mwake usiku ule. Miongoni mwa washauri wake wote na wenye hekima, hapakuwa na mtu yeyote mwenye uwezo wa kutoa maana ya ndoto hizo.

Kwakuwa Mwenyezi Mungu alikuwa amemjalia Yusufu uwezo wa kipekee wa kutafsiri ndoto, Farao, mfalme wa Misri, aliamuru Yusufu aletwe kwake kutoka gerezani ili atoe maana halisi ya ndoto hiyo. Kwa kuongozwa na Mwenyezi Mungu, Yusufu akasimama mbele ya Farao kutafsiri ndoto zile akisema; "Wakati unakuja ambapo Mwenyezi Mungu ataruhusu pawepo na kipindi cha miaka saba ya mavuno mengi, itakayofuatiwa na miaka mingine saba ya ukame na njaa."

Yusufu akateuliwa kuwa mtu wa pili kwa mamlaka katika nchi yote ya Misri, kwa kuwa Farao, mfalme wa Misri, alifurahishwa na kuvutiwa sana na Yusufu.

Basi Yusufu akawatangazia watu wote wa Misri kujiwekea akiba ya chakula cha kutosha watakapovuna katika kipindi cha miaka saba ya mavuno mengi. Ilipowadia ile miaka saba mingine ya njaa, ndipo Yusufu akatumia sehemu ya akiba ya chakula kuwauzia watu ili kiwafae katika kile kipindi cha miaka saba ya njaa.

Hali ya ukame na njaa, ikazidi kuwaathiri watu wengi wa Misri yenyewe na hata nchi ya Kanaani alikoishi Yakobo baba yake na Yusufu pamoja na familia yake.

Hivyo, Yakobo akawaagiza vijana wake wakubwa kwenda Misri kununua chakula. Walipokuwa wakingojea zamu yao ya kununua chakula, Yusufu aliwaona kaka zake na akawatambua, ila wao walikuwa wamemsahau Yusufu.

Yusufu aliamua kufanya mahojiano nao akitaka kujua iwapo walikuwa wamebadilika kitabia, kisha akawaambia hivi: "msihofu ndugu zangu, mimi mnaeniona ndiye mdogo wenu Yusufu. Najua fika hamkuwa na nia njema na mimi mliponiuza kama mtumwa, lakini Mwenyezi Mungu aliitumia nia yenu mbaya kwa ajili ya kusudi jema." Nawakaribisha muwe huru kuja kuishi hapa Misri ili niwatunze ninyi na familia zenu.

Ndipo kaka zake Yusufu waliporudi nyumbani kwao, Kanaani, walimpasha habari baba yao kuwa Yusufu , mwanae mpendwa bado yuko hai; Yakobo baba yake na Yusufu alijawa na furaha isiyo kifani.

Katika kipindi hicho, Yakobo alikuwa amekwisha kuwa mzee sana. Lakini akalazimika kuhamia katika nchi ya Misri yeye na familia yake yote. Hivyo, Yakobo akaishi pamoja na familia yake katika nchi ya Misri na kabla hajafariki akawapa mibaraka wanae wote, kila mmoja na mbaraka wake.

Kama ambavyo Mwenyezi Mungu alikuwa amemuahidi Ibrahimu, maagano yote yakarithishwa kwa vizazi vyake yaani, Isaka, kisha Yakobo, na hatimaye watoto kumi na wawili wa Yakobo pamoja na uzao wao, ambao ndio wanaounda kabila kumi na mbili za Israeli.

相關信息

生命之道 - 環球錄音網擁有用數以千計的語言去錄製的福音信息,內容包括一些有關救恩和基督徒樣式的聖經信息。

免費下載 - 免費下載傳教及發展教會組織所用的錄音、圖片、文本和其他相關資料。內容包括聖經故事與傳教課程,并已被翻譯成上千種語言。

環球錄音網音頻圖書館 - 提供mp3,CD和磁帶形式的傳播福音和基本的宣教材料,適宜人們的需要和文化。錄音材料的形式多樣,包括簡單的聖經故事,福音信息,經文朗誦和歌曲。

Copyright and Licensing - GRN shares it's audio, video and written scripts under Creative Commons

Choosing the right audio or video format - What audio and video file formats are available from GRN, and which one is best to use?