unfoldingWord 48 - Yesu ndiye Masihi aliyeahidiwa

unfoldingWord 48 - Yesu ndiye Masihi aliyeahidiwa

개요: Genesis 1-3, 6, 14, 22; Exodus 12, 20; 2 Samuel 7; Hebrews 3:1-6, 4:14-5:10, 7:1-8:13, 9:11-10:18; Revelation 21

스크립트 번호: 1248

언어: Swahili

청중: General

장르: Bible Stories & Teac

목적: Evangelism; Teaching

성경 인용: Paraphrase

지위: Approved

이 스크립트는 다른 언어로 번역 및 녹음을위한 기본 지침입니다. 그것은 그것이 사용되는 각 영역에 맞게 다른 문화와 언어로 조정되어야 합니다. 사용되는 몇 가지 용어와 개념은 다른 문화에서는 다듬어지거나 생략해야 할 수도 있습니다.

스크립트 텍스트

Mwenyezi Mungu alipoumba ulimwengu, vitu vyote vilikuwa sawa pasipo dosari yoyote. Hapakuwa na dhambi, wala magonjwa, wala kifo duniani. Adam na Mkewe, Eva, walipendana sana na walimpenda Mungu pia. Hivi ndivyo Mwenyezi Mungu alivyokusudia ulimwengu uwe.

Katika bustani ya Edeni, Shetani alijitokeza kama nyoka. Akazungumza na Eva kwa lengo la kumdanganya. Kwa njia hiyo, Adam na Eva wakawa wamemtenda Mungu dhambi, na leo watu wote duniani tunaweza kuugua na kufa kama matokeo ya dhambi.

Jambo jingine la hatari zaidi likajitokeza kama matokeo ya dhambi ya Adam na Eva. Uhusiano wao na Mungu ukaharibika na toka wakati huo, kila mwanadamu anazaliwa akiwa na asili ya dhambi, akiwa hana mahusiano mazuri na Mwenyezi Mungu. Hata hivyo, Mwenyezi Mungu akawa na mpango wa kurejesha uhusiano ulioharibiwa na dhambi baina ya mwanadamu na Mungu.

Kupitia mpango huo, Mwenyezi Mungu aliahidi kuwa mmoja wa wazaliwa katika uzao wa Eva atakiponda kichwa cha shetani, na shetani atakigonga kisigino chake. Maneno haya yana maana kwamba, shetani atamuua Masihi, lakini Mwenyezi Mungu atamfufua tena, na kisha huyo Masihi atazishinda nguvu za shetani milele. Baada ya miaka mingi kupita, Mwenyezi Mungu akaudhihirishia ulimwengu kuwa Yesu ndiye Masihi.

Katika siku zile Mwenyezi Mungu alipouangamiza ulimwengu kwa mafuriko, aliandaa chombo cha kuwaokoa na gharika hilo watu wote waliokuwa wanamwamini. Kwa sababu ya dhambi, ni kwa namna iyo hiyo, watu wote duniani wanastahili kuangamizwa. Lakini ashukuriwe Muwenyezi Mungu aliyemtoa Yesu kumuokoa kila mtu anayemwamini.

Katika kipindi cha mamia ya miaka, makuhani wakadumu katika kutoa sadaka za kuteketezwa, wakidhihirisha aina ya adhabu iliyowapasa kupewa kwa ajili ya dhambi zao. Hata hivyo, sadaka hizo hazikuweza kabisa kuwaondolea dhambi zao. Hivyo, Yesu ndiye kuhani mkuu asiyelingana na makuhani wengine. Yeye alijitoa nafsi yake mwenyewe ili awe sadaka ya pekee ya kuteketezwa kwa ajili ya kuziondoa dhambi za watu wote duniani. Yesu ndiye kuhani mkuu wa kweli maana alibeba adhabu ya dhambi iliyotendwa na watu wote.

