unfoldingWord 41 - Mungu Anamfufua Yesu kutoka katika Wafu

unfoldingWord 41 - Mungu Anamfufua Yesu kutoka katika Wafu

План-конспект: Matthew 27:62-28:15; Mark 16:1-11; Luke 24:1-12; John 20:1-18

Номер текста: 1241

Язык: Swahili

Aудитория: General

Жанр: Bible Stories & Teac

Цель: Evangelism; Teaching

Библейская цитата: Paraphrase

статус: Approved

Сценарии - это основные инструкции по переводу и записи на другие языки. Их следует при необходимости адаптировать, чтобы сделать понятными и актуальными для каждой культуры и языка. Некоторые используемые термины и концепции могут нуждаться в дополнительном пояснении или даже полностью замещаться или опускаться.

Текст программы

Baada ya askari kuwa wamemsulubisha Yesu, viongozi wa Kiyahudi wasioamini walimwambia Pilato, "Yule Muongo, Yesu, alisema angefufuka baada ya siku tatu. Mtu mmoja lazima alilinde kaburi ili kujihakikishia kwamba wanafunzi wake hawatauiba mwili wake na kusema amefufuka kutoka katika wafu."

Pilato alisema, "Chukueni baadhi ya askari na muhakikishe kaburi limelindwa ipasavyo." Hivyo wakaweka muhuri kwenye jiwe katika mlango wa kuingilia kaburini na kuweka maaskari ili kuhakikisha kwamba hakuna mtu yeyote ambaye angeuiba mwili.

Siku iliyofuata baada ya Yesu kuzikwa ilikuwa ni Sabato, na wayahudi hawakuruhusiwa kwenda kaburini siku hiyo. Hivyo asubuhi na mapema baada ya Sabato, wanawake wengi walijiandaa kwenda kwenye kaburi la Yesu kuupaka mwili wa Yesu marashi ya maziko.

Ghafla, kulikuwa na tetemeko kubwa. Malaika ambaye mng'ao wake ulikuwa kama mng'ao wa mwanga wa radi alitokea kutoka mbinguni. Aliliviringisha mbali lile jiwe lilokuwa limeufunika mlango wa kaburi na kulikalia. Askari waliokuwa wanalilinda kaburi waliogopa sana na kuanguka chini na kuwa kama watu waliokufa.

Wale wanawake walipofika kaburini, malaika aliwaambia. "Msiogope. Yesu hayupo hapa. Amefufuka kutoka katika wafu, kama alivyosema kwamba atafufuka! Angalieni kaburini na muone." Wale wanawake wakaangalia mle kaburini na kupaona mahali mwili wa Yesu ulipokuwa umelazwa. Mwili wake haukuwepo pale!

Malaika akawaambia wale wanawake, "Nendeni na mkawaambie wanafunzi, 'Kwamba Yesu amefufuka kutoka katika wafu na atawatangulia kwenda Galilaya."

Wanawake walijawa na hofu na furaha kuu. Wakakimbia kwenda kuwaambia wanafunzi habari njema.

Wale wanawake walipokuwa wanaenda kuwaambia wanafunzi wake habari njema, Yesu aliwatokea wale wanawake, nao wakamuabudu. Yesu akasema, "Msiogope. Nendeni mkawaambie wanafunzi wangu waende Galilaya.Wataniona huko."

Схожая информация

Free downloads - Here you can find all the main GRN message scripts in several languages, plus pictures and other related materials, available for download.

Аудиотека GRN - Евангелистские и базовые Библейские учебные материалы , присущие людским нуждам и культуре в различных стилях и форматах

Copyright and Licensing - GRN shares it's audio, video and written scripts under Creative Commons

Choosing the right audio or video format - What audio and video file formats are available from GRN, and which one is best to use?