unfoldingWord 20 - Kuchukuliwa Mateka na Kurudi

unfoldingWord 20 - Kuchukuliwa Mateka na Kurudi

概要: 2 Kings 17; 24-25; 2 Chronicles 36; Ezra 1-10; Nehemiah 1-13

文本編號: 1220

語言: Swahili

聽眾: General

類型/流派: Bible Stories & Teac

目的: Evangelism; Teaching

聖經摘錄: Paraphrase

狀態: Approved

腳本是翻譯和錄製成其他語言的基本指南,它們需要根據實際需要而進行調整以適合不同的文化和語言。某些使用術語和概念可能需要有更多的解釋,甚至要完全更換或省略。

文本文字

Ufalme wa Israel na ufalme wa Yuda walitenda dhambi mbele za Mungu. walivunja agano waliloweka na Mungu Sinai. Mungu aliwatuma Manabii wake kuwaonya ili watubu na kumuabudu yeye lakini walikataa.

Ndipo Mungu aliadhibu falme zote kwa kuruhusu maadui zao kuwapiga. Ufame wa Ashuru ulikua ni ufalme wenye nguvu, taifa korofi likaharibu ufalme wa Israel. katika ufalme wa Israel Waashuru waliwaua watu wengi sana na kuwanyang'anya kila kitu cha thamani kisha kuchoma moto sehemu kubwa ya ardhi yao.

Waashuru waliwakusanya viongozi wote, matajiri na watu wenye ujuzi kisha kuwapeleka Ashuru. Masikini ambao hawakuuawa ndio waliobaki Israeli.

Waashuru waliwaleta wageni ili waishi katika nchi ya Israel. Wageni hao walijenga miji iliyoharibiwa na kuoa waisrael waliobaki. Kizazi cha wana wa Israel waliooana wa wageni kiliitwa Wasamaria.

Watu wa ufame wa Yuda waliona jinsi ambavyo Mungu alivyowaadhibu watu wa Israel kwa kutokumtii na kumwamini Mungu. lakini waliendelea kuiabudu miungu na akiwemo Mungu wa wakaanani. Mungu alituma manabii kuwaonya lakini hawakusikia.

Takribani miaka 100 baada ya Waashuru kuharibu ufalme wa Israeli Mungu alimtuma Nebukadneza mfalme wa Babiloni kuvamia taifa la Yuda. Babiloni lilikua taifa ;enye nguvu. Mfalme wa Yuda akakubali kuwa mtumishi wa Nebukadneza na kulipwa pesa nyingi kila mwaka.

Miaka michace baadae Mfalme wa Yuda akasi juu ya Babiloni. Ndipo wababiloni wakarudi na kuuteka ufalme wa Yuda. Waliuvamia mji wa Yerusalem wakaharibu hekalu na kuchukua vitu vyote vya thamani vilivyokuwemo katika mji.

Kwa sababu ya uasi Askari wa Mfalme Nebukadneza waliwaua watoto wote wa mfalme wa Yuda mbele ya macho yake kisha wakamharibu macho yake. Baada ya hayo wakamchukua mfalme na kumpeleka gerezani Babiloni ili afie huko.

Mfalme Nebukadneza pamoja na jeshi lake waliwapeleka watu wengi wa Yuda Babiloni, wakawaacha masikini ili wafanye kazi katika mashamba. Kipindi ambacho watu wa Mungu walilazimishwa kuondoka nchi ya ahadi kiliitwa kipindi cha Mateka.

Japokua Mungu aliwaadhibu watu wake kwa dhambi zao kwa kuwafanya mateka lakini hakuwasahau watu wake na ahadi aliyowaahidi. Mungu aliendelea kuwaangalia na kuzungumza nao kupitia manabii. Aliwaahidi kua baada ya miaka sabini atawarudisha kwenye nchi ya ahadi.

Miaka sabini baadae mfalme wa Uajemi alimshinda Babiloni hivyo ufalme wa Uajemi ukachukua nafasi ya ufalme wa Babiloni. Waisrael wakaanza kuitwa wayahudi na wengi wao waliishi Babiloni. Wachache waliokua wazee waliikumbuka nchi ya Yuda.

Ufalme wa Uajemi ulikua na nguvu lakini ulikua na huruma kwa watu waliowateka. Baada ya Koreshi kua Mfalme wa Uajemi alitoa amri kuwa Myahudi yeyote anaetaka kurudi Yuda anaweza kuondoka uajemi na kurudi Yuda. Aliwapa pesa kwa ajili ya kujenga upya hekalu. Baada ya miaka sabini ya kuwa mateka wayahudi wachache walirudi Yuda katika mji wa Yerusalemu.

Waliporudi Yerusalemu walijenga upya hekalu pamoja na ukuta wa mji. Japokua walikua wakitawaliwa na watu wengine lakini walipata nafasi ya kuishi kwenye nchi ya ahadi na kumwabudu Mungu hekaluni.

相關信息

生命之道 - 環球錄音網擁有用數以千計的語言去錄製的福音信息,內容包括一些有關救恩和基督徒樣式的聖經信息。

免費下載 - 免費下載傳教及發展教會組織所用的錄音、圖片、文本和其他相關資料。內容包括聖經故事與傳教課程,并已被翻譯成上千種語言。

環球錄音網音頻圖書館 - 提供mp3,CD和磁帶形式的傳播福音和基本的宣教材料,適宜人們的需要和文化。錄音材料的形式多樣,包括簡單的聖經故事,福音信息,經文朗誦和歌曲。

Copyright and Licensing - GRN shares it's audio, video and written scripts under Creative Commons

Choosing the right audio or video format - What audio and video file formats are available from GRN, and which one is best to use?