Ndipo Mwenyezi Mungu akazungumza na Ibrahimu akamwambia, "Kupitia wewe Ibrahimu, watu wa kila kabila duniani wamebarikiwa." Naye Yesu alitokana na uzao wa Ibrahimu, na watu wa kila namna wanabarikiwa kupitia Ibrahimu. Hivyo, kila anayemwamini Yesu ameokolewa kutoka katika dhambi, na anafanyika kuwa uzao wa Ibrahimu kwa jinsi ya kiroho.

Mwenyezi Mungu alipomwagiza Ibrahimu kumtoa mwanae, Isaka, kama sadaka ya kuteketezwa na akatii, Bwana Mungu akampatia Ibrahimu mwana kondoo achinjwe na kutolewa sadaka badala ya mwanae, Isaka.Hii inatufundisha kuwa sisi sote tunastahili kufa kwa ajili ya dhambi zetu. Lakini Mwenyezi Mungu amemtoa Yesu, mwanakondoo wa Mungu ili atolewe kama sadaka na kisha kufa badala yetu.

Hata Mwenyezi Mungu alipoamuru mapigo saba katika nchi ya Misri, aliagiza kila familia ya kiisraeli kuchinja mwana kondoo asiye na kasoro na kisha kunyunyiza damu ya kondoo juu na chini ya miimo ya milango yao. Na ndipo Mwenyezi Mungu alipoiona damu katika miimo ya milango yao, aliziruka nyumba zile na hakuwauwa watoto wao wa kiume wa kwanza .Tendo hilo linajulikana kama pasaka.

Yesu hakuwa na kosa wala dhambi yoyote na aliuawa katika kipindi cha maazimisho ya pasaka. Hakika Yesu ndiye mwanakondoo wetu wa pasaka. kwa yeyote anaemwamini Yesu, damu yake Yesu hulipia dhambi za mtu huyo na adhabu ya Mungu humruka mtu huyo.

Ni kweli kuwa Mwenyezi Mungu alifanya agano na watu wake, taifa la Israel. Bali sasa Mwenyezi Mungu anafanya agano lililo wazi kwa kila mtu. Kwa sababu ya agano hili jipya, watu wote wa kila mahali, wanaweza kuwa sehemu ya watu wa Mungu kwa kumwamini Yesu Kristo.

Japokuwa Musa pia alikuwa ni nabii mkubwa aliyetangaza neno la Mungu, Yesu ndiye nabii mkuu zaidi ya manabii wote.Kila jambo alilolifanya na kulisema Yesu lilikuwa ni tendo na neno la Mungu kwakuwa yeye ni Mungu. Ndio maana wakati mwingine Yesu anaitwa neno la Mungu.

Mungu alimuahidi mfalme Daudi kuwa mmoja ya wazaliwa wake atawatawala watu wa Mungu milele. Kwakuwa Yesu ni mwana wa Mungu na Masihi, yeye ndiye yule mzaliwa wa uzao wa Daudi atakayetawala milele.

Daudi alikuwa mfalme wa Israeli, lakini Yesu ni mfalme wa ulimwengu wote. Atarudi tena kuutawala ufalme wake kwa haki na amani milele.

관련정보

생명의 말씀 - GRN 은 성경에 기반한 구원과 그리스도인의 삶에 대한 수천개의 오디오 복음 메시지를 가지고 있습니다.

무료 다운로드 - 여기에서 다운로드 가능한 여러 언어로 된 주요 GRN 메시지 스크립트, 그림 및 기타 관련 자료를 찾을 수 있습니다.

GRN 오디오 도서관 - 전도와 기본 성경 가르침을 위한 자료는 mp3, CD, 카세트 테이프 형태로 사람들의 필요와 문화에 맞추어졌습니다. 녹음은 성경이야기, 전도 메시지, 말씀 읽기, 노래를 포함하여 다양한 스타일로 구성되었습니다.

Copyright and Licensing - GRN shares it's audio, video and written scripts under Creative Commons

Choosing the right audio or video format - What audio and video file formats are available from GRN, and which one is best to use?